Aua watoto watatu wa mke mdogo kisa wanapendwa zaidi

Aua watoto watatu wa mke mdogo kisa wanapendwa zaidi

Mstahiki Mea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
5,581
Reaction score
10,110
Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Wende Luchagula (30) mkazi wa kijiji cha Milonji kata ya Lusewa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, anadaiwa amewaua watoto watatu wa mke mwenzie kwa kuwachinja na kitu chenye ncha kali shingoni kwa madai kuwa mumewe anampenda zaidi mke mdogo pamoja na watoto hao kitendo ambacho hakimpendezi.

Inaelezwa kuwa tukio hilo limetokea Julai 12, 2025 majira ya saa nane mchana huko katika kijiji cha Milonji kata ya Lusewa wilayani humo ambapo mtuhumiwa alivizia mumewe akiwa ametoka pamoja na mke mdogo kisha akatekeleza tukio hilo la mauaji.

Aidha watoto waliouawa na mama huyo wametajwa kwa majina yao kuwa ni Lugola Samweli (06), na mapacha ambao ni Kulwa Samweli na Doto Samweli wenye umri wa miezi (08).

Hata hivyo Jeshi la Polisi mkoa wa Ruvuma limethibitisha kumshikilia mwanamke huyo kwaajili ya taratibu za kisheria na uchunguzi zaidi.
 
Alooo jamani

Tuendelee kuomba ndugu zangu tunaelekea kubaya sana, unyama umekuwa mwingi sana ndugu zangu

Wapumzike kwa amani hawa watoto wadogo
 
Jinga sana huyo maza. Aliyetakiwa kuuliwa ni baba watoto🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️
 
Badala ya kupambana na mume wake kawaua watoto wasio na kosa. Na watoto wake sasa watauona moto, nao watatumikia adhabu ya makosa yake. Hii ni dhulma kubwa sana kwa watoto.
 
Hawa jamaa wanazaliana kuliko hata wale wa im proud to be…..
Kifupi miaka ya 2050 katika kila watu 3 mmoja atakua msukuma.

Hongereni sana mashemeji zangu nchi inajengwa na watu.

Msi merge uzi wangu
 
Nasikia Mzee mkapa aliwasafirisha Hadi mtwara kule wakalime na uzalishaji ili kuilisha mtwara coz wanamtwara eti wamejaa uswahili na hawataki kuchapa kazi sana kama wasukuma!!
 
JESHI la Polisi Mkoa wa Ruvuma linamshikilia Wende Luchagula, Miaka 30, Kabila Msukuma, Mkazi wa Kijiji cha Milonji kwa kosa la mauaji baada ya kuwachinja watoto wa mke mwenzake watatu mpaka kufa.Tukio hilo limetokea Julai 12, 2025 majira ya saa nane mchana huko Kijiji cha Milonji, Kata ya Lusewa, Wilaya ya Namtumbo ambapo mtuhumiwa alivizia mume wake na mama mzazi wa watoto hao ambaye ni mke mdogo wakiwa wameenda mnadani kisha akatekeleza tukio hilo la kuwachinja watoto watatu kati yao wawili wakiwa mapacha ambao ni Lugola Lutelemula Samweli (6), Kulwa Lutelemula Samweli, Umri miezi 8 na Doto Lutelemula Samweli Umri Miezi 8, wote wakazi wa Kijiji cha Milonji chanzo kikiwa ni wivu wa mapenzi.Akizungumza na vyombo vya habari kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma SACP- Marco Chilya amesema, mume wa mtuhumiwa huyo alikuwa ameoa wake watatu lakini alikuwa akimpenda zaidi mke mdogo na Watoto wake kitendo ambacho mtuhumiwa hakukipenda ndipo akavizia mume wake na mama mzazi wa watoto hao ambaye ni mke mdogo wakiwa wameenda mnadani kisha akatekeleza tukio hilo la kikatili la kuwa chinja watoto hao mpaka kufa.Miili ya marehemu imekabidhiwa kwa familia kwa ajili ya taratibu za mazishi. Mtuhumiwa amekamatwa kwa hatua zaidi za kisheria.


Taarifa ya Maulid Kitenge.
 
Karibu huku Nambendo-Songea tunawafundisha wenyeji kulima mpunga.
 
Hhga Hilo halina shaka, jamaa niwatu wachangamfu sana,
Sio Ruvuma tu mpaka uko vijiji vya Lind wamejqzana
 
Back
Top Bottom