Askofu Bagonza: Kuzuia Taharuki Kunaleta Taharuki

Torch

JF-Expert Member
Aug 11, 2013
1,200
1,116
KUZUIA TAHARUKI KUNALETA TAHARUKI

Kuwazuia watu kutoogopa kitu kinachoogopesha ni kuwakosea haki watu hao. Binadamu kamili huogopa. Kutoogopa kinachoogopesha ni kasoro ya kimaumbile hata kama si dhambi.

Hatari huogopesha. Hatari isiyoogopesha si hatari tena. Hatari inayoogopesha imekamilika, siyo feki.

Mwenyezi Mungu anapoagiza TUSIOGOPE haina maana kuwa hakuna hatari. Anasema MSIOGOPE kwa sababu anajua iko hatari.

Kuzuia watu wasiwe na taharuki kwa jambo lenye taharuki ni kusababisha taharuki. Kwa mfano:

1. Kutovaa barakoa katikati ya waliovaa barakoa ni kuzua taharuki.

2. Kutovaa barakoa katika mazishi ya mtu aliyekufa kwa Corona ni kuleta taharuki zaidi.

3. Kuwakejeli wanaotahadharisha juu ya uwepo wa Corona ni kustawisha taharuki.

4. Kuzuia matangazo ya taarifa za Corona au kumilikisha taarifa hizo ni kustawisha taharuki.

5. Kusema hakuna taharuki ni kuchochea taharuki.

6. Kukemea matamko, mahubiri na nyaraka za kuelimisha kuhusu Corona ni kuchochea taharuki.

7. Kuona majeneza mengi airport, misururu ya Coaster na ibada za mazishi kunazua taharuki hata pasipo kutangaza chanzo cha kifo.

8. Kuona hospitali zinatangaza nafasi za kazi za watunza Mortuary kunaleta taharuki.

9. Kuona mafundi majeneza wakitafuta mbao kwa wingi kunaongeza taharuki.

10. Ongezeko la bei ya malimao, tangawizi, vitunguu na asali kunaongeza taharuki.

KWA hiyo taharuki ni sehemu muhimu ya ugonjwa wa Corona. Bila taharuki, Corona haiwi Corona na Elimu haitolewi kikamilifu. Corona bila taharuki haiwezekani. Jitihada za kuondoa taharuki, zinaongeza taharuki. Wanaoshtakiwa kwa kusababisha taharuki ni mashujaa wa vita hii, watastahili nishani ushindi ukipatikana. Zingatia, chukua hatua.
 
Dunia imeelemewa na mzigo mzito wa dhambi.
Watu wanaogopa kifo kuliko dhambi..
Nashangaa sana Maaskofu, wachungaji na waongozaji wengi wa kiroho ndio wamekuwa wapotoshaji zaidi juu ya maisha ya watu.

Rais wetu, nadhani wengi wa wapinzani bado hawajaelewa dhamira yake kuu kwa hawa wanyonge watanzania.
Wengi wanapinga jambo wasilolifaham, Ukweli utajulikana tu.
Na naamini pia Mungu yu pamoja nasi watanzania.
 
Tumeumbwa hivo laZima tutofautiane mawazo yetu kukosoa mawazo yamtu bila kutoa mubadala tunakuita mchonganishi huyo askofu nikiongozi wakiroho yy atusaidie kutupa elimu yakujikinga na maradhi yote yanayotusumbua
 
Dunia imeelemewa na mzigo mzito wa dhambi.
Watu wanaogopa kifo kuliko dhambi..
Nashangaa sana Maaskofu, wachungaji na waongozaji wengi wa kiroho ndio wamekuwa wapotoshaji zaidi juu ya maisha ya watu.

Rais wetu, nadhani wengi wa wapinzani bado hawajaelewa dhamira yake kuu kwa hawa wanyonge watanzania.
Wengi wanapinga jambo wasilolifaham, Ukweli utajulikana tu.
Na naamini pia Mungu yu pamoja nasi watanzania.
Kweli mkuu
 
Ana maana Jiwe anazua taaluki mpaka makanisani,eti leo ameenda kuwakagua masista kama hawavai barakoa

Ila jiwe alitakiwa awe Mirembe sio kwa ukiazi huu,halafu kinachoshangaza zaidi ana PhD tena ya maganda ya koroshow
 
Una kichwa kizito sana kama hujui namna ya kujikinga na haya maradhi


Tumeumbwa hivo laZima tutofautiane mawazo yetu kukosoa mawazo yamtu bila kutoa mubadala tunakuita mchonganishi huyo askofu nikiongozi wakiroho yy atusaidie kutupa elimu yakujikinga na maradhi yote yanayotusumbua
 
Dunia imeelemewa na mzigo mzito wa dhambi.
Watu wanaogopa kifo kuliko dhambi..
Nashangaa sana Maaskofu, wachungaji na waongozaji wengi wa kiroho ndio wamekuwa wapotoshaji zaidi juu ya maisha ya watu.

Rais wetu, nadhani wengi wa wapinzani bado hawajaelewa dhamira yake kuu kwa hawa wanyonge watanzania.
Wengi wanapinga jambo wasilolifaham, Ukweli utajulikana tu.
Na naamini pia Mungu yu pamoja nasi watanzania.
Wapo pamoja kwa lipi ulilomridhisha mungu wako
 
Back
Top Bottom