Askari wa uhamiaji wasio waadilifu waonywa

Rashda Zunde

Senior Member
May 28, 2022
199
231
Rais Samia amewaonya askari wa uhamiaji wasio waaadilifu, wanaohujumu fedha za vibali vya makazi na viza na kutaka hatua zichukuliwe kwa wote wanaofanya uhujumu huo.

Rais Samia amesema kupitia utafiti mdogo uliofanyika kwenye mkoa wa Dar es Salaam na Zanzibar wamebaini upotevu mkubwa wa fedha unaofanywa na maafisa uhamiaji na kutaka vitendo hivyo vikomeshwe.

“Wale wote waliohusika na mambo yale washughulikiwe,” ameongeza Rais.

Ili kukomesha vitendo vya vya rushwa na unyanyasaji wa raia wa kigeni unaofanywa kwa maafisa wahamiaji, Rais Samia amesema kuwa kuna haja maafisa hao wanaofanya vitendo hivyo kurudi tena kwenye mafunzo ili wakumbushwe wajibu wao.

Aidha Rais Samia amesema Serikali imetoa fedha ili maafisa wa vikosi vyote vya Tanzania wapate mafunzo yatakayo wawezesha kuongeza ufanisi kwenye vituo vyao vya kazi.
 
CAG ameonesha hao Askari ni weziiiiiiiiii Sasa analalamika nini,yeye ilitakiwa aseme ikifika jumanne wawe mahakamani
 
Yaani maafisa wanaofanya vitendo hivyo vya rushwa, unyanyasaji n.k warudi tena kambini wakajifunze upya ingali kuna vijana wako mtaani miaka kadhaa na vyeti vyao hawana kazi!?

Hakuna cha msalia mtume, inatakiwa vibarua viote mbawa akili ziwakae vizuri.

Punda afe mzigo wa bwana ufike.
 
Rais Samia amewaonya askari wa uhamiaji wasio waaadilifu, wanaohujumu fedha za vibali vya makazi na viza na kutaka hatua zichukuliwe kwa wote wanaofanya uhujumu huo.

Rais Samia amesema kupitia utafiti mdogo uliofanyika kwenye mkoa wa Dar es Salaam na Zanzibar wamebaini upotevu mkubwa wa fedha unaofanywa na maafisa uhamiaji na kutaka vitendo hivyo vikomeshwe.

“Wale wote waliohusika na mambo yale washughulikiwe,” ameongeza Rais.

Ili kukomesha vitendo vya vya rushwa na unyanyasaji wa raia wa kigeni unaofanywa kwa maafisa wahamiaji, Rais Samia amesema kuwa kuna haja maafisa hao wanaofanya vitendo hivyo kurudi tena kwenye mafunzo ili wakumbushwe wajibu wao.

Aidha Rais Samia amesema Serikali imetoa fedha ili maafisa wa vikosi vyote vya Tanzania wapate mafunzo yatakayo wawezesha kuongeza ufanisi kwenye vituo vyao vya kazi.
Arusha kuna kiwanda cha A-Z wahindi wasio na vibali vya makazi au kufanya kazi Tanzania wamejaa kiwandani, hawatoki nje labda jumapili husombwa na basi na kuzungushwa mjini.

Hiki kiwanda hugawa pesa kwa watumishi wa uhamiaji na idara ya kazi kuwalinda hawa wahindi wanao fanya kazi ambazo Watanzania wana uwezo wa kuzifanya.

Pia kuna kituo cha kulea watoto wenye mahitaji maalum hapa hapa Arusha kinaitwa SUBISISO. Wamemuajiri dada toka nchi jirani hana vibali vya kazi walakuishi Tanzania. Nae amekuwa mtoa hongo Uhamiaji na idara ya kazi ili aendelee kuwa nyanyasa wafanyakazi walio chini yake.

Hii nchi kumekuwa na mambo ya aibu mnoo. Au ndio ile ruhusa ya kula urefu wa kamba?
 
Waliobaki watie akili !!
Yaani maafisa wanaofanya vitendo hivyo vya rushwa, unyanyasaji n.k warudi tena kambini wakajifunze upya ingali kuna vijana wako mtaani miaka kadhaa na vyeti vyao hawana kazi!?

Hakuna cha msalia mtume, inatakiwa vibarue viote mbawa akili ziwakae vizuri.

Pund afe mzigo wa bwana ufike.
 
Back
Top Bottom