Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
KAMPUNI ya Ndege Tanzania (ATCL), inatarajia kupata ndege nyingine kutoka Misri, baada ya ndege yake kupata ajali ikiwa mkoani Kigoma hivi karibuni. Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi wa ATCL, Paul Chizi, maofisa wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) wanatarajia kwenda Misri kukagua ndege itakayotumiwa na kampuni hiyo kwa ajili ya safari zake nchini.