mkonomtupu
JF-Expert Member
- Jul 5, 2011
- 441
- 118
Jana majira ya jioni, nikiwa naangalia mpira, mida ya saa moja usiku. Rafiki yangu ambaye ni askari ambaye yuko Mkuranga alinipigia simu akinitaarifu kuwa kuna askari mwenzao anayejulikana zaidi kama Tekamaji, amegongwa na Landcruiser wakati yupo doria, barrier eneo la mizani Mkuranga maarufu kama Magogo Matatu.
Alikuwa on duty na askari wenzake, ambapo marehemu alikuwa analisimamisha gari hilo kwa tochi kwa ishara ya kuichezesha ili dereva asimame.
Inaonekana dereva alikuwa mwendo kasi sana, hivyo basi badala ya kusimama, alimgonga askari huyo, na kukimbia baadae alilitelekeza gari na kukimbia kwa miguu.
Marehemu alichukuliwa na ambulance, na kupelekwa hospitali ya Wilaya. Lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya na kukimbizwa Muhimbili, na alipofika huko hali ilizidi kuwa mbaya na hatimaye alifariki.
Alikuwa on duty na askari wenzake, ambapo marehemu alikuwa analisimamisha gari hilo kwa tochi kwa ishara ya kuichezesha ili dereva asimame.
Inaonekana dereva alikuwa mwendo kasi sana, hivyo basi badala ya kusimama, alimgonga askari huyo, na kukimbia baadae alilitelekeza gari na kukimbia kwa miguu.
Marehemu alichukuliwa na ambulance, na kupelekwa hospitali ya Wilaya. Lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya na kukimbizwa Muhimbili, na alipofika huko hali ilizidi kuwa mbaya na hatimaye alifariki.