Athari za kulazimisha mahusiano

Athari za kulazimisha mahusiano

Sinoni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
7,044
Reaction score
12,526
Penda unapopendwa, usipopendwa stress zinatosha.Ni ukweli kuwa wanaume tulio wengi tumekuwa ving'ang'anizi kwenye suala la mapenzi. Kwa kulazimisha huko kumepelekea baadhi ya wanaume kuingia kwenye mlango wa kifo, kukata tamaa, kujishusha thamani n.k.

Kulazimisha penzi kumekuwa na athari kubwa za moja kwa moja kuliko faida tulizozitarajia hapo awali.Mwanamke ni kiumbe dhaifu pale tu unapomtongoz na kukukatalia zaidi ya mara 4 na ya 5 akakukubalia lazima utambue huo uamuzi wake ni wa kujilazimisha na si wa hiari yake.

Wote tunajua mwanamke mwerevu hawezi kumkubali mwanaume kirahisi, ila kuna kule kuona wazi anasisitiza kitu kuwa hakutaki na pia hakupendi.Mwanamke wa kulazimisha badala ya kukuita honey, baby, mpenzi yeye atakomaa na jina lako halisi na ukihoji atakwambia si lazima "nikuite bby" kwani we mtoto.

Kwa misingi hiyo mwanaume unategemea nini hapo zaidi ya kuingia kwenye ulingo wa penzi la mateso.Huyo mwanamke naye jua akipata ampendaye hatokwambia ila ukweli ukiujua utakuwa ndiyo mwisho wa penzi lako na kuanza kuishi maisha ya kuteswa na mapenzi na wivu usio na mipaka.

Kama ni mwanafunzi haijalishi ulikuwa kichwa hapo kuanguka kitaaluma ni muhimu.kama ni mwajiriwa basi ajira yako itakuwa shakani kwa kuwaza mateso ya penzi kuliko kazi mwisho nikuachishwa kazi.Kama ndo Mfanyabiashara huo ndo wakati wa kujuta kwani mapenzi ya pesa yanatumia hadi mtaji kwani utakapokumbuka muda utakuwa umepita na huna namna tena.

Mwisho wa mapenzi ya kulazimisha ni :-

#Kujinyonga . (hehe)
#Kuua bila ridhaa yako.
#Kuwa kichaa wa penzi la mateso (gogo)
#kufilisika kimtaji na kimawazo
kujipiga risasa (Chagga

Onyo mapenzi ni ushawishi na si kulazimishana.
 
PetCash

Unaugua kulazimisha penzi au?
 
Last edited by a moderator:
Very interesting
cc:Vijana wote wa kiume na wa kike,asante kwa ukumbusho kwa hakika utawafaa wenye kuamini
 
PetCash

Unaugua kulazimisha penzi au?

Dunia ni chungu sana once unapoingia kwenye kupenda asiyekupenda ama kuachwa na unayempenda.
Unaweza kufanya mambo ya kukudistract na kusubiri muda uliopangiwa wa maumivu uishe na maisha yaendelee.
That is the only way out. Ukisema utajichunga usipende. U'll never know you are in love until u r in love.
Na hapo inakuwa too late kujizuia kwa sababu ndo ushapenda tena.

My point as u see is, we have no control over these things and we don't blame for things people do when they are...
 
I personally hii thread imenikumbusha mbal sana..i loved a lot bt nothng i get from her..Now am free becoz i realized she dont lov m back!!
 
I personally hii thread imenikumbusha mbal sana..i loved a lot bt nothng i get from her..Now am free becoz i realized she dont lov m back!!

Pole sana mkuu binadamu tunapitia mengi🙂
 
Fact....kupenda usipopendwa ni sawa na kusubiri meli uwanja wa ndege!
 
nilipenda nisipopendwa nilijuta hakuna rangi ambayo sikuiona

pole sana yaliyokusibu , historia liwe somo la kudumu katika maisha yetu ya sasa na ya baadae ..

=========================
hakuna love chini ya jua usiingie kichwa kichwa.
 
Mwanamke mwerevu hawezi kumkubali mwanaume kirahisi....ha ha ha haaaaaaaa
Uerevu ni nini na urahisi ndiyo upi?
Kwanini mtu kama anakupenda na ana akili ya kumuwezesha kutambua analolitaka ambalo pengine ndo liko mbele yake asikubali? Mnapenda complication ,hamjiamini mkipata mlichokitaka mnaona mmepata kirahisi kwa sababu mnajua hamstahili....viumbe wazito sana wanaume wengine!
 
Very interesting
cc:Vijana wote wa kiume na wa kike,asante kwa ukumbusho kwa hakika utawafaa wenye kuamini

Hilo ndilo jibu ni utoto kwenda ujana
sisi tumeshaoa tuna majukumu ya kulea watoto mtaapofika hapo mtaona watoto wanawaunganisha na hakuna mateso hayo
kwani stress za watoto tu zatosha
  • ada ya chekechea
  • malipo ya matibabu
  • chakula tofauti cha watoto
  • mavazi
  • Klinik, uumini wa DINI, malezi kibao
vyote hivyo vinakusubiri huwezi anzisha mapenzi ya kutesana hadi kujipiga risasi km hao wachagga ambao wanaacha kutafuta hela mapenza yatakuja tu
 
Back
Top Bottom