MSHINO
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 1,069
- 713
Wana jamii tangu maandalizi ya Christmas na mwaka mpya yaanze, polisi wa usalama barabarani wameamua kuweka kambi kwenye daraja dogo pale karibu na JKT makao makuu mlalakua, askari hawa wanachukua pesa (RUSHWA) bila hata aibu.
Kila gari wamekuwa wakichukua Tzs 5000/= mpaka 10,000/= hakuna dereva anayeandikiwa/kutozwa fine. Wakikukamata wanadai kukuandikia fine kulingana na idaidi ya makosa, lakini hawatozi fine mtu watakwambia uchague fine ya TRAFFIC au ya SUMATRA.
SWALI: Je tume ya kupambana na kuzuia rushwa TAKUKURU wako wapi? Inatia aibu kuona polisi wetu wakichukua rushwa wazi wazi hata kwa wageni kutoka nje ya nchi.
Jana nilishuhudia mzungu mmoja akitoa shilingi 5,000/= ya rushwa, sikujua alikuwa na kosa gani. Tunaomba TAKUKURU wafanye kazi yao, kwaani kuwakamata ni rahisi sana, wachukue gari wakifika pale wajifanye wana wasi wasi kutaka kurudi baada ya waendelee, lazima polisi watawakamata na kuombwa rushwa.
Serikali inapoteza mapato huku askari hawa wakijipatia fedha nyingi kwa njia isiyo halali.
Kila gari wamekuwa wakichukua Tzs 5000/= mpaka 10,000/= hakuna dereva anayeandikiwa/kutozwa fine. Wakikukamata wanadai kukuandikia fine kulingana na idaidi ya makosa, lakini hawatozi fine mtu watakwambia uchague fine ya TRAFFIC au ya SUMATRA.
SWALI: Je tume ya kupambana na kuzuia rushwa TAKUKURU wako wapi? Inatia aibu kuona polisi wetu wakichukua rushwa wazi wazi hata kwa wageni kutoka nje ya nchi.
Jana nilishuhudia mzungu mmoja akitoa shilingi 5,000/= ya rushwa, sikujua alikuwa na kosa gani. Tunaomba TAKUKURU wafanye kazi yao, kwaani kuwakamata ni rahisi sana, wachukue gari wakifika pale wajifanye wana wasi wasi kutaka kurudi baada ya waendelee, lazima polisi watawakamata na kuombwa rushwa.
Serikali inapoteza mapato huku askari hawa wakijipatia fedha nyingi kwa njia isiyo halali.