R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,573
MMOJA wa askari wa bandari, Cornell Kufahaizuru aliyeshiriki operesheni ya kuzuia jaribio la wizi wa shaba na mafuta Bandari ya Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, juzi ametekwa na watu wanaodaiwa ni wahusika wa jaribio hilo.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe zilieleza kuwa juhudi za kumtafuta zinafanywa na vyombo vya dola nchini.
Licha ya Dk Mwakyembe,chanzo kingine cha habari cha kuaminika kutoka Kitengo cha Ulinzi na Usalama katika bandari hiyo, kimethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Waziri Mwakyembe alisema Kufahaizuru alitoweka siku moja baada ya kupambana na katika zoezi la wizi huo, hajulikani alipo.
Juhudi za kumtafuta huyo kijana na waliomteka zinaendelea, lakini mpaka sasa hajapatikana ingawa kuna taarifa zisizo rasmi zinazoeleza kuwa kuna maeneo huwa anaonekana, alisema Dk Mwakyembe na kuongeza:
Uhalifu wa aina hii ni mpya kabisa, huu ni ukurasa mpya wa uhalifu nchini lazima tupambane nao, unaweza kuufananisha na zile filamu za nchini Nigeria.
Awali, askari mmoja katika kitengo cha ulinzi bandarini hapo kwa sharti la kutotajwa, alidaiKufahaizuru alitekwa na watu wasiojulikana juzi.
Alisema jana kuanzia saa 7:00 mchana walianza kupokea ujumbe mfupi wa maneno kutoka simu ya askari huyo, ukitoa masharti ya kuachiwa kwa wahusika wote waliokamatwa kwa tuhuma za kuhusika na jaribio la wizihuo.
Chanzo hicho kinadai kuwa, watekaji hao wametoa saa 24 kutimizwa kwa sharti hilo na iwapo halitatekelezwa kwa wakati, wametishia kumuua askari huyo.
Kuhusu hatua zilizochukuliwa mpaka sasa za kumwokoa askari huyo, chanzo kingine cha habari kutoka ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama, kimedai kuwa wanafanya kila linalowezekana na wameshaanza rasmi msako mkubwa wa kuwasaka wale wote wanaohusika na utekekaji huo na wanatarajia kuwanasa muda wowote.
Ofisa Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama wa Bandari, Mranda hakukanusha wala kukubali na kudai kuwa yuko safarini akirejea Dar es Salaam.
Jumamosi iliyopita, watu 10 wakiwamo polisi wawili walikamatwa kwa tuhuma za kutaka kuiba shaba katika bandari hiyo.Shaba hiyo iliyokuwa katika kontena, inakadiriwa kuwa na thamani ya Sh1 bilioni na ilikuwa iibwe saa 9:00 usiku wa kuamkia juzi.
Tukio hilo linadaiwa lilikuwa likiratibiwa na polisi kadhaa wakiwamo wa Kikosi cha Mamlaka Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara), walioingiza bandarini kichwa cha treni pamoja na watu wengine wanane kwa ajili ya kutekeleza wizi huo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi, askari wa bandari walipata taarifa za kuwapo kwa uhalifu huo na kwenda eneo hilo na walikuta watuhumiwa hao wakipakia shaba hiyo.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe zilieleza kuwa juhudi za kumtafuta zinafanywa na vyombo vya dola nchini.
Licha ya Dk Mwakyembe,chanzo kingine cha habari cha kuaminika kutoka Kitengo cha Ulinzi na Usalama katika bandari hiyo, kimethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Waziri Mwakyembe alisema Kufahaizuru alitoweka siku moja baada ya kupambana na katika zoezi la wizi huo, hajulikani alipo.
Juhudi za kumtafuta huyo kijana na waliomteka zinaendelea, lakini mpaka sasa hajapatikana ingawa kuna taarifa zisizo rasmi zinazoeleza kuwa kuna maeneo huwa anaonekana, alisema Dk Mwakyembe na kuongeza:
Uhalifu wa aina hii ni mpya kabisa, huu ni ukurasa mpya wa uhalifu nchini lazima tupambane nao, unaweza kuufananisha na zile filamu za nchini Nigeria.
Awali, askari mmoja katika kitengo cha ulinzi bandarini hapo kwa sharti la kutotajwa, alidaiKufahaizuru alitekwa na watu wasiojulikana juzi.
Alisema jana kuanzia saa 7:00 mchana walianza kupokea ujumbe mfupi wa maneno kutoka simu ya askari huyo, ukitoa masharti ya kuachiwa kwa wahusika wote waliokamatwa kwa tuhuma za kuhusika na jaribio la wizihuo.
Chanzo hicho kinadai kuwa, watekaji hao wametoa saa 24 kutimizwa kwa sharti hilo na iwapo halitatekelezwa kwa wakati, wametishia kumuua askari huyo.
Kuhusu hatua zilizochukuliwa mpaka sasa za kumwokoa askari huyo, chanzo kingine cha habari kutoka ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama, kimedai kuwa wanafanya kila linalowezekana na wameshaanza rasmi msako mkubwa wa kuwasaka wale wote wanaohusika na utekekaji huo na wanatarajia kuwanasa muda wowote.
Ofisa Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama wa Bandari, Mranda hakukanusha wala kukubali na kudai kuwa yuko safarini akirejea Dar es Salaam.
Jumamosi iliyopita, watu 10 wakiwamo polisi wawili walikamatwa kwa tuhuma za kutaka kuiba shaba katika bandari hiyo.Shaba hiyo iliyokuwa katika kontena, inakadiriwa kuwa na thamani ya Sh1 bilioni na ilikuwa iibwe saa 9:00 usiku wa kuamkia juzi.
Tukio hilo linadaiwa lilikuwa likiratibiwa na polisi kadhaa wakiwamo wa Kikosi cha Mamlaka Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara), walioingiza bandarini kichwa cha treni pamoja na watu wengine wanane kwa ajili ya kutekeleza wizi huo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi, askari wa bandari walipata taarifa za kuwapo kwa uhalifu huo na kwenda eneo hilo na walikuta watuhumiwa hao wakipakia shaba hiyo.