Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,615
- 40,162
Askofu wa Jimbo Katoliki la Bukoba Jovitus Mwijage amesema amani haiwezi kuwepo katika nchi mambo yanaendeshwa kwa ujanja ujanja, usiri na uongo.
Askofu Mwijage amesema kiongozi hapaswi kutumia katiba kwa vipengele tu vinavyomlinda yeye huku vingine vikitupwa mbali bali katiba inapaswa kufuatwa kwa matakwa yake yote na hapo ndipo haki itakuwa imetendeka na amani itakuwepo.
Ameyasema hayo leo katika Misa Takatifu ya kuombea Haki na Amani katika nchi ikiwa ni kutimiza takwa la waraka wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) uliotolewa ukiwataka Waamini kufunga na kusali siku ya Tarehe 23 mwezi huu kwa ajili ya kuomba haki na amani katika taifa.
Jimbo Katoliki la Bukoba limeadhimisha siku hiyo leo Agosti 21 kutokana na tarehe 23 Agosti kuwa na tukio la Kijimbo la Sakramenti ya Upadirisho.
Askofu Mwijage amesema kiongozi hapaswi kutumia katiba kwa vipengele tu vinavyomlinda yeye huku vingine vikitupwa mbali bali katiba inapaswa kufuatwa kwa matakwa yake yote na hapo ndipo haki itakuwa imetendeka na amani itakuwepo.
Ameyasema hayo leo katika Misa Takatifu ya kuombea Haki na Amani katika nchi ikiwa ni kutimiza takwa la waraka wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) uliotolewa ukiwataka Waamini kufunga na kusali siku ya Tarehe 23 mwezi huu kwa ajili ya kuomba haki na amani katika taifa.
Jimbo Katoliki la Bukoba limeadhimisha siku hiyo leo Agosti 21 kutokana na tarehe 23 Agosti kuwa na tukio la Kijimbo la Sakramenti ya Upadirisho.