Askari trafik no. F 3652 anakula rushwa

Askari trafik no. F 3652 anakula rushwa

Wewe acha u bushlawyer krek ni krek tu kama haungekuwa na kosa si ungeenda nae kituoni.
Msitete ujinga trafiki anatakiwa kukuelimisha kama kosa ni mara ya kwanza au akupatie barua ya onyo na zipo nyingi tu hizo karatasi zimechapishwa kwa fedha ya serikali hivyo askari wanatakiwa kuelimisha kwanza kabla ya kukimbilia faini hiyo ni njia ya kutaka rushwa .muhimu hizi fedha za faini zilipwe bank mwisho wao huo.
 
Labda namna ya kuwasilisha maelezo yake ninachokifahamu ni kuwa taratibu zao ni kuwa wanatakiwa kupeleka makosa sitini kiidadi kwa mwezi hivyo ni sawa na makosa mawili kila siku ya mungu iendayo.

Kumbuka siku anazoenda kazini hazifiki 30 ndugu.
Makosa 60 kwa siku chini ya 25(kuna mapumziko)
 
Msitete ujinga trafiki anatakiwa kukuelimisha kama kosa ni mara ya kwanza au akupatie barua ya onyo na zipo nyingi tu hizo karatasi zimechapishwa kwa fedha ya serikali hivyo askari wanatakiwa kuelimisha kwanza kabla ya kukimbilia faini hiyo ni njia ya kutaka rushwa .muhimu hizi fedha za faini zilipwe bank mwisho wao huo.
Hivi wale sio binadamu kama mimi na wewe??
Madereva barabarani mna nyodo sana mnawaona kama milingoti.
Mimi na wewe hatujui walijibishanaje hadi kufika huko.
Sio wote wakikutwa na kosa wanalimwa faini au kutoa rushwa

Acheni hizo
 
...kata ngumi tambaa na chombo teh teh...
 
Kamanda Mpinga askari wako wa barabarani (Trafik) mwenye Namba F.3652. Ni mfupi mweupe. Leo muda mfupi uliopita kanisimamisha nikiwa naendesha gari maeneo ya makutano ya barabara ya shekilango na Morogoro, baada ya kuona sina kosa akanambia nimpe elfu 10,000 niende nikakataa akaamua kuniandikia faini eti side mirror ina cracks. TAKUKURU na wanaohusika mchunguzeni.
Shit!!yani ugomvi wetu wa mademu unaufikisha kwa bosi wangu mkuu?Yani kukwambia achana na demu wangu ndio umeamua kunitengenezea sred ndg???si uungwana kiongozi.Anyway ngoja nimsubiri bosi wangu aseme chochote kisha ntajua cha kukufanya!
 
kama ulikutwa na kosa,hata dogo kiasi gani,ulitakiwa kuhukumiwa kwa kosa lako. Mi nilijua haukua na hata tone la kosa! kama ulishindwa kuongea vizuri nae,usituletee umbea hapa!

Swat lakini afande hakua na sababu ya KUOMBA RUSHWA
 
Last edited by a moderator:
We unatwanga maji kwenye kinu. Serikali kila kukicha inaandaa mianya mipya ya rushwa ili vijana wake watoke shavu. Nenda pale KAMATA kwenye traffic lights uone jinai wapanda pikipiki wanavyokamatwa kimanyanyaso na askari na vijamaa vingine vya CCM na mara baada ya kukamatwa kuna kakivanda ka polisi ndio kanatumika km mahakama ya kuamua rushwa kiasi gani utoe.

Siamini km kweli huu sio mpango wa pamoja
 
na wewe hiyo 10000 ulitoa ya nn faini mngeenda mpaka kituo ukawaambie ukweli kuhusu hili kukimbilia humu ni ujinga


inaonekana hujasoma vzur nilichokiandika,soma afu ndo utoe comment,matakoweeeeee!kill
 
Huo ni mradi wa trafiki na unafanywa bila kificho miongoni mwao. Kuna mwingine alikuwa pale ubungo stend anaitwa Kamote anachukua rushwa mchana ya jua kali, tena wanakuingiza pale kituoni na kukuambia uweke hiyo hela mezani!
 
Hivi nchi hii ndio mnapiga kelele swala la rushwa!!!
Sasa ukitaka kujua rushwa nzuri angalia sakata la viungo vya binadam litakapoisha..
Ukijua kuitumia rushwa raha sana.
 
Wewe acha uzushi kama mlishindwa kuelewana si useme tu. Ni askari gani wa barabarani asiyechukua ubani hasa hichi kipindi cha sikukuu. Au ni mtumishi gani wa serikali hatachukua chau chau akipata hiyo nafasi ? Wewe mwenye hiyo gari kama zio wizi tuambie hela ya kkulinunua ulipata wapi ? Acha unafiki katika kipindi hiki kigumu cha mfungo.
 
nchi hi isha feli ktk kuzuia rushwa.......rushwa itaendelea kuwepo
 
Nawashukuru sana ma trafiki, maana nakutwa na makosa kama ma tatu lakini nampa elfu tano ananiacha. Trafiki endeleeni kuwa na moyo wa huruma kama huu.
 
Mkuu watu8, hivi hili huwa ni kweli!??



Mkuu Escoba, endelea hivyo hivyo kuikataa rushwa. Nenda katengeneze side mirror ya gari lako ili siku nyingine asiwe na sababu ya kukuandikia hata notification!



Rushwa ni ugonjwa wa taifa. Huenda kweli huyo askari hapo awali alitaka rushwa na baada ya kukataliwa akaamua amtoze faini kwa kosa la crack kwenye kioo. Kosa kama hilo kawaida mtu hupewa onyo.

Mimi niongezee kuwa;

- Ni wajibu wa kila raia kukataa (R) kukataa rushwa - kuomba na kutoa!

- Jitahidi kutengeneza chombo chako cha usafiri na kuendesha kwa usalama wakati wote. Hii ni kwa ajili ya usalama wako na watumiaji wengine wa njia za usafiri

- Hakikisha unafuata sheria (hasa za barabarani) na kuzitii

- Jitahidi kuwa na lugha nzuri unaposimamishwa na askari - you will be shocked matokeo yake yatakavyo kuwa!

- Tusiache kutoa ripoti kwa viongozi wa Polisi pale tunapopewa huduma pungufu na mategemeo/haki yetu.

- Tusiache kuwatia moyo na kutoa ushirikiano kwa Polisi pale tupatapo nafasi/uwezo wa kufanya hivyo.


Wenu x-polisi, Mentor.

Pia unapoombwa vijisenti kama hivo acha ubishi toa ona sasa umelipa zaidi.crack kwenye mirror ni kosa pia
 
Last edited by a moderator:
kumbe wewe hujasoma kichwa cha habari ameandika kuwa askari mwenye Namba hizo anakura rushwa soma vizuri.

Hii ndio namba ya kamanda Mpinga 0754 360 046 pia anapatikana whataspp. mpigieni kukata mzizi wa fitna. Hua haachi kupokea simu. ni mkweli na muwazi na ni mtu hodari
 
Back
Top Bottom