Sanyambila
JF-Expert Member
- Jan 24, 2018
- 339
- 457
Ujumbe kutoka kwa Baba Askofu Dr Benson Bagonza PhD..
HONGERA CHADEMA, lakini...
Nawapongeza wana Chadema kwa kumaliza uchaguzi. Nawapongeza viongozi wote walioshiriki, wakashindwa na kushinda. Mlichokozwa, hamkuchokozeka. Waleteeni watanzania fikra mpya, hoja mpya na siyo Tanzania mpya.
Tanzania ni moja isiyo na mipaka mipya na kwa hiyo Tanzania siyo mpya.
Mnapoanza awamu mpya zingatieni haya:
1. Taifa imara linahitaji Chama tawala imara.
2. Chama tawala imara kinahitaji chama mbadala/Pinzani imara.
3. Serikali imara inahitaji chama tawala na chama pinzani imara.
4. Bunge imara linahitaji chama tawala imara, serikali imara na kambi ya upinzani imara. Nje ya haya, hakuna spika imara.
5. LAKINI, uimara wa chama cha upinzani hautokani na uimara wa chama tawala. Msibweteke.
6. Mkutano wenu umeonyesha haya:
- Chadema ina mashabiki wengi kuliko wanachama. CCM ina wanachama wengi kuliko mashabiki.
- Kazi ya Chadema ni kubadili mashabiki kuwa wanachama, na ya CCM ni ya kuongeza mashabiki bila kupoteza wanachama. Msichukiane, msipendane, msimalizane bali mjifunze kuishi na hali msiyoweza kuibadilisha.
- Wanachama wanapenda kuchagua viongozi wao. Hujuma kutoka wapinzani wenu zina nguvu sawa hujuma za kutengeneza wenyewe. Jilindeni na chachu ya ubaguzi, ukanda, U-wenyewe na ubabe. Haya ni mabaya kwa watani wenu, hayawezi kuwa mazuri ndani yenu.
7. Kubalini bila uchungu kuwa, hakuna chama cha siasa Tanzania chenye uwezo wa kushinda uchaguzi kwa kutegemea kura za wanachama wake tu. Kazi ya kushawishi haiepukiki. Kulazimishana ni kubaka demokrasia. Hakuna anayezaliwa akiwa mzalendo au msaliti. Kuna wakati Yuda anahitajika ili kuujua uimara wako. Bila ushirikiano, kuna chama pinzani cha milele na chama tawala cha milele.
8. Haja ya kuwa na taasisi imara kuliko kuwa na viongozi/watawala imara ni kubwa sasa kuliko huko nyuma. Hakuna taasisi imara nje ya KATIBA MPYA inayolipatia taifa tume huru ya uchaguzi, bunge huru, mahakama huru, asasi huru za kiraia, media huru na wananchi walio huru. Hofu ni adui wa maendeleo.
Amani endelevu imo ndani ya tumbo la katiba mpya.
Tanzania yenye amani ni tunda la mshikamano wenye haki ndani yake. Msichoke kutafuta maridhiano ndani na nje yenu.
Mungu ibariki Tanzania.
HONGERA CHADEMA, lakini...
Nawapongeza wana Chadema kwa kumaliza uchaguzi. Nawapongeza viongozi wote walioshiriki, wakashindwa na kushinda. Mlichokozwa, hamkuchokozeka. Waleteeni watanzania fikra mpya, hoja mpya na siyo Tanzania mpya.
Tanzania ni moja isiyo na mipaka mipya na kwa hiyo Tanzania siyo mpya.
Mnapoanza awamu mpya zingatieni haya:
1. Taifa imara linahitaji Chama tawala imara.
2. Chama tawala imara kinahitaji chama mbadala/Pinzani imara.
3. Serikali imara inahitaji chama tawala na chama pinzani imara.
4. Bunge imara linahitaji chama tawala imara, serikali imara na kambi ya upinzani imara. Nje ya haya, hakuna spika imara.
5. LAKINI, uimara wa chama cha upinzani hautokani na uimara wa chama tawala. Msibweteke.
6. Mkutano wenu umeonyesha haya:
- Chadema ina mashabiki wengi kuliko wanachama. CCM ina wanachama wengi kuliko mashabiki.
- Kazi ya Chadema ni kubadili mashabiki kuwa wanachama, na ya CCM ni ya kuongeza mashabiki bila kupoteza wanachama. Msichukiane, msipendane, msimalizane bali mjifunze kuishi na hali msiyoweza kuibadilisha.
- Wanachama wanapenda kuchagua viongozi wao. Hujuma kutoka wapinzani wenu zina nguvu sawa hujuma za kutengeneza wenyewe. Jilindeni na chachu ya ubaguzi, ukanda, U-wenyewe na ubabe. Haya ni mabaya kwa watani wenu, hayawezi kuwa mazuri ndani yenu.
7. Kubalini bila uchungu kuwa, hakuna chama cha siasa Tanzania chenye uwezo wa kushinda uchaguzi kwa kutegemea kura za wanachama wake tu. Kazi ya kushawishi haiepukiki. Kulazimishana ni kubaka demokrasia. Hakuna anayezaliwa akiwa mzalendo au msaliti. Kuna wakati Yuda anahitajika ili kuujua uimara wako. Bila ushirikiano, kuna chama pinzani cha milele na chama tawala cha milele.
8. Haja ya kuwa na taasisi imara kuliko kuwa na viongozi/watawala imara ni kubwa sasa kuliko huko nyuma. Hakuna taasisi imara nje ya KATIBA MPYA inayolipatia taifa tume huru ya uchaguzi, bunge huru, mahakama huru, asasi huru za kiraia, media huru na wananchi walio huru. Hofu ni adui wa maendeleo.
Amani endelevu imo ndani ya tumbo la katiba mpya.
Tanzania yenye amani ni tunda la mshikamano wenye haki ndani yake. Msichoke kutafuta maridhiano ndani na nje yenu.
Mungu ibariki Tanzania.