only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
na Francis Godwin, Iringa
WAKATI zikiwa zimepita siku mbili tangu Jeshi la Polisi nchini kuzuia maandamano ya wanaharakati wanaopinga hatua ya serikali kutaka kuilipa kampuni ya kufua umeme ya Dowans, Makamu Mwenyekiti wa bodi ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini Makumira, Iringa, Askofu Dk. Peter Mwamasika ameibuka na kupinga maandamano hayo kwani hayana tija kwa taifa.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mahafali ya 14 ya chuo kikuu hicho jana, Dk. Mwamasika alisema kuwa maandamano ni njia ya mwisho hivyo kinachopaswa ni kuhakikisha wanaharakati hao wanakutana katika meza ya mazungumzo na viongozi au hata ikiwezekana kutumia vyombo halali vya maamuzi na si kuitisha maandamano ambayo mwisho husababisha vurugu .
Alisema kuwa matatizo ya taifa hili hayawezi kutatuliwa na vikundi vya watu wachache wanaochochea wananchi ili wafanye maandamano ya kuipinga serikali bali ni muhimu kukaa katika meza moja ili kutoa ushauri kwa viongozi wa serikali.
Hata hivyo aliwataka wanasheria kuhakikisha wanashiriki katika kutoa msaada kwa Watanzania katika kutafuta suluhu ya kweli juu ya malipo hayo.
Alisema suala la serikali kulipa ama kutolipa malipo kwa kampuni hiyo si suala la kuwadanganya Watanzania ili kushiriki katika kufanya maandamano bali ni suala la kisheria ambalo linahitaji zaidi msaada wa wanasheria katika kupinga ama kuridhia malipo hayo. Katika hatua nyingine, Dk. Mwamasika alipongeza hatua ya serikali ya kuanzisha shule za sekondari za kata ambazo zimesaidia katika kufuta ujinga miongoni mwa Watanzania.
Source. Tanzania Daima
Uwa inasemwa usimseme vibaya mpaka mafuta wa bwana,nadhani huyu ni mpaka mafuta wa ibilisi,anatenda kazi ya ibilisi bila kujua au kwa kujua...nani hajui uovu wa viongozi wetu? Tatizo viongozi wengi wa dini si wa waislamu wala wa wakristo wanatumiwa na wahuni wachache kuficha uozo wao....