Asimamishwa kazi kwa kukamata Wanyarwanda porini

Nchi hii haikomi maajabu! Kuna taarifa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa Mkuu wa Pori la Burigi mkoani Kagera, kwa kosa la mkuu huyo kukamata ng’ombe 400 walioingizwa na raia wa Tanzania na Rwanda porini humo.

Pamoja na mifugo, wenye ng’ombe hao wamekamatwa wakiwa na nyara (wanyamapori waliouawa).

Kusimamishwa kwake kumetokana na shinikizo la Wabunge wa Kamati ya Utalii, Maliasili na Mazingira wakiongozwa na Mbunge Musukuma, waliotaka mifugo hiyo iachiwe mara moja bila masharti.

Inaelezwa kuwa Mkuu wa Pori anayeitwa Bigilamungu, alihoji uhalali wa kuachiwa kwa ng’ombe pamoja na watuhumiwa hao waliokamatwa wakiwa na nyara za Serikali. Kitendo cha kusita kutekeleza amri hiyo, kumegharimu kazi yake!

Sasa wabunge wanashinikiza hata Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Profesa Songorwa naye asimamishwe kazi!



My take: Sitaki kuhukumu, lakini ndugu zangu mtambue kuwa Uhifadhi nchi hii unauawa na wanasiasa. Tatizo la mifugo katika Mapori na Hifadhi zetu nchini ni kubwa mno kuliko hata ujangili.

-Naomba niwe mchochezi kwa kutoa mwito kwa Wakuu wa Mapori wote nchini kusimama imara kumtetea mwenzao, na hilo litawezekana tu endapo wataamua kuacha mifugo iingie kwenye Mapori na Hifadhi bila kizuizi! Hatuwezi kuendelea kuwachekea wanasiasa ambao utajiri wao unatokana na mifugo- maelfu kwa maelfu- wanayoingiza katika Mapori na Hifadhi zetu.
Taarifa yako siyo sahihi, mambo hayaendagi hivyo hata Siku moja, labda KWA kuwa hujui ukweli wa jambo lenyewe. Mara nyingi hao wahifadhi huruhusu MIFUGO kuingia kwnye mapori baada ya kupewa rushwa.
 
Kagame ni Rafiki ya mkuru hagusiki.Watanzania 56 waliuwawa kagera tuko kimya Rafiki yetu anatutawala
Ukikaidi amri ya kukamatwa na wanajeshi basi utarazimishwa ukamatwe KWA risasi na hapo akiikosa miguu yako kitafuata ni kifo mjomba.
 
Nilipita lile pori mwezi uliopita nikashangaa sana. Tulikuwa tunakutana na wanyama kuanzia mlima simba mpaka Kasindaga. Sasa hivi tunakutana na makundi makubwa ya ng'ombe kila sehemu ya poli hilo. Na kweli kabisa wanaochunga mle ni wanyarwanda maana hawa watu hawjifichi hata kwa kuwaangalia tu. Nilijaribu kuwauliza walinzi wa huo msitu (polisi wa doria) nao walilalamika na kusema kuwa ukimkamata mfugaji wa kinyarwanda basi huna kazi. Hata nao mapolisi walionyesha kutopenda hiyo hali.
Mwigulu Nchemba bila shaka umeisoma hii maana polisi wapo chini ya wizara yako.
 
Mkuu Mpiganaji Comredi Manyerere, this is too good to be true, lazima kuna a missing link in between, huyo mtoa habari wako hakukuambia, haiwezekani mtu akamate muhalifu na ushahidi wa nyara alafu yeye ndie aadhibiwe, kisha wamtake na mkurugenzi wanyamapori awajibike!, I belive there is more than what meet the eye, just time will tell.

Nilimsikia huyu Musukuma kwenye two series za interview yake Star TV, huyu sio mzima, ila kama amefanikiwa kuiconvince kamati yote ya bunge kumuwajibisha huyo Bigilamungu, ujue huyo jamaa ana madudu yake makubwa zaidi, ukiyasikia, utanielewa!. Hapa ninamaanisha kasimamishwa kazi kwa mengine, hayo ni chambo tuu, lets wait and see.

Tusiilaumu kamati, wala kulaani kilichotokea hadi tupate facts zote at hand, kwa sababu, nimeishashuhudia mifugo iliyokamatwa ikiteswa kuzuiliwa na kufa njaa huku wenye mifugo wakiwa chini ya ulinzi, mifugo inayochungwa, haina makosa yoyote ya mifugo hiyo kuadhibiwa, inapoingizwa popote kwenye malisho, na madhumuni ya mapori yote ya akiba ni utunzaji wa miti na uoto wa asili na sio nyasi!. Kwa maoni yangu, hakuna ubaya wowote kulisha mifugo pori la akiba as long as lengo sio uchomaji misutu, ukataji kuni, uchomaji mkaa na uwindaji haramu!, usikute hizo nyara walizokamatwa nazo ni nyama ya Swala au digidigi, na hakuna details, waliizuia kwa siku ngapi hadi walipoamriwa kuiachia!.

Get more details tuweze kuijadili hii issue kwa mizania ya haki, hapa ilipo bado ni one sided na single source ya upande wa utetezi kwa Bigilamungu.

Pasco

Pasco
Hata ikisemwa si kosa kuchunga ng'ombe hao wanyarwanda wakachungie huko kwao sio kwenye nchi yetu.
 
kweli tunatakiwa kuikosoa serikali pale panye udhaifu.

Lakini hili la kuleta taarifa za uongo nalo linakuwa faida gani.??

Hivi ukishatoa habari za uongo na watu wakiiponda serikali kwa sababu ya umbeya wako hivi unafaidika na nini??
watanzania nani kawaloga ninyi??
 
Nchi hii haikomi maajabu! Kuna taarifa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa Mkuu wa Pori la Burigi mkoani Kagera, kwa kosa la mkuu huyo kukamata ng’ombe 400 walioingizwa na raia wa Tanzania na Rwanda porini humo.

Pamoja na mifugo, wenye ng’ombe hao wamekamatwa wakiwa na nyara (wanyamapori waliouawa).

Kusimamishwa kwake kumetokana na shinikizo la Wabunge wa Kamati ya Utalii, Maliasili na Mazingira wakiongozwa na Mbunge Musukuma, waliotaka mifugo hiyo iachiwe mara moja bila masharti.

Inaelezwa kuwa Mkuu wa Pori anayeitwa Bigilamungu, alihoji uhalali wa kuachiwa kwa ng’ombe pamoja na watuhumiwa hao waliokamatwa wakiwa na nyara za Serikali. Kitendo cha kusita kutekeleza amri hiyo, kumegharimu kazi yake!

Sasa wabunge wanashinikiza hata Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Profesa Songorwa naye asimamishwe kazi!



My take: Sitaki kuhukumu, lakini ndugu zangu mtambue kuwa Uhifadhi nchi hii unauawa na wanasiasa. Tatizo la mifugo katika Mapori na Hifadhi zetu nchini ni kubwa mno kuliko hata ujangili.

-Naomba niwe mchochezi kwa kutoa mwito kwa Wakuu wa Mapori wote nchini kusimama imara kumtetea mwenzao, na hilo litawezekana tu endapo wataamua kuacha mifugo iingie kwenye Mapori na Hifadhi bila kizuizi! Hatuwezi kuendelea kuwachekea wanasiasa ambao utajiri wao unatokana na mifugo- maelfu kwa maelfu- wanayoingiza katika Mapori na Hifadhi zetu.

Una uhakika! Ama ni uzushi?
Kwani hakuna serikali?
Na vipi anaweza kuonewa na kusimamishwa bila kosa wakati kila vyombo vya serikali viko uko hata anaweza kujitetea na kusiklizwa.?
Kidogo nina mashaka na huu uzi!
 
kweli tunatakiwa kuikosoa serikali pale panye udhaifu.

Lakini hili la kuleta taarifa za uongo nalo linakuwa faida gani.??

Hivi ukishatoa habari za uongo na watu wakiiponda serikali kwa sababu ya umbeya wako hivi unafaidika na nini??
watanzania nani kawaloga ninyi??
Wewe mtutsi nini? Maana ungekuwa mtanzania usingeandika hivyo kwenye blue bold. Kama unaona taarifa ni ya uongo kwanini usiseme ukweli unaoujua wewe?
 
Aliyesema mwezi moja na nusu haitazid miwili mpaka leo kimya na bado ana dunda na hakuna mtu aliyemtumbua

-Aliyesema GPA ya 3.5 baadae ikawa GPA 3.0 naye bado anadunda hakuna alitemtumbua

-Yule aliyeuza nyumba za serikali kipind akiwa waziri naye ana dunda tu hakuna aliyemtumbua

-Yule anayekomaa na uhakiki miezi nenda rudi naye yupo ana dunda tu

-Yule aliyehaidi milion 50 kila kijiji mpaka leo hajatumbuliwa ana dunda tu.

Huu mchezo wa kucheza na maisha ya watu utaisha lini?
YAKUAMBIWA CHANGANYA NA YAKO.
 
Wewe mtutsi nini? Kama unaona taarifa ni ya uongo kwanini usiseme ukweli unaoujua wewe?
Jina lako tu linatia mashaka
MWANAPROPAGANDA.
Pole kwa hilo, kwasababu wengi wetu watanzania tunapenda kudanganywa kuliko ukweli.
Wewe endelea tu na propaganda zako hapo, mpaka utakapokuja kupata ukweli tayari muda umeshakutupa mkono.
 
Hao wabunge/mawaziri wanaoshabikia kila jambo ni mzigo mkubwa kwa taifa.Naomba JPM awaangalie kwa jicho la Tatu.!
 
Back
Top Bottom