tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 27,195
- 27,810
Askari 12 wanaodhaniwa kuwa kikosi kinachopambana na vitendo vya ujangili katika hifadhi ya taifa ya Tarangire Wilayani Babati mkoani Manyara wanadaiwa kufanya mauaji ya kutisha baada ya kumteka nyara mkulima mmoja mkazi wa mji mdogo wa Galapo ambaye hajulikani alipo na kisha kumtesa na kumshambulia kwa kipigo mke wa mkulima huyo na kusababisha kifo chake kutokana na kile kinachodaiwa kuhusika katika vitendo vya ujangili.
Akizungumza na mamia ya wananchi waliokuwa na hasira huku baadhi yao wakiwa wamepoteza fahamu kwenye nyumba ya msiba katika Kitongoji cha Olongadida mwenyekiti wa kitongoji hicho Bw Rashidi Kajogoo amesema anashangazwa na askari wa hifadhi hiyo kumteka Nyara Bw Eliasi Kibuga Oktoba 14 kinyemela bila ya uongozi kufahamu aidha baada ya mke wake Bi Evaline Gaspa kufuatilia nae Alikamatwa na kisha kufa katikamzingira ya kutatanisha na mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya mrara mjini babati.
Wakati jitihada za kumtafuta mkuu wa hifadhi hiyo bw stephen qoolzikiendelea kufanyika ili kuzungumzia tukio hilo,nae kamanda wa Polisi mkoani hapa afande Akili Mpwapwa akizungumza kwa njia ya simu amekiri kukamatwa kwa mwanamke huyo ambaye amedai baada ya upekuzi alikutwa na mkia wa twiga lakini kifo chake akidai kimetokana na mshtuko wa mahojiano na kufariki na timu ya polisi Imefuatilia kubaini mume wa marehemu mahali alipo,kauli ambayo imepingwa na watoto wa familia hiyo walioshuhudia kipigo cha mama yao huku baba yao akiwa hajulikani alipo.
Hata hivyo kufuatia kuwepo kwa tukio hilo la mauaji liliamsha hasiramamia ya wanawake kupinga mauaji hayo dhidi ya mwanamke mwenzao Bi. Evaline Gaspa huku wakidai kifo chake kimetokana na unyanyasaji ambao haukushirikisha askari wa kike na kutishia kumfungulia mashtaka mkuu wa hifadhi hiyo.
SOURCE: ITV
Akizungumza na mamia ya wananchi waliokuwa na hasira huku baadhi yao wakiwa wamepoteza fahamu kwenye nyumba ya msiba katika Kitongoji cha Olongadida mwenyekiti wa kitongoji hicho Bw Rashidi Kajogoo amesema anashangazwa na askari wa hifadhi hiyo kumteka Nyara Bw Eliasi Kibuga Oktoba 14 kinyemela bila ya uongozi kufahamu aidha baada ya mke wake Bi Evaline Gaspa kufuatilia nae Alikamatwa na kisha kufa katikamzingira ya kutatanisha na mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya mrara mjini babati.
Wakati jitihada za kumtafuta mkuu wa hifadhi hiyo bw stephen qoolzikiendelea kufanyika ili kuzungumzia tukio hilo,nae kamanda wa Polisi mkoani hapa afande Akili Mpwapwa akizungumza kwa njia ya simu amekiri kukamatwa kwa mwanamke huyo ambaye amedai baada ya upekuzi alikutwa na mkia wa twiga lakini kifo chake akidai kimetokana na mshtuko wa mahojiano na kufariki na timu ya polisi Imefuatilia kubaini mume wa marehemu mahali alipo,kauli ambayo imepingwa na watoto wa familia hiyo walioshuhudia kipigo cha mama yao huku baba yao akiwa hajulikani alipo.
Hata hivyo kufuatia kuwepo kwa tukio hilo la mauaji liliamsha hasiramamia ya wanawake kupinga mauaji hayo dhidi ya mwanamke mwenzao Bi. Evaline Gaspa huku wakidai kifo chake kimetokana na unyanyasaji ambao haukushirikisha askari wa kike na kutishia kumfungulia mashtaka mkuu wa hifadhi hiyo.
SOURCE: ITV