Askofu Mwamasika apinga maandamano ya DOWANS

amka2.gif
na Francis Godwin, Iringa
WAKATI zikiwa zimepita siku mbili tangu Jeshi la Polisi nchini kuzuia maandamano ya wanaharakati wanaopinga hatua ya serikali kutaka kuilipa kampuni ya kufua umeme ya Dowans, Makamu Mwenyekiti wa bodi ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini Makumira, Iringa, Askofu Dk. Peter Mwamasika ameibuka na kupinga maandamano hayo kwani hayana tija kwa taifa.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mahafali ya 14 ya chuo kikuu hicho jana, Dk. Mwamasika alisema kuwa maandamano ni njia ya mwisho hivyo kinachopaswa ni kuhakikisha wanaharakati hao wanakutana katika meza ya mazungumzo na viongozi au hata ikiwezekana kutumia vyombo halali vya maamuzi na si kuitisha maandamano ambayo mwisho husababisha vurugu .
Alisema kuwa matatizo ya taifa hili hayawezi kutatuliwa na vikundi vya watu wachache wanaochochea wananchi ili wafanye maandamano ya kuipinga serikali bali ni muhimu kukaa katika meza moja ili kutoa ushauri kwa viongozi wa serikali.
Hata hivyo aliwataka wanasheria kuhakikisha wanashiriki katika kutoa msaada kwa Watanzania katika kutafuta suluhu ya kweli juu ya malipo hayo.
Alisema suala la serikali kulipa ama kutolipa malipo kwa kampuni hiyo si suala la kuwadanganya Watanzania ili kushiriki katika kufanya maandamano bali ni suala la kisheria ambalo linahitaji zaidi msaada wa wanasheria katika kupinga ama kuridhia malipo hayo. Katika hatua nyingine, Dk. Mwamasika alipongeza hatua ya serikali ya kuanzisha shule za sekondari za kata ambazo zimesaidia katika kufuta ujinga miongoni mwa Watanzania.

Source. Tanzania Daima


Uwa inasemwa usimseme vibaya mpaka mafuta wa bwana,nadhani huyu ni mpaka mafuta wa ibilisi,anatenda kazi ya ibilisi bila kujua au kwa kujua...nani hajui uovu wa viongozi wetu? Tatizo viongozi wengi wa dini si wa waislamu wala wa wakristo wanatumiwa na wahuni wachache kuficha uozo wao....
 
Jamani hii nyongo imetoka wapi yaani ingejua tulivyo na machungu isingesema upuuzi km huu lakini kila kitu kin mwisho.
 
Hivi jamani watanzania wenzangu jaribuni kufunguka akili zenu hivi ni kweli kuwa Richmond peker ndio iliotifikisha hapa kama nchi,jaribuni kujadili kwa kina matatizo yanayotisibu kuliko.kuwa wanafiki kisa ni makundi 2015
 
Kwa kawaida mimi nawaheshimu sana hawa watumishi wa Mungu. Hasa kama ni Maaskofu, na huyu ni Mkuu wa K.K.K.T!!!!!!!!!!!!

Lakini kwa heshima na taadhima, Mheshimiwa Askofu, mahubiri yako yamekosa TIJA. Hujajijulisha kwamba DOWANS ni nini na hujui kwamba inamilikiwa na nani. Hata Rais wetu Jakaya Kikwete amekiri hajui wamiliki wa DOWANS. Wewe nani kakujulisha shareholders wa Dowans?

Wengi wetu tunaamini Dowans na Richmond ni kampuni feki zilizoundwa na mafisadi waliokwapua fedha zetu sisi WaTz. toka BoT (EPA) na kuzitumia kwa madhumuni yao ya kisiasa mwaka wa 2005. Hata Marehemu Daudi Balali alikiri kwamba aliagizwa na Mkuu wake atoe fedha kusaidia uchaguzi. Wakubwa wakazichukua toka EPA. Zilizosalia wakajidai wao ni Wamerikani na kuwapelekea Tanesco mitambo ya umeme wa dharura, wakati huo wakijibandika jina la RICHMOND DEVELOPMENT CORPORATION (P.L.C.).

Kama kawaida katika mashughuli ya haraka haraka ya matumizi ya fedha za wizi, mitambo yao haikukidhi vigezo vilivyotamkwa na Tanesco. Hapo ndipo Bunge letu tukufu lilipoingilia na kugundua, baada ya uchunguzi yakinifu, ulioonyesha uzalendo wa hali ya juu, ufedhuli wa watu tuliodhani ni viongozi wetu ukagundulika. Sasa tumewabatiza ni "MAFISADI"!!!!!!!! Tunakusihi Mheshimiwa Askofu, usali tena na utatambua kuna waumini wako wameku-mislead. Nakuombea Mwenyezi Mungu akusaidie ktk sala hiyo.

Wazalendo jasiri wa Tanzania, ambao wanajali kwa dhati maslahi ya nchi yetu, na watu wanaoona uchungu wa wanyonge wanaotumbukizwa katika lindi la umaskini, unaosababishwa na na hawa wezi wa fedha za umma, wameona njia pekee ni kuhamasisha WaTanzania kuandamana kwa amani na kupinga kwa nguvu zote, malipo kwa hawa wezi na baradhuli. Naamini Dowans hawajajitambulisha kwako. Watakaofaidika na hili tozo la Doawans ni wezi wa mali ya umma.

Hata kama hawa majiizi yatafanikiwa kuwapumbaza Serikali kupinga maandamano ya amani kupinga malipo haya, sisi wanyonge tutaendelea kusali ili hatimae fedha zetu watakazolipwa hatimae zirudishwe kwa kutaifisha mali za hawa baradhuli. Crime does not pay.
 
mwamasika?
Kwanza anakashfa ya ngono.(hata you tube pcha yake ipo)
Ametafuna hela za usharika wa dodoma mjini.
Hospitali ya dcmc anamkono wake pale cjui imekuwaje anajifanya ndo yake.
Kuna mradi wa matofali kawapa wajeruman na ni mradi wa kanisa.
Kiwanda cha maji ya A_sante NAPO???? Mchungaji uyo
 
Go to hell Mwamasika. Twakujua wewe ni nepi ya mafisadi akina Lowassa. Mkipewa vijipesa kidogo vya ufisadi kwenye miradi yenu uchwara mnajiuza kama vyangu. Mkimaliza kutoa matamko haya ya kifala mnakimbilia Monduli kukatiwa pesa ya Kagoda bado mwajiita watu wa Mungu wakati mmejaa roho mtakakitu.
 
mwamasika?
Kwanza anakashfa ya ngono.(hata you tube pcha yake ipo)
Ametafuna hela za usharika wa dodoma mjini.
Hospitali ya dcmc anamkono wake pale cjui imekuwaje anajifanya ndo yake.
Kuna mradi wa matofali kawapa wajeruman na ni mradi wa kanisa.
Kiwanda cha maji ya A_sante NAPO???? Mchungaji uyo

Huyu askofu mstaafu hahusiki na hospitali ya dcmc wala miradi inayoihusu hospitali hiyo ; alikwisha ondolewa kwenye bodi!!
 
Huyu mzee Askofu mstaafu asamehewe kwani hajui alisemalo!!Historia ya maisha yake na utumishi wake hapo dayosisi ya Dodoma ni vielelezo tosha kuwa hajui alisemalo.

itabidi sasa hivi tufanye mgomo wa kwenda kanisani tuone watakula wapi!
 
Huyu askofu nasikia kuwa naye ni UT. Kuna siku alionekana akiendesha gari ya jeshi JWTZ. Huwezi tegemea kupata jipya kutoka kwake, anawatumikia mabwana zake.
 
Huyu askofu mstaafu hahusiki na hospitali ya dcmc wala miradi inayoihusu hospitali hiyo ; alikwisha ondolewa kwenye bodi!!

Mtu akistaafu anakua hana mamlaka ya kiutawala.unajua anakula nini kuhusiana na mkataba aliokula na wazungu kwenye hospital ile? Uwe wise tu usiseme kastaafu.
 
Huyu sio askofu, kwani alishajiuzulu uaskofu akaomba kugombea ubunge kwa tiketi ya ccm mwaka 2010 lakini akashindwa kwenye kura za maoni. Huyu alilivuruga kanisa huko dodoma na alikuwa na mpango wa kutimkia ulaya kwa hiyio naye ni mmoja wa mafisadi
 
huyu askofu anafikiri kwa kutumia sehem gani ya mwili wake? kichwa hakiwezi kufikiria hivi, itakuwa sehem nyigine. eti anapongeza shule za kata... Useless old man.

amka2.gif


na Francis Godwin, Iringa
WAKATI zikiwa zimepita siku mbili tangu Jeshi la Polisi nchini kuzuia maandamano ya wanaharakati wanaopinga hatua ya serikali kutaka kuilipa kampuni ya kufua umeme ya Dowans, Makamu Mwenyekiti wa bodi ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini Makumira, Iringa, Askofu Dk. Peter Mwamasika ameibuka na kupinga maandamano hayo kwani hayana tija kwa taifa.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mahafali ya 14 ya chuo kikuu hicho jana, Dk. Mwamasika alisema kuwa maandamano ni njia ya mwisho hivyo kinachopaswa ni kuhakikisha wanaharakati hao wanakutana katika meza ya mazungumzo na viongozi au hata ikiwezekana kutumia vyombo halali vya maamuzi na si kuitisha maandamano ambayo mwisho husababisha vurugu .
Alisema kuwa matatizo ya taifa hili hayawezi kutatuliwa na vikundi vya watu wachache wanaochochea wananchi ili wafanye maandamano ya kuipinga serikali bali ni muhimu kukaa katika meza moja ili kutoa ushauri kwa viongozi wa serikali.
Hata hivyo aliwataka wanasheria kuhakikisha wanashiriki katika kutoa msaada kwa Watanzania katika kutafuta suluhu ya kweli juu ya malipo hayo.
Alisema suala la serikali kulipa ama kutolipa malipo kwa kampuni hiyo si suala la kuwadanganya Watanzania ili kushiriki katika kufanya maandamano bali ni suala la kisheria ambalo linahitaji zaidi msaada wa wanasheria katika kupinga ama kuridhia malipo hayo. Katika hatua nyingine, Dk. Mwamasika alipongeza hatua ya serikali ya kuanzisha shule za sekondari za kata ambazo zimesaidia katika kufuta ujinga miongoni mwa Watanzania.

Source. Tanzania Daima
 
Askofu ambaye anahubiri neno la Mwenyanzi Mungu na anaona kulipa dowans ni halali basi ujue yeye mwenyewe amejificha kwenye mwamvuli wa dini kuwachuna kondoo za Mungu sadaka yao.

... anayesema hivyo ana sababu zake. Ninahisi ni njia yake ya kutoboa siri ilyo wazi.
 
Back
Top Bottom