Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

mfianchi

Platinum Member
Jul 1, 2009
11,855
8,253
Imebidi nijiulize baada ya kusoma kwenye gazeti kuwa Askofu Malasusa alikuwa msemaji wa familia ya Lowasa kwenye harusi ya binti yake,sijui huu urafiki umeanza baada ya Malasusa kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mashariki pwani,kwa kiongozi wa dini ambaye anaelewa tuhuma za Lowasa kujifanya anamfagilia kwa kumsifia mambo amabyo wala Lowasa hanayo ni unafiki mkubwa si ntashangaa hapo baadaye tukimsikia Askofu Malsusa akisema Lowasa ni chaguo la Mungu,Si elewi uhusiano uliopo kati ya Lowasa na hawa maaskofu wetu kwanza Askofu Laizer wa Arusha naye akajitoma kumpokea Lowasa pale Arusha baada ya kupima hoja za Richmond hata akajiuzulu,kabla hatujakaa sawa mkewe Lowasa akazindua kitabu kama kawaida Maaskofu akiwemo Kardinali Pengo wakajitoma kwenye hiyo hafla jamani maaskofu kama hamjijui Lowasa anawatumia kwa malengo yake na sisi waumini wenu mnatutia kinyaa kwa hizo tabia zenu !!
 
Mkuu kwa kauelewa kangu kadogo Lowasa anasali pale azania front ambapo ndio shughuli nyingi za uongozi wa KKKT tanzania zinafanyikia so i hope wanajuana kabla hata ya Malasusa kuwa askofu... lkn hii ya viongozi wetu wa dini kuwabeba wenye pesa na madaraka na kuwapa sifa zisizohitajika hata pale wanapoonekana kutengwa na jamii kamekuwa sugu. na huwa ndio hapo naona safari ya mbinguni ni ngumu kwa kweli, hatuiigi mfano wa yesu aliye wasema wazi wazi viongozi wa kipindi hicho, any way labda ndio mambo leo ya kwenye dini haya
 
Waswahili walisema "Penye njaa penyeza rupia" hii ndio kazi ya rupia za kifisadi. Wataitumia kujisafisha kwa kila gharama na kwakushibisha kila tumbo lenye njaa na lisiloshiba.
Tusisahau pia Malasusa ni binadamu na ni baba wa familia. Pamoja na kuwajibika kwa kanisa anawajibika kwa familia pia hivyo anajaribu kuwajengea watoto wake mtandao maana si lazima wao wajewaelekee mrengo wake aliopo(Uchungaji/ Uaskofu).Na kanchi haka kamekua ka mtandao kila pahala.Naamini roho yake haitaki ajihusishe na hawa mafisadi lakini mwili wake ni dhaifu. Hii hali ya mwili na roho kutofautiana kimatakwa ilimtokea hata masiha pale alipokua anaelekea kusulubiwa, hivyo huu ni udhaifu wa kawaida kikubwa ni uwezo wa kuushinda ambao Malasusa ameshadhihirisha kushindwa kuuhimili udhaifu huu.

Tutoe wito kwa watanzania wenye imani wawaombee viongozi waregevu hawa
 
Imebidi nijiulize baada ya kusoma kwenye gazeti kuwa Askofu Malasusa alikuwa msemaji wa familia ya Lowasa kwenye harusi ya binti yake,sijui huu urafiki umeanza baada ya Malasusa kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mashariki pwani,kwa kiongozi wa dini ambaye anaelewa tuhuma za Lowasa kujifanya anamfagilia kwa kumsifia mambo amabyo wala Lowasa hanayo ni unafiki mkubwa si ntashangaa hapo baadaye tukimsikia Askofu Malsusa akisema Lowasa ni chaguo la Mungu,Si elewi uhusiano uliopo kati ya Lowasa na hawa maaskofu wetu kwanza Askofu Laizer wa Arusha naye akajitoma kumpokea Lowasa pale Arusha baada ya kupima hoja za Richmond hata akajiuzulu,kabla hatujakaa sawa mkewe Lowasa akazindua kitabu kama kawaida Maaskofu akiwemo Kardinali Pengo wakajitoma kwenye hiyo hafla jamani maaskofu kama hamjijui Lowasa anawatumia kwa malengo yake na sisi waumini wenu mnatutia kinyaa kwa hizo tabia zenu !!


kwel mzee

maaskofu ni wa kuchukuliwa kwa tahadhari kubwa. wengine walisema jk alikuwa chagupo la Mungu. siku hizi makanisa ni mitaji ya kisiasa. si mnamuona makamba, anatumia biblia pale tu anapotafuta jibu la kombora la kisiasa.

huyo malasusa ni mjasiriamali. anataka michango ya kifisadi kujendgea makanisa na chuo kikuu cha mwenge, yuko tayari kumsifia hata rostam muhimu anaangalia upepo wa fedha unakoelekea

marufuku kuchanganya siasa kwenye dini lakini kuchanganya dini kwenye siasa sawa!!!!!!!

tafakari, chukua hatua
 
Askofu Malasusa ni Askofu wa dayosisi ya mashariki na pwani pia ni Askofu mkuu wa Kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania [KKKT].Ushiriki wa Askofu Malasusa na Askofu Thomas Laiser kwenye sherehe za kumwaga mtoto wa E N Lowassa kwa mara nyingine umelizalilisha kanisa na viongozi wake jinsi walivyotayari kuwakumbatia matajiri bila kujali njia walizotumia kuupata utajiri.

Mara kadha kanisa limejikuta linajitia doa kwasababu viongozi wake hawataki kufuata maandiko matakatifu.Sikuwepo kwenye sherehe lakini bila shaka kulikuwepo pombe nyingi zilizowafanya wageni kukaa kwenye sherehe hadi usiku wa manane.Fikiria kanisa la KKKT linavyokemea ulevi [unywaji wa pombe] lakini viongozi wake wa juu yaani maaskofu wawili na akili zao wanashiriki kwenye sherehe kwasababu tu Lowassa ana fedha.

Sipendi viongozi wa kanisa kukubali kutumika na wanasiasa wasiokuwa na maadili kama E N Lowassa.
 
........Ukute Askofu mmojawapo alifungua sherehe...ya pombe nyingi mnoooo....na mwingine kufunga....njia ile ni nyembamba.........
 
Mtandao wa Eddo bado una nguvu sana... Msishangae 2010 WANAMTANDAO WAKAMPENDEKEZA!! kama Bartholomew Diaz aka Vasco aka Mvumbuzi akikaa pembeni.
 
Wajemeni, Maaskofu ni Wachungaji, kazi ya wachungaji ni kuwachunga kondoo wa Bwana wasipotee, Masiya alikuja kwa waliopotea na wale walio elemewa na mizigo ili wapumzishwe.

EL amepotea na ameelemewa na mizigo ya tuhuma, shutuma na kila aina ya bezo, dhihaka, kejeli, matukano, ya kila aina mpaka chuki binafsi mumo humo, kwa watu wa Mungu, huu ndio wakati wa kukaa karibu kabisa na EL na sio kumtenga, bali kumkumbatia mpaka aguswe na roho wa Bwana, atakuja mbele ya kadamnasi ya watu, atatubu, atasamehewa, atatakaswa na atangara kama mbalamwezi tayari kwa 2015!.

Amini nawaambieni, 'jiwe walikolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni'. Kwake Yeye, wa kwanza atakuwa wa mwisho, na wamwisho atakuwa wa kwanza.

Acha Maaskofu watimize mapenzi ya Bwana, ya kuwarudisha kundini kondoo waliopotea.
 
Suprisingly Malasusa kuwa msemaji wa familia. Kwa ufahamu wangu, Malasusa ni mwenyeji wa kusini nyanda za juu, siamini familia ya EL ilikosa ndugu/jamaa kutoka katika huko Ar awe msemaji wa familia. Naona nafasi hiyo alipewa kisiasa zaidi na si kiimani.


Wakati makanisa ya Ulaya na Marekani yameingiliwa na habari za mashoga kutaka kutambuliwa, makanisa ya Tanzania yananunuliwa na mafisadi kutimiza malengo yao.
 
yote yataisha hayo ni kipindi cha mpito,hivi vitabu vya ibada viko so tricky kuna wakati vinakukuza na wakati mwingine vinakumaliza ..kwa sababu content zake zinabadilika kutokana na aina ya wasomaji ambao kwa hakika wanabadilika kila mwaka time will tell.. kama hukulipa gharama zake wewe mwenyewe basi kizazi chako kitaface hiyo,unachofanya ni kukwepa wewe mwenyewe but your generation will have to answer it!! you can't fool all the pple all the time.Tatizo la hizi dini zetu zilishindwa toka siku zinaletwa hivyo utaambiwa mara metaphysics mara philosophy lakini mbona unafiki unaongezeka? mbona wanadamu hawana faida?mbona maisha yanazidi kuwa magumu? majibu ya maswali haya ndo hizo tabia za akina malakasuka wanapigania uhai wao kwanza na wala tusiwaweke mbele sana kwenye mikakati tunayotaka ya kupigana na adha za watawala wetu....
 
Ni kawaida kwa kanisa la Lutherani kuongozwa na viongozi wa siasa. Nafikiri Lowasa ana say sana ndani ya kanisa lile. Ndo maaana askofu Laizer alisafiri toka Arusha hadi Dar. Pia ninakumbuka vizuri namna ambavyo David Msuya alivyowahi kuwa na influence kubwa katika doyosisi mojawapo nchini na kusababisha migogoro mikubwa. I guess kanisa la kilutheri linajipendekeza sana kwa wenye pesa. Lichunge sana maana huyo Malasusa, ningemwalika aje abariki harusi yangu angesema nimwone mchungaji wa usharika wangu. lakini kwakuwa aliyemwomba anazo, mmmh hata kazi ya kuhudumia waumini wengine inasitishwa. Kuna haja ya kanisa hili kujiangalia upya, namna ambavyo linawahudumia waumini wake. Naamin waumini wote masikini kwa matajiri ni sawa.
 
ufisadi hadi makanisani now days........sijui tuwe tunasalia home!!!???
 
Can you imagine askofu wa kikatoliki kuwa msemaji wa fisadi kigogo?Tunaona KKKT mafisadi hupewa status kubwa sana!Nendeni Azania Front muone wenyewe.Malasusa a disgrace!
 
Ishu sio maaskofu tu, mchangia hoja aseme hata Dk Salim, warioba,Mbatia walikuwepo pia lakini tatizo isiwe kuwepo kwa hao prominent figures, je Watanzania tumefikia zama ambazo hatuwezi kuhudhuria shughuli za kijamii za watanzania wenzetu eti kwa kuwa tu tuna tofauti nao kimitazamo? sioni hoja hapo
 
Ishu sio maaskofu tu, mchangia hoja aseme hata Dk Salim, warioba,Mbatia walikuwepo pia lakini tatizo isiwe kuwepo kwa hao prominent figures, je Watanzania tumefikia zama ambazo hatuwezi kuhudhuria shughuli za kijamii za watanzania wenzetu eti kwa kuwa tu tuna tofauti nao kimitazamo? sioni hoja hapo

Sidhani kama Askofu Malasusa angehudhuria kama mwalika tu kungekuwa na hoja ya kujadili, au kama angekuwa anaitwa Askofu Alex Lowasa sina shaka tungekosa hoja ha kujadili lakini kwa nafasi yake kama kiongozi wa juu wa waluteri ni kweli hata mimi msharika wa kawaida pale Azania angekubali kuwa msemaji wa familia yangu? Je si kwamba kanisa linaingia kwenye mgongano kati ya huduma inazotoa kwa waumini wake kutokana na uwezo wa kifedha au nafasi zao katika jamii?
 
Hakuna hoja ya msingi hapa, EL kama fisadi aende jela, Rostam naye alitoa michango KKKT akasemwa sana.

Hawa jamaa ,mafisadi rafiki zetu na ndugu zetu, tunaoishi nao mitaani hatuwezi kuwatenga kwa style hii mnayoitaka.

Core issues hapa ni kuwa hawa jamaa waende jela, tukishindwa hapo tukae kimya, maana hata mke wangu anaweza akawa fisadi.

Hii ni dalili ya kushindwa vita ya ufisadi, .....lets discuss core issue.Malasusa hana na hatakuwa na namna ya kumtenga mtu, EL angekuwa jela angempata wapi?

Another core issues, ni KKKT wangapi waliolalamikia hili swala? je ni RC wangapi wanapiga kelele na kusema no, Pengo hapa usifanye hivi.

OK LET SAY EL KWELI KATHIBITIKA FISADI; Ufisadi umekulia na kuanzia makanisani na misikitini-watoaji wakubwa wa sadaka ni mafisadi!!, umesambaa katika jamii, kuuong'oa inabidi kuanza na watu kama akina Malasusa! Ukiona wafuasi wake WENGI WAKO KIMYA THEN BE SURE KUWA UFISADI TANZANIA NI SEHEMU YA MAISHA YA WATU. La asingekuwa hivyo Malasusa asingesimama kusema.


After all uhusiano wa EL na malasusa haujaanza leo, na kama mtoa maada ungekuwa makini na issue hizi za urafiki ungetoa alert mapema. Wewe mwenywe unaonyesha haujali, unasubiri miti itoe majani ndio tunataka tukate majani.

so wewe mwenyewe unabaki kuwa sample ya watanzania wengi tusiotaka kuzuia haya matatizo, na kuacha hili gonjwa la ufisadi lienee sana
 
Ni kawaida kwa kanisa la Lutherani kuongozwa na viongozi wa siasa. Nafikiri Lowasa ana say sana ndani ya kanisa lile. Ndo maaana askofu Laizer alisafiri toka Arusha hadi Dar. Pia ninakumbuka vizuri namna ambavyo David Msuya alivyowahi kuwa na influence kubwa katika doyosisi mojawapo nchini na kusababisha migogoro mikubwa. I guess kanisa la kilutheri linajipendekeza sana kwa wenye pesa. Lichunge sana maana huyo Malasusa, ningemwalika aje abariki harusi yangu angesema nimwone mchungaji wa usharika wangu. lakini kwakuwa aliyemwomba anazo, mmmh hata kazi ya kuhudumia waumini wengine inasitishwa. Kuna haja ya kanisa hili kujiangalia upya, namna ambavyo linawahudumia waumini wake. Naamin waumini wote masikini kwa matajiri ni sawa.
Sio kanisa, ni Malasusa na Laizer kwa sababu zao binafsi na njaa zao. Wapo viongozi wengi tu wa kanisa wanaokemea ufisadi hata j2 iliyopita kuna mchungaji mmoja aliongelea hii tabia ya viongozi wa kanisa kununuliwa na mafisadi kwa uchungu sana.

Lowasa ni mjanja anawatumia kujiuza kwa waumini na kujifariji kutokana na madongo anayotupiwa.
 
Bado yaonekana tunaogopa kivuli cha EL! Ni kwa nini???

Inawezekana kijamii bado ana nafasi yakutumia kipaji chake kuwaongozaa wananchi kufikia maisha bora!!!

Sina tatizo na EL,bali kero yangu kubwa ni aina ya mfumo wa kiuongozi uliopo unaotokana na KATIBA DHAIFU YA KUWAPENDELEA WATAWALA TUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU....

TUDAI MABADILKO YA KWELI KWA KUANZIA KWENYE KATIBA ILI KULETA DEMOKRASIA YA KWELIIIII.....
 
EL pamoja na pesa nyingi za kifisadi alizo nazo akumbuke vitu 10 hivi hawezi kuvinunua ili kujisafisha!



10. Money can buy a bed, but it cannot buy sleep.
9. Money can buy books, but it cannot by brains.
8. Money can buy food, but not appetite.
7. Money can buy finery, but not beauty.
6. Money can buy a house, but not a home.
5. Money can buy medicine, but not health.
4. Money can buy luxuries, but not culture.
3. Money can buy amusement, but not happiness.
2. Money can buy companions, but not friends.
1. Money can buy flattery, but not respect.




http://www.nomad4ever.com/2007/07/09/10-things-money-cannot-buy/
 
Back
Top Bottom