Atheist wengi hawajui wanachokitafuta

Allaha katika Quran ametwambia ivi:

4:124. "Na anaye fanya mema, akiwa mwanamume au mwanamke, naye ni Muumini - basi hao wataingia Peponi wala hawatadhulumiwa hata kadiri ya tundu ya kokwa ya tende."
sasa hii ina uhusiano gani na kuonana na Mungu??ukiwa hapa duniani?
 
sasa hii ina uhusiano gani na kuonana na Mungu??ukiwa hapa duniani?
Hatujaja duniani kumuona Mungu, tumeletwa duniani kufanya mema ili tuingizwe peponi, huko tutatapata majibu ya maswali yote unayoyajua na usiyoyajua, huko ndio tutayajua yote kinaga ubaga.
 

Unajibu kwa kukurupuka hujui hata mantiki ya hilo swali nililokuuliza na sizani kama umelielewa

Mimi sijazungumzia kubadilika kwa maono au lah, na ndio maana nilikua nasisitiza kuuliza kua kama naye anatabia ya kukosea ili niweze kujenga hoja kupitia jibu utalonipa

Nimeuliza kama mungu anajua kila kitu na hakuna kitu utachokifanya leo hii kikawa kigeni machoni mwake kwasababu yeye ni mungu asiyekosea alichokiona ni lazima kiende sawa sawa. Sasa wewe leo hii ukiamua kutoenda kanisani au msikitini utakua umebadilisha chochote katika ujuzi wake kuhusu hatma yako???
 

Mungu akijua kua utaenda motoni, wewe ukiwa unafanya ibada kwasababu hujui alilolipanga mungu juu yako hakubadilishi chochote
 
Huyo Mungu hawezi kujitetea mwenyewe mpaka wewe ukauke sauti humu !!!
Kwani mbona wewe unatokwa mishipa humu kusema hakuna Mungu kwani kama kitu hakipo si hakipo na kila mtu anaona kiwa kweli hakipo sasa kuna haja gani wewe kutwa kubishana na watu kuwa hakuna Mungu?
 
Unaweza kuwa muaminii Mungu kwa sababu umezaliwa na kukuzwa na hiyo imani ya Mungu kama ambavyo huko china au korea watu wengi huzaliwa na kukuzwa na hali ya kutokuwa na imani ya dini wala Mungu,hivyo kwao hawaamini Mungu kwa sababu ndivyo walivyo lelewa hadi kukulia katika mazingira hayo.

Hivyo suala la atheists kwamba walikuwa wakiamini Mungu mwanzoni si jambo la kuwafanya kuwa wana hoja za msingi maana wapo pia wanaomini Mungu sasa ambao nao walikuwa atheists hivyo kungekuwa na hoja za msingi basi wasingeacha huo msimamo na kuja kuamini uwepo wa Mungu.

Tatizo watu wangekubali kuwa suala la uwepo wa Mungu ni imani hivyo tungejadili kwa kuangalia sababu za msingi zenye kuwapelekea watu kukubali imani ya uwepo wa Mungu basi tungepiga hatua kwenye hii mijadala.
 

Tatizo ndo hilo, kila kitu mnaishia kusema imani, ukweli ni kua watu mpo dini flani kwankua mlizaliwa huko, exactly kama ulivyosema, inakua ngumu kuacha kitu ambacho ulikua brain washed toka utotoni. Miungu ipo zaidi ya 3,000 na mingi inapingana hehehe anayeamini wa kwake ndiye wa kweli anajidanganya.
Mungu kama yupo basi kafeli, yeye kila kitu analaumu shetani tu huku kamtengeneza mwenyewe hehehe mara mia niamini Thor. Ukweli ni kua hakuna mwenye proof yoyote ile ya uwepo wa mungu, tutaongea wee miaka nenda rudi hajawahi prove mtu hata moja, hata vitabu vya dini ni ambiguous mno. Total waste of time nafurahi sana niliachana na huo upuuzi
 
Sio tunaishia kusema tu bali huo ndio ukweli kwamba suala la uwepo wa Mungu ni jambo la imani,tusipoelewana hapa huko hakuna kitakachoeleweka na ndiyo maana unakuja na za et hakuna proof ya uwepo wa Mungu kitu ambacho inaonesha tatizo ninalolisema hapa. Kuna watu walikuwa kama wewe wenye misimamo ya kuwa Mungu hakuna na hakuna proof ya uwepo ila sasa wamekubali uwepo wa Mungu na si kwamba walipata proof ya uwepo wa Mungu.

Kwahiyo mie mtu kama wewe unayejiona uko sahihi kwa huko kwako kusema hakuna Mungu naona kawaida tu najua ni misimamo tu kama ambayo wengine walikuwa nayo na sasa wamebadili,na si kwamba una sababu au hoja za msingi sana maana ingekuwa basi tusingeona watu kama nyie kuja kukubali uwepo wa Mungu bila hata proof. Ukweli ni kwamba wote sie(waamini Mungu na wakana Mungu) misimamo tuliyonayo ni zaidi ya hoja tunzotoa hapa,na ndiyo wewe unaona sawa tu kwamba hakuna Mungu na kuona ajabu inakuje wengine hawaoni unachokiona wewe na wengine pia tunaona hivyohivyo ni vp mtu inawezekana kusiwe na Mungu na vp wewe unashindwa kuona dalili na sababu za uwepo wa Mungu? Na ndiyo maana si ajabu atheist kuja kuamini Mungu na muamini Mungu kuja kuwa atheist ni kawaida tu.
 
Sijaona swali la kiranga lisilojibika. Kikubwa ni kwamba yeye hajibu maswali ukimuuliza.
mfano mkuu ukiulizwa kwanini Mungu ameamua kujificha kabisa na hakuna ambaye amewahi kumuona.

Hilo ni moja ya swali la.kiranga

Hebu tupe wewe jibu sahihi sio tu ujibu swali tupe jibu sahihi na uthibitishe pia mkuu

Note : am not an atheist
 
So kuna allah

So Mungu wetu sisi wakristo si wa kweli

Mambo kama haya ndo hufanya wakina kiranga kutuona sisi waamini Mungu watu tusiojitambua

Tukianza kutetea uwepo wa Mungu tunaungana

Ila sasa baada ya hapo utasikia mkristo ni kafiri

What the fvck !
 
Hapa wakristo na waislamu tutaungana subiri baadae

Aisee ... Hizi issue ni complicated sana ukubali au ukatae

Nashangaa sana ani .. Tunatumia Nguvu nyingi kumtetea mtu ambaye hajaokba tumtetee

Hivi ni wapi aliwahi tuombe tumthibitishe kama yupo
 
Uzi ni mzuri lakini hauna uhalisia
Mtu anaamini Mungu ni mjuzi wa kila kitu ila et kuna watu Mungu hajui hatima zao kwa sababu hao watu hawajajikabizi kwake hivyo Mungu hajui hatima zao,sasa hapo utasemaje Mungu anajua kila kitu!
 
Duh hatari sana mkuu
 
Matendo mema sio tafsiri ya uwepo wa Mungu.

Ipo hivi, uwepo wa Mungu ni project kama ilivyo project ya kuweka mipaka na kugawa majina yaa nchi.
Au kama ilivyokua project ya kuunda herufi na kuzipa majina
Au kama ilivyokua project ya kuunda namba na mengi kadharika.

Ukiangalia lengo la hayo yote, ilikua ni kuifanya dunia iishi kwa utamaduni mmoja.

Nitaendelea....
 
Kwanin uamin Allah na sio ng'ombe
 
mfano mkuu ukiulizwa kwanini Mungu ameamua kujificha kabisa na hakuna ambaye amewahi kumuona.

Hilo ni moja ya swali la.kiranga

Hebu tupe wewe jibu sahihi sio tu ujibu swali tupe jibu sahihi na uthibitishe pia mkuu

Note : am not an atheist
Safi sana...Sasa Wewe ni Free thinker
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…