Atheists tulionekana wa ajabu sana!

Umeshindwa kuthibitisha origin ya mwanadamu nenda kawaambie na atheist wanzako..paka mpate jibu hapa.. Ndio mje hapa tuendelee na point zingine..hahaha
We umeweza kuthibitisha mletaji wa mungu?

Nilikuuliza swali

Ili kitu kiwepo kuna ulazima wa mletaji naye kuwepo?

Ukajibu ndiyo

Nikakuuliza kipi kilichomleta huyo mungu mpaka akawepo ulijibuje?
 
Kushindwa kwa mwanadamu kuelezea origin yake mwenyewe au hata origin ya ngombe au ndege au universe ..ni ushahidi ulitukuka kua Mungu yupo yu hai..Amen
We umeweza kuthibitisha mletaji wa mungu?

Nilikuuliza swali

Ili kitu kiwepo kuna ulazima wa mletaji naye kuwepo?

Ukajibu ndiyo

Nikakuuliza kipi kilichomleta huyo mungu mpaka akawepo ulijibuje?
 
mabaya
[/QUOT
Unamkataa Mungu kwa sababu huoni uwezo na nguvu zake hazifanyi dunia na watu kuwa na furaha. Kwamba Mungu anashindwa kufanya dunia na wanadamu wasiwe na matatizo.
Ili kujua nguvu na uwezo wa Mungu katika nyakati zetu nakuomba ujifunze: kwanini Mungu alimuumba mtu? Ukishaelewa mwanadamu kaumbwaje na kwa ajili ya mini ndiyo utaweza kuelewa uwezo na nguvu ya Mungu.
Hatahivyo, kuhusu ulimwengu, dunia na watu wasio/usio/isio na matatizo ndivyo itakuwa. Ili kujua haya yote jifunze na kuelewa Mungu ni nani na nini? Jifunze kwanini alimwumba mwanadamu.
 
Hahahaaa!!,
Wanadamu hupotea katika njia panda za fikra Zao.

Nmefurahishwa na jinsi unavyojieleza na kutaja wafuasi wa Mrengo wako. Kitu pekee ninachoweza kukwambia ni kuwa kila Swali litajibiwa. Ikiwa utataka majibu.

Ukiujua ukweli utakuweka huru, Nao ukweli ni nini basi?

Ukweli ni kumjua asiyekuwepo kwa mambo yaliyopo. Kumtafuta kwa bidii zote kwa akili aliyokupa. Ukweli hauji kwa kumpinga Asiyekuwepo katika njia panda ya Fikra za nyama.

Basi Nakusihi,, angalia sana katika siku zako, siku za mapito zako. usije ukajipoteza kwa yaliyopo machoni pako nawe ukakosa yasiyokuwepo katika macho yako na Akili yako ambayo katika hayo ndio asili ya roho yako.
Mwenye masikio na macho na asikie na kusoma neno hili
 
Unamkataa Mungu kwa sababu huoni uwezo na nguvu zake hazifanyi dunia na watu kuwa na furaha. Kwamba Mungu anashindwa kufanya dunia na wanadamu wasiwe na matatizo.
Ili kujua nguvu na uwezo wa Mungu katika nyakati zetu nakuomba ujifunze: kwanini Mungu alimuumba mtu? Ukishaelewa mwanadamu kaumbwaje na kwa ajili ya mini ndiyo utaweza kuelewa uwezo na nguvu ya Mungu.
Hatahivyo, kuhusu ulimwengu, dunia na watu wasio/usio/isio na matatizo ndivyo itakuwa. Ili kujua haya yote jifunze na kuelewa Mungu ni nani na nini? Jifunze kwanini alimwumba mwanadamu.

Kwanza kabisa, jifunze kunukuu hapa JF. Maana, kwa jinsi ulivyoninukuu hapo juu mtu anaweza kufikiri maneno hayo yako hapo juu nimeandika mimi. Hilo la kwanza.

Pili, umeandika "Unamkataa Mungu kwa sababu huoni uwezo na nguvu zake hazifanyi dunia na watu kuwa na furaha."

Hujanielewa, hii si sababu yangu ya kumkataa Mungu.

Na kama hujaelewa sababu yangu ya kukataa uwepo wa Mungu, huwezi kuipinga.

Hapo juu unaelezea kitu tofauti kabisa na sababu yangu ya kupinga dhana ya kuwepo Mungu.

Rudia kunisoma, unielewe kwa nini napinga dhana ya uwepo wa Mungu.

Kama hujaelewa, niulize tu "Kwa nini unapinga dhana ya kuwepo kwa Mungu, kama umeikataa sababu hii niliyoitoa, sababu yako ni ipi?".

Nitakusaidia uielewe sababu yangu, na ukiielewa tutaweza kujadiliana vizuri zaidi.

Kwa sasa hatuwezi kujadiliana vizuri, kwa maana, hata sababu ya pingamizi langu hujaielewa.
 
Mimi nimeelewa vema pingamizi lako. Unadai kwamba, Mungu mwenye uwezo na nguvu, maarifa na ujuzi kwanini aumbe dunia yenye matatizo?
Mwanzoni nilikujibu kwanza ujielimishe juu ya dunia, ulimwengu, mwanadamu na matatizo ni nini? Nilikuomba kwamba jifunze na uelewe kwanza vitu hivyo kama kweli wewe ni mtu makini na unafikira za kutaka kujifunza.
Pili, nikakuomba ujifunze na uelewe juu ya Mungu ni nini na nini? Nakaendelea kusema, kwamba, jifunze na kuelewa kwanini Mungu alimwumba mwanadamu na alimwumbaje?
Kando na hapo, nikakuomba ujielimishe kuhusu ubongo wa mwanadamu unavyofanya kazi. Hapa kimsingi nilizungumza juu ya kutumia hisia kupima na kuelewa mambo.
Lakini pia, nikasema kwamba iko nafasi kubwa sana hauna ushahidi wa kisayansi ambao wewe unadai unathibitisha malalamiko yako juu ya kutokuwepo Mungu, lakini umezingatia hoja za watu engine ambazo hujaweza kuzifanyia utafiti kujua ukweli wa madai hayo.
Kwa mantiki hiyo, hija yako haitazami eneo lingine ispokuwa kwamba Mungu mwenye nguvu na uwezo wote na huruma na upendo alishindwaje kuumba ulimwengu usio na matatizo na badala yake ni kinyume chake? Hoja yako siyo kwa sababu inaelekea pekee Mungu na jinsi mambo unavyoyaona, lakini kwasababu unaelewa vibaya Mungu ni nani na nini.
Naweza kukujibu kwa kukuomba utafakati mfano huu: maji ni muunganiko wa elementi ya haidrojeni na oksijeni. Hivyo ndivyo ilivyo katika sayansi, lakini jambo hilo ukimweleza mtu asiyefahamu hawezi kukuelewa na atakuwa na maswali mengi.
Lakini kama wewe humwoni Mungu kama ambavyo mafundisho ya dini sahihi yanavyofundisha, basi wewe unamwona nani? Na kwanini unamwona huyo? Lakini pia kwa mwelekeo huo unaouchukua, maana yake unayaona matatizo ndiyo yenye nguvu, uwezo, maarifa na ujuzi kamili na kwa maana hiyo, matatizo ni zaidi ya mwanafamu.
 
Kwa sababu dini hizi zililetwa na wageni ili kurahisisha kututawala.
KAMA WALITUTAWALA UNADHANI WALILETA DINI NZURI?
Haohao walioleta makanisa na misikiti, leo wanasema wanaume tuoane, wanasema si lazima kuvaa nguo. Yaani wanakana mafundisho yao wenyewe. Ya nini kuwaamini?
Hao watu unaowazungumzia wameleta dini tu hawakuleta vitu vyengine? kama wameletq na vitu vyengine kwanini kama tunataka kuacha mambo ya kuletewa tusiache yote ?
 
Mimi nimeelewa vema pingamizi lako. Unadai kwamba, Mungu mwenye uwezo na nguvu, maarifa na ujuzi kwanini aumbe dunia yenye matatizo?
Mwanzoni nilikujibu kwanza ujielimishe juu ya dunia, ulimwengu, mwanadamu na matatizo ni nini? Nilikuomba kwamba jifunze na uelewe kwanza vitu hivyo kama kweli wewe ni mtu makini na unafikira za kutaka kujifunza.
Pili, nikakuomba ujifunze na uelewe juu ya Mungu ni nini na nini? Nakaendelea kusema, kwamba, jifunze na kuelewa kwanini Mungu alimwumba mwanadamu na alimwumbaje?
Kando na hapo, nikakuomba ujielimishe kuhusu ubongo wa mwanadamu unavyofanya kazi. Hapa kimsingi nilizungumza juu ya kutumia hisia kupima na kuelewa mambo.
Lakini pia, nikasema kwamba iko nafasi kubwa sana hauna ushahidi wa kisayansi ambao wewe unadai unathibitisha malalamiko yako juu ya kutokuwepo Mungu, lakini umezingatia hoja za watu engine ambazo hujaweza kuzifanyia utafiti kujua ukweli wa madai hayo.
Kwa mantiki hiyo, hija yako haitazami eneo lingine ispokuwa kwamba Mungu mwenye nguvu na uwezo wote na huruma na upendo alishindwaje kuumba ulimwengu usio na matatizo na badala yake ni kinyume chake? Hoja yako siyo kwa sababu inaelekea pekee Mungu na jinsi mambo unavyoyaona, lakini kwasababu unaelewa vibaya Mungu ni nani na nini.
Naweza kukujibu kwa kukuomba utafakati mfano huu: maji ni muunganiko wa elementi ya haidrojeni na oksijeni. Hivyo ndivyo ilivyo katika sayansi, lakini jambo hilo ukimweleza mtu asiyefahamu hawezi kukuelewa na atakuwa na maswali mengi.
Lakini kama wewe humwoni Mungu kama ambavyo mafundisho ya dini sahihi yanavyofundisha, basi wewe unamwona nani? Na kwanini unamwona huyo? Lakini pia kwa mwelekeo huo unaouchukua, maana yake unayaona matatizo ndiyo yenye nguvu, uwezo, maarifa na ujuzi kamili na kwa maana hiyo, matatizo ni zaidi ya mwanafamu.
Tatizo unaambiwa hujaelewa, hata kabla ya kuuliza hujaelewa wapi, unajibu umeelewa.

Kwa msingi huo, sio tu hujaelewa, huna hata utashi wa kuelewa.

Unakimbilia kujiona umeelewa bila ya kuwa na utashi wa kuuliza "sijaelewa wapi?" ueleweshwe vizuri.
 
Your question is a non sequitur.

Nikishindwa kuthibitisha origin ya mtu hilo ndilo linathibitisha Mungu yupo?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
Hivi toka lini kitu kisichokuwepo kikajadilika au kujulikana? Kila mara mnasema Mungu hayupo,sasa hili neno Mungu mmelitoa wapi???

Kitu kisichokuwepo kina maana hakijulikani!
 
Hivi toka lini kitu kisichokuwepo kikajadilika au kujulikana? Kila mara mnasema Mungu hayupo,sasa hili neno Mungu mmelitoa wapi???

Kitu kisichokuwepo kina maana hakijulikani!
Kama kitu kisichokuwepo hakijulikani, wewe umejuaje hakijulikani?

Unajua kujua kitu hakijulikani ni kujua?

Unajua ukisema umejua kitu hakijulikani unaji contradict kwa sababu ukishajua kitu hakijulikani umeshajua hicho kitu na hakiwezi tena kuwa hakijulikani?

Unajua kitu kinaweza kutajwa kwa hadithi tu, bila kuwapo?

Unajua characters wa hadithi za kutunga kina James Bond, Willy Gamba, Kipepe, Ndumilakuwili, Lodi Lofa, Madenge, etc wanajulikana lakini hawapo kiukweli nje ya hadithi?

Sasa mtu akikwambia Mungu naye ni character wa hadithi tu kama hao, na kiukweli hayupo, utasema kwa vile Willy Gamba kaandikwa kwenye hadithi za Aristablus Elvis Musiba, utasema ni lazima yupo vile vile, kwa sababu huwezi kufikiria kitu ambacho hakipo?
 
binafsi napinga. hizi ni nadharia za falsafa katika mwelekeo wa kuwaaminisha watu vitu vya kufikirika tu
umewai kuangalia historia za kwel nje ya vitabu vya dini/?/ hata za mwaka 200 bc?// au je kwann tunatumia bc kuwakilisha miaka..???
 
umewai kuangalia historia za kwel nje ya vitabu vya dini/?/ hata za mwaka 200 bc?// au je kwann tunatumia bc kuwakilisha miaka..???
Ndiyo, kimsingi zina ushahidi katika maisha ya sasa.
Lakini unaposema mungu yupo wakati wakat hata picha ya the so called God sijawahi kuiona.
Halafu mfumo wa dini umekaa kiunyonyaji fulani coz kila ibada ni kupeleka sadaka lakini hata siku moja sijawahi kuona kuna zawadi toka kwa mungu zaidi ya jasho langu
 
Ndiyo, kimsingi zina ushahidi katika maisha ya sasa.
Lakini unaposema mungu yupo wakati wakat hata picha ya the so called God sijawahi kuiona.
Halafu mfumo wa dini umekaa kiunyonyaji fulani coz kila ibada ni kupeleka sadaka lakini hata siku moja sijawahi kuona kuna zawadi toka kwa mungu zaidi ya jasho langu

Hi ni fursa tu wajanja waliigundua kupiga hela
 
Huoni hayo yanatokana na kukiuka amri za Mungu. Binadamu asingekiuka amri za Mungu mabaya yangetoka wapi?(rejea amri kumi za Mungu)
Mabaya yameletwa na binadamu mwenyewe na siyo Mungu.
Magonjwa, vifo, wapendanao kutengana, ujinga, njaa, majanga ya kiasili, uonevu, wizi na mengine yanayofanana na hayo.

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao haya hayawezekani?
 
Huoni hayo yanatokana na kukiuka amri za Mungu. Binadamu asingekiuka amri za Mungu mabaya yangetoka wapi?(rejea amri kumi za Mungu)
Mabaya yameletwa na binadamu mwenyewe na siyo Mungu.
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo, na si hadithi za watu tu?
 
Ndiyo, kimsingi zina ushahidi katika maisha ya sasa.
Lakini unaposema mungu yupo wakati wakat hata picha ya the so called God sijawahi kuiona.
Halafu mfumo wa dini umekaa kiunyonyaji fulani coz kila ibada ni kupeleka sadaka lakini hata siku moja sijawahi kuona kuna zawadi toka kwa mungu zaidi ya jasho langu
bro hujanijibu swali../
je kwann tunatumia bc kuwakilisha miaka..???
 
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo, na si hadithi za watu tu?
Wewe aliyekwambia hizi ni hadithi za watu ni nani? Hivyo vitabu vya wanasayansi unavyotumia kupinga uwepo wa Mungu ni nini kama si hadithi zao pia?

Kama Mungu hayupo hilo neno Mungu umelitoa wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom