GE2025 Askofu Bagonza: Uchaguzi umekwisha, tuonane mezani

GE2025 Askofu Bagonza: Uchaguzi umekwisha, tuonane mezani

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe, Dkt. Benson Bagonza, amesema hali ya sasa ya kisiasa nchini, baada ya kuenguliwa kwa Mgombea Urais wa ACT Wazalendo Luhaga Mpina, inathibitisha hitaji kubwa la wadau wa siasa kurudi mezani kujadiliana.

1756367637833.png
Akizungumza na SAUT DIGITAL, saa chache baada ya Mpina kuzuiwa kuingia katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kurejesha fomu Agosti 27, 2025, Bagonza amesema mfumo wa sasa unaonesha dalili za kuvuruga misingi ya demokrasia na uhuru wa vyombo vya uchaguzi.

“Mambo yote ni magumu sana haya, yanasisitiza kitu kimoja tu ambacho nimekuwa nikikisema- tunahitaji kurudi mezani. Kwa mfano hili la kuengua mgombea, mimi nilitegemea anakwenda kurejesha fomu halafu kama kuna sababu basi Msajili aweke pingamizi huko, siyo Msajili amuengue mgombea. Kazi ya kuengua mgombea siyo ya Msajili ni ya Tume, lakini cha ajabu zaidi pia nikaona Tume ikatoa barua ya kumzuia kabla hata hajaenda, kana kwamba kulikuwa na mawasiliano kati ya Tume na Msajili,” amesema Askofu Bagonza.

Askofu huyo ameongeza kuwa kitendo cha vyombo vinavyotakiwa kuwa huru na vinavyojitegemea kuonekana kushirikiana katika kumzuia mgombea ni ishara ya hatari kwa mustakabali wa uchaguzi.

“Hatutakuwa na uchaguzi ila tutakuwa na siku ya uchaguzi, kwahiyo uchaguzi ni kama umekwisha, tunawashukuru sana WanaCCM wameteua wamemaliza, tusonge mbele lakini uchaguzi ni kama umekwisha. Matokea yake hapo baadaye ni kwamba hakuna mzigo mimi ninaoufahamu hapa duniani kwa kiongozi kama kuongoza watu ambao una mashaka kama walikuchagua, ni mzigo sana”, amesisitiza.

Bagonza amehimiza kuwepo kwa chombo cha maelewano kitakachokutanisha vyama vyote na wadau wa siasa kujadili namna ya kusonga mbele, akibainisha kuwa kutumia nguvu kufanikisha maendeleo badala ya ushawishi ni mzigo mkubwa kwa serikali yoyote.

“Sasa Bunge lilikwishavunjwa kwahiyo hatuna wabunge, lakini bado tuna Mawaziri na hili ni jambo jema kwasababu huwezi kuiacha serikali hewani. Kwahiyo hata sasa tuna wagombea Urais lakini bado tunaye Rais, huwezi kuiacha nchi bila Rais, ni Rais na wakati huohuo ni wagombea, ninadhani ipo haja ya kuitana mezani na kutengeneza mazungumzo
 
Mtu muongea sana baadaye unadharaulika

Papa wa Katoliki huheshimiwa sana sababu kuongea kwake nadra .Na akitoka kuongea dunia yote hutega masikio

Hawa akina Bagonza ashakuwa wa kupuuzwa

Anaongea utafikiri kameza CD ya kwaya
 
Mtu muongea sana baadaye unadharaulika

Papa wa Katoliki huheshimiwa sana sababu kuongea kwake nadra .Na akitoka kuongea dunia yote hutega masikio

Hawa akina Bagonza ashakuwa wa kupuuzwa

Anaongea utafikiri kameza CD ya kwaya
angekuwa anaipigia debe CCM ungesema hayo?
OGOPA sana mtu anayependa kusifiwa tu na hapendi KUKOSOLEWA!
 
angekuwa anaipigia debe CCM ungesema hayo?
OGOPA sana mtu anayependa kusifiwa tu na hapendi KUKOSOLEWA!
Ndio ningesema
Ndio maana hata Raisi huwa haongei sana kama Bagonza

Akiongea nchi yote hutega sikio
 
Mtu muongea sana baadaye unadharaulika

Papa wa Katoliki huheshimiwa sana sababu kuongea kwake nadra .Na akitoka kuongea dunia yote hutega masikio

Hawa akina Bagonza ashakuwa wa kupuuzwa

Anaongea utafikiri kameza CD ya kwaya
Huwezi kukaa kimya mambo yanakwenda hovyo huo ni udhaifu na woga mkubwa sana.
 
Mtu muongea sana baadaye unadharaulika

Papa wa Katoliki huheshimiwa sana sababu kuongea kwake nadra .Na akitoka kuongea dunia yote hutega masikio

Hawa akina Bagonza ashakuwa wa kupuuzwa

Anaongea utafikiri kameza CD ya kwaya
Tunaanza kukupuuza wewe kwanza.
 
Mtu muongea sana baadaye unadharaulika

Papa wa Katoliki huheshimiwa sana sababu kuongea kwake nadra .Na akitoka kuongea dunia yote hutega masikio

Hawa akina Bagonza ashakuwa wa kupuuzwa

Anaongea utafikiri kameza CD ya kwaya
Screenshot_20250729-090555~2.png
 
Mtu muongea sana baadaye unadharaulika

Papa wa Katoliki huheshimiwa sana sababu kuongea kwake nadra .Na akitoka kuongea dunia yote hutega masikio

Hawa akina Bagonza ashakuwa wa kupuuzwa

Anaongea utafikiri kameza CD ya kwaya
Papa ni raia wa Vatican, rais au mkuu wa Vatican ni nani na anapatikana kwa namna gani halikadhalika siasa za Vatican zina athari kiasi gani kwa Papana jamii yake?

Bagonza ni raia wa Tanzania anayo haki ya kuongelea siasa na uongozi wa nchi yake kama mwananchi ambe siasa za Tanzania zinamuhusu yeye na jamii yake. Zikiwa siasa nzuri na maendeleo Bagonza, hivyo Bagonza kuongelea siasa za nchi yake sioni kama.kuna tatizo.
 
Mtu muongea sana baadaye unadharaulika

Papa wa Katoliki huheshimiwa sana sababu kuongea kwake nadra .Na akitoka kuongea dunia yote hutega masikio

Hawa akina Bagonza ashakuwa wa kupuuzwa

Anaongea utafikiri kameza CD ya kwaya
Kwani ameongea ukweli au sio kweli??
 
Siku Bagonza akirudi kwao Burundi, wana Karagwe watalia sana
 
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe, Dkt. Benson Bagonza, amesema hali ya sasa ya kisiasa nchini, baada ya kuenguliwa kwa Mgombea Urais wa ACT Wazalendo Luhaga Mpina, inathibitisha hitaji kubwa la wadau wa siasa kurudi mezani kujadiliana.

Akizungumza na SAUT DIGITAL, saa chache baada ya Mpina kuzuiwa kuingia katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kurejesha fomu Agosti 27, 2025, Bagonza amesema mfumo wa sasa unaonesha dalili za kuvuruga misingi ya demokrasia na uhuru wa vyombo vya uchaguzi.

“Mambo yote ni magumu sana haya, yanasisitiza kitu kimoja tu ambacho nimekuwa nikikisema- tunahitaji kurudi mezani. Kwa mfano hili la kuengua mgombea, mimi nilitegemea anakwenda kurejesha fomu halafu kama kuna sababu basi Msajili aweke pingamizi huko, siyo Msajili amuengue mgombea. Kazi ya kuengua mgombea siyo ya Msajili ni ya Tume, lakini cha ajabu zaidi pia nikaona Tume ikatoa barua ya kumzuia kabla hata hajaenda, kana kwamba kulikuwa na mawasiliano kati ya Tume na Msajili,” amesema Askofu Bagonza.

Askofu huyo ameongeza kuwa kitendo cha vyombo vinavyotakiwa kuwa huru na vinavyojitegemea kuonekana kushirikiana katika kumzuia mgombea ni ishara ya hatari kwa mustakabali wa uchaguzi.

“Hatutakuwa na uchaguzi ila tutakuwa na siku ya uchaguzi, kwahiyo uchaguzi ni kama umekwisha, tunawashukuru sana WanaCCM wameteua wamemaliza, tusonge mbele lakini uchaguzi ni kama umekwisha. Matokea yake hapo baadaye ni kwamba hakuna mzigo mimi ninaoufahamu hapa duniani kwa kiongozi kama kuongoza watu ambao una mashaka kama walikuchagua, ni mzigo sana”, amesisitiza.

Bagonza amehimiza kuwepo kwa chombo cha maelewano kitakachokutanisha vyama vyote na wadau wa siasa kujadili namna ya kusonga mbele, akibainisha kuwa kutumia nguvu kufanikisha maendeleo badala ya ushawishi ni mzigo mkubwa kwa serikali yoyote.

“Sasa Bunge lilikwishavunjwa kwahiyo hatuna wabunge, lakini bado tuna Mawaziri na hili ni jambo jema kwasababu huwezi kuiacha serikali hewani. Kwahiyo hata sasa tuna wagombea Urais lakini bado tunaye Rais, huwezi kuiacha nchi bila Rais, ni Rais na wakati huohuo ni wagombea, ninadhani ipo haja ya kuitana mezani na kutengeneza mazungumzo

"Njia pekee ambayo Wananchi wataitumia katika kuzungumza au kujadiliana na Watawala wao ambao ni Madikteta ili kufikia muafaka wenye maslahi kwa pande zote mbili ni kwa kuipitia mtutu wa bunduki."
Jeffs O'Brien
 
Ndio ningesema
Ndio maana hata Raisi huwa haongei sana kama Bagonza

Akiongea nchi yote hutega sikio
Mama akiongea sana huwa anaishia kutoa mashudu, usimlinganishe na wenye akili kama bagonza!
 
Back
Top Bottom