Askari wa usalama barabarani wakimpiga raia

Askari wa usalama barabarani wakimpiga raia

Mbona hiyo video kwangu inaonyesha huyo mkamatwaji alikuwa tayari kashakubari kukamatwa na ndio maana hata mikono yake kwapamoja alikuwa kaiweka kwenye kibamia chake hapo haikupaswa kabisa traffic kuanza kumrushia makonde mtu ambae tayari ni mateka na inavyoonyesha yote aliyokuwa anayafanya traffic alijua nikinyume kabisa na ndio maana wakati anafanya kitendo kile alikuwa anapapasa macho yake kila mahari ili kuona ka kunawatu wanamtazama na baada ya kugundua kunawatu wanamtazama akapunguza speed ya kutwanga makonde na kusingelikuwa na watu wanaomtazama jamaa angeenda kusimulia ahhhhhh
 
Askari wapo sawa, kisheria hiyo inaitwa "reasonable force" na imeruhusiwa.
 
Tueleze kwanza jamaa kafanyeje ndo uulize sheria zinasemaje. Traffic nao ni law enforcers endapo mkosaji alifanya au kuwafanyia kitu ambacho ni ukiukwaji Wa sheria na ni jeuri, lazima nguvu itumike.
Hakuna mtu anayeruhusiwa kumpiga mwenzake hata awe askari, nguvu haitumiki kupiga
 
Tii Sheria Bila Shuruti maana Tii "heshimu".Sheria" mwongozo".Bila shuruti"Adhabu kukamatwa Pole au kwakutumia nguvu na makofi juu
 
Embu nipe hiyo Sheria inayoruhusu polisi kupiga raia kaka, hayo ni mazoea ya kikoloni ambayo hata huko kwao hayapo
Tafuta criminal procedure act, kipengele cha ground of arrest hapo wameainisha askari kutumia reasonable force.
 
top down effect,aliye juu mwenyewe hajali hakia za raia, ni ubabe na roho mbaya,basi inaigwa hadi chini huko
 
Hivi unajua mtu anayepigwa anapigwaje???

Umeshawahi kuona mtu anatandikwa wewe???

Huyo mtu amepigwa,au anavutwa vutwa shati??

Huyu hajapigwa labda hujui mtu anapigwaje???
Mkorintho wewe ni askari?
Samahani nataka tu kufahamu.
 
naona wengi wenu hamjaona vizuri kabla kidogo traffic hajavua koti kamtia kibao baada ya kibao akavua koti
 
Tafuta criminal procedure act, kipengele cha ground of arrest hapo wameainisha askari kutumia reasonable force.
Mkuu Polo, Acha kujiamini kwa kitu usichokijua. Labda nikuwekee kifungu ili uache ligi.
SURA YA 20 . SHERIA YA MWENENDO WA MAKOSA YA JINAI YA NOV 1. 1985 AMBAYO ILIFANYIWA MAREKEBISHO 2002.

SEHEMU YA PILI
KUHUSU UTARATIBU UNAOHUSIANA NA UPELELEZI WA MAKOSA YA JINAI.

UTUMIAJI WA NGUVU KATIKA UKAMATAJI

21. -(1) Afisa wa polisi au mtu mengine hatatakiwa, wakati wa kumkamata mtu, kutumia nguvu zaidi au kuvunja utu wa mtu huyo zaidi ya ilivyolazima kufanikisha ukamataji au kuzuia utorokaji wa mtu baada kukamatwa.

(2) Bila nkipunguza matumaini ya kifungu kidogo (1). Afisa polisi hatatakiwa wakati wa kukamata mtu kitendo kinachoweza kusababisha kifo kwa mtu huyo, usiponipa kama afisa polisi anaamini kwa sababu za msingi kwamba kufanya kitendo hicho ni muhimu katika kulinda maisha au kuzuia madhara makubwa kwa mtu mwingine.
 
Back
Top Bottom