Askofu Gwajima ajisalimisha kituo cha Polisi

Askofu Gwajima ajisalimisha kituo cha Polisi

Casuist

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2014
Posts
1,189
Reaction score
2,971
Pamoja na leo kipande cha sauti kusambaa kuwa Gwajima angejisalimisha Jumatatu kwa kuwa kwa sasa yupo Arusha na kuwataka waumini wake kufika polisi Jumatatu bila kufanya vurugu.

Kwa sababu ambazo hazijatolewa bado, askofu Gwajima amejisalimisha kituo cha Polisi tayari leo Ijumaa ili kuhojiwa juu ya kutoa lugha chafu dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo.


Audio: Askofu Gwajima awajibu Polisi Kuhusu kuitwa aende kujieleza

Gwajima.jpg



Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, amejisalimisha katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, kwa ajili ya kuhojiwa kutokana na tuhuma za kutoa lugha chafu dhidi ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo.


Akizungumza nje ya kituo hicho kabla ya kuanza kuhojiwa, Gwajima amekaririwa na FikraPevu akisema kwamba alichofanya yeye ni kutumia fursa ya kumuonya kiongozi mwenzake wa kiroho kutokana na kuwageuka wenzake juu ya makubaliano waliyofikia katika tamko lao linalowahamasisha waumini wao kupiga kura ya hapana kwa Katiba Inayopendekezwa.


Gwajima, anasema mbali na hilo la Katiba Inayopendekezwa, tamko husika lililotolewa na Jukwaa la Wakristo Tanzania, lilipinga kutungwa kwa sheria ya Bunge, chini ya uratibu wa Serikali, inayoruhusu kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi.


"Mimi kama kiongozi wa kiroho niliona nimkemee (Kardinali Pengo) kwa sababu mimi ni Askofu wa Kanisa, na yeye pia ni Askofu wa Kanisa. Ilibidi nimkemee kwamba aache kufanya vile alivyofanya, kuwageuka Maaskofu wenzake," amekaririwa Gwajima akisema na kuongeza, "Lakini cha msingi ambacho ndicho cha kuwaza niliyemkemea ni Kardinali Pengo au Polisi?"


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, alimtaka Gwajima kujisalimisha kuhojiwa kufuatia kusambaa mitandaoni sauti na picha za video zinazomuonyesha akimshambulia kwa maneno makali Kardinali Pengo.



Soma zaidi => Gwajima mikononi mwa Kamanda Kova kwa tuhuma za Kumkashifu Kardinali Pengo
 
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo, Josephat Gwajima amejisalimisha kituo cha polisi kati kuhojiwa juu ya kutoa lugha chafu dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Haya mliosema hawezekaniki haogopi polisi ataenda jumatatu kwa wakati wake kama alivyosema kwenye kavideo kake yako wapi?

Chezea Polisi wewe.Kaona wamemzingira kila kona kajua maji marefu jumatatu kaiona iko mbali.Nilishasema kuwa anajitia sijui yuko Arusha,uwongo mtupu kajichimbia tu mahali.Si huyo kaibuka.Chezea dola wewe.
 
Kwani leo Jumatatu ama!! Nimesikiliza clip yake imetoka leo na amesema tukikusanyika Polisi Kati tusifanye vurugu.Katusaliti aise.
 
Jamani ile clip naiskiliza inasema atakwenda Juma tatu

Hana ubavu wa kuwapangia polisi aripoti lini.Walitoa order ajisalimishe mara moja. Jeuri yeyote ya kukataa na kujipangia angekiona cha mtema kuni.Hana ubavu wa kutishia nyau polisi huyo.Polisi wakiamua kula sahani moja na mtu hachomoki.
 
Hana ubavu wa kuwapangia polisi aripoti lini.Walitoa order ajisalimishe mara moja. Jeuri yeyote ya kukataa na kujipangia angekiona cha mtema kuni.Hana ubavu wa kutishia nyau polisi huyo.Polisi wakiamua kula sahani moja na mtu hachomoki.

Duuuuh.......lazima awe mtiifu ni Raia wa nchi hii na si mhaini.
 
Hana ubavu wa kuwapangia polisi aripoti lini.Walitoa order ajisalimishe mara moja. Jeuri yeyote ya kukataa na kujipangia angekiona cha mtema kuni.Hana ubavu wa kutishia nyau polisi huyo.Polisi wakiamua kula sahani moja na mtu hachomoki.
​So Polisi hawajaamua tu kupambana na mafisadi eeeenh?na Polisi hawajaamua kupambana wenyewe kwa wenyewe Kukomesha rushwa?
 
Gwijama ajisalimisha polisi ni baada ya kumtusi kadinali pengo hadharani na kurekodiwa kisha kusambazwa mitandaoni,alipo kupinga tamko la maaskofu tanzania kuwataka waikatae na wapige kura ya hapana
 
Wala hawatampata ng'o! Hayo ni mambo yaliyonenwa madhabahuni! Alafu, inabidi Pengo afungue kesi kwanza! Hii kesi ya sasa kafungua Kova!

Ule uwanja si kanisa ni public open space kama uwanja wa jangwani.Si jengo la kanisa lile.Kamtukana pengo kwenye uwanja wa wazi mbele ya watu wenye dini na wasio na dini kwenye eneo lisilokuwa la kidini la viwanja vya Tanganyika Packers visivyokuwa vya kidini.Pale hakuna madhabahu pana jukwaa mbele ya sheria.Ambapo alitumia hilo jukwaa kumtukana Pengo akijua fika kuwa pengo si muumini wa kanisa lake wala si kiongozi aliye chini yake akaamua kumporomoshea matusi ya nguoni wakati akjijua pengo hakuwemo humo kanisani kujitetea dhidi ya matusi aliyomporomoshea.

Si kesi zote za jinai lazima mtu aliyekashifiwa akashtaki.Mfano wewe ni askofu ukatukana waislamu hadharani kuwa mohamed alikuwa anakula nguruwe Waislamu wakaja juu.Polisi wanaweza kukufungulia mashtaka ya kutoa matamshi yanayoletelea uvunjifu wa amani bila mwislamu yeyote kupeleka mashtaka.

Kutukana pengo ni kuletelea uvunjifu wa amani kwa waumini wanaomheshimu Pengo.Hivyo Polisi kumfungulia mashtaka Gwajima ni sahihi.Pengo wala hahitaji kwenda polisi.

Gwajima ashikiliwe hadi jumatatu ili asizidi kuzua na kuporomosha matusi na tuhuma zitto.Ikumbukwe kuwa pamoja na kutafutwa ameendelea kutoa Audio za matusi kwa viopngozi ikiwemo aliyoweka leo.Kwa hiyo ili asiendelee na hayo ashilkiliwe hadi jumatatu
 
Back
Top Bottom