Asili ya neno Mbeya

Uyole CTE

Member
Apr 17, 2015
7
12
Historia ya mkoa wa Mbeya imegawanyika katika vipindi tofauti tofauti kabla ya uhuru na baada ya uhuru, Mji wa Mbeya ulianzishwa na wakoloni waingereza mnamo mwaka 1927, Wakati huo dhahabu ilianza kupatikana sana katika milima iliyopo karibu na Mbeya hadi Chunya hivyo Mbeya ulikuwa ni mji wa mapumziko kwa Wazungu kutokana na hali yake nzuri ya hewa.

katika kipindi cha ukoloni ulifahamika kama "Southern highland provience" kwa kujumuisha baadhi ya maeneo ya mikoa ya Iringa na Rukwa na baadaye Mbeya. Asili ya neno Mbeya imekuwa na nadharia kadha wa kadha ambazo zinaelezwa na wataalam na wazee mbalimbali, Baadhi ya nadharia hizo ni pamoja na:-

1. Ibheya - Chumvi
Nadharia hii inaeleza kuwa asili ya Neno Mbeya ni neno la kisafwa "Ibheya" lenye maana ya chumvi, Hii inatokana wafanyabiashara kufika katika mji huu na kubadirishana mazao yao kwa chumvi iliyokuwa ikipatikana kwa wingi kipindi hicho. Ikapeleka wenyeji kuita eneo hili Ibheya kama sehemu ya kubadilishia chumvi na mazao, kutokana na sababu za kimatamshi ikapelekea wageni kuzoea kutamka na kuandika Ibheya.

2. Agamba mbeye - Kamlima Mbeye
Nadharia hii inaeleza kuwa jina Mbeya limetokana na Mlima uliopo nyuma ya Chuo cha Kilimo Uyole (Agricultural Research Institute -ARI- Uyole) uliojulikana kwa jina la kisafwa kama Agamba Mbeye (kamlima Mbeye kwa kiswahili) Ambao hivi sasa ni maarufu sana kwa jina la Mlima ugari, ni mlima ambao una muonekano wa mviringo, sehemu za chini umeota nyasi japo si nyingi sana kama ilivyo sehemu ya juu ambayo haioti nyasi kabisa, hivyo ikawa sehemu nzuri ya kupumzikia wageni ili kupata hewa nzuri na muonekano mzuri wa mji, kutokana na changamoto za kimataishi ikapelekea wageni kuliendeleza sana jina la eneo kama Mbeya kimaandishi na kimatamshi.

Ibheya.JPG
 
Mimi nilijua labda pia watakuwa na tabia ya umbeya ndio maana ukaitwa hivyo..!
 
Hii ya pili ina mantiki zaidi kua ukaribu sana kati ya MBEYA na MBEYE.
 
Ndio mkuu,Wanaykyusa kwao ni Rungwe,ila kwa makelele yao na kuwahi kwenda shule ndio wakaonekana wenyewe ndio wenyeji/wazawa halisi wa Mbeya
Kweli ndo maana hata wasafwa sasa weng hujiita wanyaki ...shule muhmu.ni kama wazalamo dar
 
Ubishi na kujifanya wajuaji ndo kumepelekea mji wa Mbeya kupangika vibaya
 
Chuo cha kilimo uyole hakuna mlima pale mlima uko kule juu nmb bank acha uongo
 
Chuo cha kilimo uyole hakuna mlima pale mlima uko kule juu nmb bank acha uongo
mnazungumzia milima tofauti. Mwenzako anazungumzia mlima Ugali. Nimwewahi panda haka ka mlima. ukiwa juu pale kanapoteza ule muonekano wa mviringo.
 
Kweli ndo maana hata wasafwa sasa weng hujiita wanyaki ...shule muhmu.ni kama wazalamo dar

Kweli Wanyakyusa kwa hasa ni Rungwe. Mbeya mjini walikuwa wanakuja kufanya vibarua vya kulima mashamba ya wasafwa. Walipoanza kuwa wengi Wasafwa wakaamua kuenda kukaa milimani. Kimsingi Wanyakyusa wamewahi kuwa 'watumwa' wa Wasafwa. Usishangae sana ndio mambo ya historia. Hata Waingereza Wana kelele sana leo lakini wamewahi kutawaliwa na Denmark na pia Warumi.
 
Ubishi na kujifanya wajuaji ndo kumepelekea mji wa Mbeya kupangika vibaya

Wanajionaaaa, malaya na siku hizi wanajidai kuokoka. Ni kabila linaloongoza kwa kuzalisha wachungaji uchwara. Modern Masadukayo
 
Ndio mkuu,Wanaykyusa kwao ni Rungwe,ila kwa makelele yao na kuwahi kwenda shule ndio wakaonekana wenyewe ndio wenyeji/wazawa halisi wa Mbeya

Siku hizi makabila yote Mbeya yanasomesha watoto wao. No more mwa mwa mwa .....
 
Kweli Wanyakyusa kwa hasa ni Rungwe. Mbeya mjini walikuwa wanakuja kufanya vibarua vya kulima mashamba ya wasafwa. Walipoanza kuwa wengi Wasafwa wakaamua kuenda kukaa milimani. Kimsingi Wanyakyusa wamewahi kuwa 'watumwa' wa Wasafwa. Usishangae sana ndio mambo ya historia. Hata Waingereza Wana kelele sana leo lakini wamewahi kutawaliwa na Denmark na pia Warumi.
Ahahaha ko watawala waliwakimbia watumwa?
 
Back
Top Bottom