Askofu Malasusa: Sijalelewa kuwa Kinyume na Serikali, Sijalelewa kutoitii Serikali

malasusa jitu la hovyo kabisa bladidaken
Baadhi ya dondoo kwenye hotuba zake:-

1. Sikulelewa kuipinga serikali.

2. Njooni tusemezane. Tusemezane (dialogue) tukiwa na neno.

3. Kama angetafutwa wa kufaa kuwa Mkuu wa Kanisa basi mimi Malasusa nisingechaguliwa.

4. Rais uchaguzi mdogo 2024 tuufanye ufanikiwe.

5. Amani na mshikamano wa kitaifa.

6. Ninaipenda sana serikali yangu.

7. Rais suala la ndoa za jinsia moja tuachia Kanisa.

8. Amzawadia rais kwa kuhudhuria kwenye ibada iliyomsimika kuwa Mkuu Mpya wa KKKT Tz.

Tathmini.
Hotuba yake imemshushia Askofu Dr. Benson Kalikawe Bagonza wa Dayosisi ya Karagwe kitu kizito utosini.

Aidha, hotuba imempa Bagonza angalizo kutathmini nafasi yake ya criticism kipindi hiki ambacho yeye Malasusa anaenda kuliongoza Kanisa.

Malasusa ni kijana wa mjini Bagonza ni kijana wa shambani, kuvumiliana kunahitajika kwa mustakabali na maslahi mapana ya Kanisa na taifa.

Bagonza alikuwa Askofu Juni 15, 2003. Alikuwa Msemaji Maarufu kwenye Makanisa ya Lutheran Western Illinois kwa miaka 7 alipokuwa akisoma katika chuo cha Wartburg Seminary Dubuque.

2020 aliamua kujiimarishia ulinzi binafsi kufuatia kuhisi hakuwa salama.

Malasusa alikuwa Askofu Aprili 17, 2004 na sasa Mkuu wa Kanisa mara 2. Anajuwa kuchanga karata na kujipatia dume zote. Ni Banker hivyo anajuwa hesabu vizuri.

Asilimia kubwa ya wafuasi wa Kanisa hawakukubaliana na Malasusa kurudi kwenye Ukuu wa Kanisa na ikadhaniwa amefanikiwa kwa mkono wa serikali.

Nijuavyo mimi, Kanisa ni Watchdog wa serikali kama lilivyo mhimili wa Bunge. Kanisa pia limepewa jukumu adhimu na MUNGU la kusahihisha utendaji na mwelekeo wa serikali ili amani idumu kazi ya MUNGU isonge mbele.

Malasusa hakuongelea yafuatayo ambayo Bagonza hasingeyaacha:-

Ugumu wa maisha.
1. Sukari 1kg 5,000/
2. Nyama ya ng'ombe 1kg 12,000/
3. Nyama ya nguruwe 1kg 13,000/
4. Nguruwe na ng'ombe wanachuana mtanange wa bei.
5. Samaki 1kg 10,000/ baada ya Ziwa Victoria na Tanganyika kufungwa.
6. Usalama wa Chakula hususan ugavi na bei kutokuwa himilivu.
7. Pengo kubwa la kipato.
8. Uhaba wa nishati unaohujumu jitihada za wananchi kujikwamua na umaskini.


Maridhiano ya kisiasa.
1. Madai ya Katiba Mpya.
2. Mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi.
3. Misighishano ndani ya vyama iliyosababisha kesi Mahakamani.
4. Changamoto za Siasa za Kanisa (Church Politics).


Nini tathmini yako.
malasusa ni hopeless guy. Eti sikulelewa kutofautiana na serikali, kama serikali haitendi haki? stupid of him!
 
Bagonza kachaguliwa na Papa na Papa ni mkubwa kuliko serikali.
Sasa kila mmoja uangalia yupi boss mkubwa.
Serikali haiwezi mfukuza wala kumzuia Bagonza
 
Askofu Malasusa, Kadinali Mstaafu Polycarp Pengo, Sheikh Alhad Mussa Salum na wengineo wengi; huwa hawafichi mahaba yai kwa chama cha Mapinduzi.

Kwa hiyo hakuna jipya hapo. Kitambo sana anafahamika yeye ni nani linapokuja suala lihusulo ccm na serikali yake.
 
Chadema mmekalia uanaharakati tu kwenye kila jambo.

Fanyeni siasa za kitaalam acheni kutegemea makanisa yawasemee.

Mmepwaya mno.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Chaguo letu walutheri lilikuwa dr.benson bagonza ila wakafanya Yao baada ya kuona TEC wanapeleka moto Sasa dhehebu la pili kwa waumini wengi ilibidi lishikiriwe kwa namna yoyote na mkumbuke Dr.Bagonza na kadinali Rugambwa ni marafiki walioshibana fikiria huo moto
Hawakushibana, washibane nini? Kama ni ukabila mbowe na Askofu Shao kwao kumoja. Bagonza is was a conman, nadhani wana ka agenda ka ushoga kama walivyokumbatiana siku ile madhabahuni na Tundu wakati wa campaign.
 
Back
Top Bottom