Asiyetunza watu wa nyumbani mwake

Asiyetunza watu wa nyumbani mwake

Mrs Gudman

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2015
Posts
613
Reaction score
1,300
Habari za asubuhi,Leo nimeamka na tafakari hii Ni baada ya kusoma Visa vingi mitandaoni vikieleza jinsi ambavyo baadhi ya familia zimepoteza muelekeo/watu wameacha msingi,Sijui Ni utandawazi ama Ni Nini lakini mambo yamebadilika sana.

Kumekuwa na wimbi kubwa la kina baba kutohudumia familia makusudically kabisa(acha wale ambao Hali imechangia).
Baba anakipato kabisa lakini ukimuuliza mara ya mwisho aliweka luku lini ajui,Alilipa ada lini ajui,alinunua chakula lini hakumbuki jukumu lote la kuprovide for family wameachiwa kina mama ,Kuna kina mama wamechukua majukumu yote ya ubaba na ya umama pia ,Kama haumo miongoni mwao hongera Sana usipanic Wala kusema hawapo wahurumie na muwaombee

Kundi la pili na kubwa waliozaa kabla ya ndoa ,kuachana au kutengana Hawa ndo wengi ,mara nyingi utasikia Kama anataka matumizi ya mtoto aende ustawi hahaha ,nikukumbushe tu my brother kutoa huduma kwa ajili ya damu yako ni IBADA,hutoi ili ifahamike unatoa hata mwanamke akikana hukutoa (Mana wapo wafanyavyo hivyo) bado haitafuta dhawabu yako mbele za Mungu.Angalia mifano ya watu ambao walishindwa kuthamini watoto zao Leo wanavyohangaika kurudisha mahusiano kwa ugumu,
Mahusiano mazuri hujengwa wakati wa utoto na si kwenye utu uzima

Soma hi

Lakini kama mtu hawatunzi watu wa jamaa yake, hasa wale wa nyumbani kwake, basi, mtu huyo ameikana imani, na ni mbaya zaidi kuliko mtu asiyeamini

Najua zipo changamoto hasa zile zinazosababishwa na wanafamilia wenyewe au wazazi wenza lakini mwanaume rijali Ni yule anayeweza kukabiliana na vikwazo ili kutimiza adhima yake.

Nikutakie tafakuri njema
 
Ni kweli lakini familia za kiafrika ni kubwa mmno,
Ukisema umtunze kila mtu huwezi kuwa na maendeleo yoyote
Hasa wale wa NYUMBANI KWAKE ,(Yani watoto,mke na wajakazi )
 
Ni kweli lakini familia za kiafrika ni kubwa mmno,
Ukisema umtunze kila mtu huwezi kuwa na maendeleo yoyote
Priorities, jua kuwa immediate family ni wewe uliileta duniani, huna budi kuihudumia. Extended family wazaziwna ndugu ni jukumu lako na ndugu zako since Africa hatuna social security safe net, family ndiyo msaada.
 
Priorities, jua kuwa immediate family ni wewe uliileta duniani, huna budi kuihudumia. Extended family wazaziwna ndugu ni jukumu lako na ndugu zako since Africa hatuna social security safe net, family ndiyo msaada.
Yes sicy,hapa Sana sana nalenga familia kwa maana ya baba mama na watoto ,Yani hata levo hii ya awali kabisa Kuna watu bado wameitupa ,Yani uzae mtoto wa damu yako ushindwe kumpa mahitaji hasa hasa ndo nalenga ndugu wengine itategemea na uwezo wako
 
Ni kweli lakini familia za kiafrika ni kubwa mmno,
Ukisema umtunze kila mtu huwezi kuwa na maendeleo yoyote
Afrika ni shida sana. Ukitoa huduma nzuri nyumbani kwa wazazi wako, na wao wanahamishia hapo vijukuu vyao na ndugu wengine. kwa hiyo badala ya kuhudumia wazee wako yaani baba na mama , unakutana na watu kama kumi wengine hapo nyumbani kwa wazee. Ni shida sana Afrika
 
Afrika ni shida sana. Ukitoa huduma nzuri nyumbani kwa wazazi wako, na wao wanahamishia hapo vijukuu vyao na ndugu wengine. kwa hiyo badala ya kuhudumia wazee wako yaani baba na mama , unakutana na watu kama kumi wengine hapo nyumbani kwa wazee. Ni shida sana Afrika
Uzi huu umelenga zaidi watoto na mke
 
Habari za asubuhi,Leo nimeamka na tafakari hii Ni baada ya kusoma Visa vingi mitandaoni vikieleza jinsi ambavyo baadhi ya familia zimepoteza muelekeo/watu wameacha msingi,Sijui Ni utandawazi ama Ni Nini lakini mambo yamebadilika sana.

Kumekuwa na wimbi kubwa la kina baba kutohudumia familia makusudically kabisa(acha wale ambao Hali imechangia).
Baba anakipato kabisa lakini ukimuuliza mara ya mwisho aliweka luku lini ajui,Alilipa ada lini ajui,alinunua chakula lini hakumbuki jukumu lote la kuprovide for family wameachiwa kina mama ,Kuna kina mama wamechukua majukumu yote ya ubaba na ya umama pia ,Kama haumo miongoni mwao hongera Sana usipanic Wala kusema hawapo wahurumie na muwaombee

Kundi la pili na kubwa waliozaa kabla ya ndoa ,kuachana au kutengana Hawa ndo wengi ,mara nyingi utasikia Kama anataka matumizi ya mtoto aende ustawi hahaha ,nikukumbushe tu my brother kutoa huduma kwa ajili ya damu yako ni IBADA,hutoi ili ifahamike unatoa hata mwanamke akikana hukutoa (Mana wapo wafanyavyo hivyo) bado haitafuta dhawabu yako mbele za Mungu.Angalia mifano ya watu ambao walishindwa kuthamini watoto zao Leo wanavyohangaika kurudisha mahusiano kwa ugumu,
Mahusiano mazuri hujengwa wakati wa utoto na si kwenye utu uzima

Soma hi

Lakini kama mtu hawatunzi watu wa jamaa yake, hasa wale wa nyumbani kwake, basi, mtu huyo ameikana imani, na ni mbaya zaidi kuliko mtu asiyeamini

Najua zipo changamoto hasa zile zinazosababishwa na wanafamilia wenyewe au wazazi wenza lakini mwanaume rijali Ni yule anayeweza kukabiliana na vikwazo ili kutimiza adhima yake.

Nikutakie tafakuri njema

Halafu wanaume wa aina hii ndo wanaongoza kwa kuchepuka kwa kisingizio cha kuwa wake zao wamejisahau na hawana tena zile mbwembwe za kitandani kama mwanzo yaani mwamaume mzima na ndevu zake hana hata aibu anaongea hivyo

Tatizo wanaume wa hivyo wanapataga wanawake mazwanzwa yaani mimi ningepata mume wa hivyo mbona asingenisumbua hata kidogo kitu ningemfanya asingekuja kusahau hadi anaingia kaburini maana huyo siyo mume tena bali ni takataka hiyo
 
Halafu wanaume wa aina hii ndo wanaongoza kwa kuchepuka kwa kisingizio cha kuwa wake zao wamejisahau na hawana tena zile mbwembwe za kitandani kama mwanzo yaani mwamaume mzima na ndevu zake hana hata aibu anaongea hivyo

Tatizo wanaume wa hivyo wanapataga wanawake mazwanzwa yaani mimi ningepata mume wa hivyo mbona asingenisumbua hata kidogo kitu ningemfanya asingekuja kusahau hadi anaingia kaburini maana huyo siyo mume tena bali ni takataka hiyo
Kama huna mume hongera,kama unaye ,aliyekuoa nampa pole
 
Kama huna mume hongera,kama unaye ,aliyekuoa nampa pole

Mpe hongera tu maana yeye siyo mwanaume wa aina hiyo yaani mwanaume nyumbani hauhudumii kila kitu anahangaika mwanamke halafu bado unachepuka kwa kisingizio cha kuwa mke wako kajisahau hakuridhishi tena kama zamani? Huyo ndo mwanaume ninayemuongelea

Hivi ungekuwa ndo wewe mwanaume unahangaika na kila kitu halafu mwanamke yupo yupo tu na bado anachepuka ungefanya nini? Mnapenda kujitetea kwenye kila kitu yaani hadi hapo napo unaona ni sawa tu mwanaume kuwa hivyo? Usimfanyie mtu kile usichopenda kufanyiwa
 
Back
Top Bottom