Assessment kwa walioko field.

Assessment kwa walioko field.

nyamalagala

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2016
Posts
744
Reaction score
675
Amani iwe kwenu wana JF.

Baada ya kusogezwa mbele kwa muda wa kuanza field mwaka huu ambapo ilikuwa ianze tarehe 25/7 ikabidi ziongezwe mbele kwa wiki mbili kutokana na zoezi la uhakiki lililokwamisha ulipwaji wa hela ya field mwaka huu.Tarehe 9/8 ndio tarehe rasmi wanafunzi waliamriwa kuripoti kwenye vituo vya kufanyia field zao.

Kama utani vile watu wameripoti Siku ya jumanne ya wiki iliyopita na ilipofika jumamosi mchana baadhi wakapigiwa simu kuwa wanakuja kuasesiwa Siku ya jumatatu tarehe 15/8. Yaani wamekaa shuleni wiki moja tu lakini Leo wanaambiwa wakae tayari kuasesiwa.

Hayawi hayawi mwisho huwa,Leo jumatatu ni kweli wameasesiwa kama kawaida.Sasa kwa mtindo huu unampimaje mtu kama ameweza kumudu mafunzo kwa vitendo wakati amefika kituoni kwake jumanne kisha jumatano akapewa vipindi,alhamisi akaingia kutambulishwa kisha akapiga pindi kidogo na ijumaa hakuwa na kipindi kisha leo jumatatu unampima kama amemudu kile alichopaswa kukifanya?.

Je kwa hali hii tutafika tunakotaka kufika kweli!.Wakati mwingine taratibu za uendeshaji wa Elimu ndizo huchangia kuiporomosha kwani haiwezekani mtu atarajiwe kukaa field miezi miwili alafu umpime ndani ya wiki moja aliyokaa kituoni kwake.Wakuu mnalionaje hili.

Hawa vijana wametendewa haki kweli kuwapima kabla ya kumaliza walau hata wiki tatu.Naomba kuwasilisha na karibuni kwa michango yenu.
 
Amani iwe kwenu wana JF.

Baada ya kusogezwa mbele kwa muda wa kuanza field mwaka huu ambapo ilikuwa ianze tarehe 25/7 ikabidi ziongezwe mbele kwa wiki mbili kutokana na zoezi la uhakiki lililokwamisha ulipwaji wa hela ya field mwaka huu.Tarehe 9/8 ndio tarehe rasmi wanafunzi waliamriwa kuripoti kwenye vituo vya kufanyia field zao.

Kama utani vile watu wameripoti Siku ya jumanne ya wiki iliyopita na ilipofika jumamosi mchana baadhi wakapigiwa simu kuwa wanakuja kuasesiwa Siku ya jumatatu tarehe 15/8. Yaani wamekaa shuleni wiki moja tu lakini Leo wanaambiwa wakae tayari kuasesiwa.

Hayawi hayawi mwisho huwa,Leo jumatatu ni kweli wameasesiwa kama kawaida.Sasa kwa mtindo huu unampimaje mtu kama ameweza kumudu mafunzo kwa vitendo wakati amefika kituoni kwake jumanne kisha jumatano akapewa vipindi,alhamisi akaingia kutambulishwa kisha akapiga pindi kidogo na ijumaa hakuwa na kipindi kisha leo jumatatu unampima kama amemudu kile alichopaswa kukifanya?.

Je kwa hali hii tutafika tunakotaka kufika kweli!.Wakati mwingine taratibu za uendeshaji wa Elimu ndizo huchangia kuiporomosha kwani haiwezekani mtu atarajiwe kukaa field miezi miwili alafu umpime ndani ya wiki moja aliyokaa kituoni kwake.Wakuu mnalionaje hili.

Hawa vijana wametendewa haki kweli kuwapima kabla ya kumaliza walau hata wiki tatu.Naomba kuwasilisha na karibuni kwa michango yenu.

wametendewa haki kabisa! mwalimu unatakiwa kujipanda muda wote.
pia assesment haifanywi mara moja nafikiri asseser atarudi tena baada ya muda
 
wametendewa haki kabisa! mwalimu unatakiwa kujipanda muda wote.
pia assesment haifanywi mara moja nafikiri asseser atarudi tena baada ya muda
Mkuu tatizo sio kujipanga bali ni unaasesiwa kwa wanafunzi wakati uliingia Mara moja kutambulishwa na mwalimu aliyekuachia kipindi,sasa unaasesiwa kwa kipi ulichokifanya darasani au kuonesha nini mbele ukiacha swala la portfolio ambalo utakuwa umeandaa kila kitu
 
ACHA SIFA NINGEKUWA MIMI NINGEFURAHI YANINI KUJILA PESA ZENYEWE MNAPEWA NUSU NUSU UKOMAE KUFUNDISHA KWANI SIFA UNALIPWA WW UMEASESIWA PIGA MPAKA IJUMAA WIKI SEPA KATAFUTE HELA AJIRA ZA WALIMU ZIKO WAPI
 
Mkuu tatizo sio kujipanga bali ni unaasesiwa kwa wanafunzi wakati uliingia Mara moja kutambulishwa na mwalimu aliyekuachia kipindi,sasa unaasesiwa kwa kipi ulichokifanya darasani au kuonesha nini mbele ukiacha swala la portfolio ambalo utakuwa umeandaa kila kitu

sasa siku ya kuanza kufundisha baada ya kutambulishwa huwa wanafundisha vp?
hapa unafundisha kama kawaida tu haina haja hata kama huwajahi ingia kufundisha, zaidi ujue content na darasa husika
 
nyinyi ndio aina ya walimu tunao dharisha ama nini mana sielewi una lala mika nini harafu hujataja hiko ni chuo gani
 
Back
Top Bottom