mult_talented_p
Senior Member
- Oct 10, 2016
- 103
- 120
Miezi kadhaa iliopita, Mungu alinifikisha mkoani Mwanza kwa ajili ya kufanya mafunzo yangu ya vitendo yaani (field practice). Kwakuwa nilikuwa mwenyeji wa Dar nilishangaa sana kuona kuwa hapo Mwanza hapakuwepo na kunguru, kama wa Dar.
Nilijaribu kudadisi na kuuliza kwa nini Mwanza hamna kunguru. Mwenyeji mmoja niliyekutana nae kwenye mabasi ya umma yaani public transport, alinidokeza kuwa, kunguru walikuwepo au wapo jijini Mwanza, lakini hawaonekani sana.
Hivi majuzi nikiwa chuoni kwetu hapa Iringa mjini, nilishangaa kuona kunguru wakubwa, wakiwa wana koti (baka) jeupe vifuani mwao. Kunguru aina hio, niliwaona sehem zingine, mbali na Dar es salaam, hususan, mikoa ya ndani ndani ya Tanzania bara.
Baada ya kuulizia juu ya tofauti wa kunguru wa huku mikoani, na wale wa Dar es salaam, nikapata majibu ambayo yalitatua mgogoro ndani ya kichwa changu, majibu ambayo yalinipendeza kushare na jamii.
Kunguru weusi, yaani Indian House Crow (Corvus splendens) wanaopatikana maeneo ya Zanzibar, Dar es salaam na mikoa mingine ya Pwani, asili yake ni India.
Hawa kitaalamu wanaitwa invasive species, na waliletwa huku ili kudhibiti tatizo la taka lilikowako kipindi hicho, visiwa vya Zanzibar mwaka 1901. Kunguru hawa wana tabia ya kula vitu vingi, hivyo kwa wakati huo, walifaa sana kwa kutatua tatizo la taka.
Kwa kuwa wakiwa huku, hawana ndege wengine wanaoweza kuwala (predators) hao Indian House Crow waliendelea kuzaliana na kusambaa kwenye mikoa ya pwani na hata nchi jirani.
Mpaka leo Indian House crow ni wengi maeneo ya Dar es salaam na wakati mwingi wamekuwa wakidokoa vifaranga vya kuku, na ndege wengine sasa wako hatarini kupotea kwa ajili ya uwepo wa hawa Indian House Crow.
Namshukuru Mungu kipekee kabisa na mwalimu wetu.
Science has led me to understand this phenomena.
Nilijaribu kudadisi na kuuliza kwa nini Mwanza hamna kunguru. Mwenyeji mmoja niliyekutana nae kwenye mabasi ya umma yaani public transport, alinidokeza kuwa, kunguru walikuwepo au wapo jijini Mwanza, lakini hawaonekani sana.
Hivi majuzi nikiwa chuoni kwetu hapa Iringa mjini, nilishangaa kuona kunguru wakubwa, wakiwa wana koti (baka) jeupe vifuani mwao. Kunguru aina hio, niliwaona sehem zingine, mbali na Dar es salaam, hususan, mikoa ya ndani ndani ya Tanzania bara.
Baada ya kuulizia juu ya tofauti wa kunguru wa huku mikoani, na wale wa Dar es salaam, nikapata majibu ambayo yalitatua mgogoro ndani ya kichwa changu, majibu ambayo yalinipendeza kushare na jamii.
Kunguru weusi, yaani Indian House Crow (Corvus splendens) wanaopatikana maeneo ya Zanzibar, Dar es salaam na mikoa mingine ya Pwani, asili yake ni India.
Hawa kitaalamu wanaitwa invasive species, na waliletwa huku ili kudhibiti tatizo la taka lilikowako kipindi hicho, visiwa vya Zanzibar mwaka 1901. Kunguru hawa wana tabia ya kula vitu vingi, hivyo kwa wakati huo, walifaa sana kwa kutatua tatizo la taka.
Kwa kuwa wakiwa huku, hawana ndege wengine wanaoweza kuwala (predators) hao Indian House Crow waliendelea kuzaliana na kusambaa kwenye mikoa ya pwani na hata nchi jirani.
Mpaka leo Indian House crow ni wengi maeneo ya Dar es salaam na wakati mwingi wamekuwa wakidokoa vifaranga vya kuku, na ndege wengine sasa wako hatarini kupotea kwa ajili ya uwepo wa hawa Indian House Crow.
Namshukuru Mungu kipekee kabisa na mwalimu wetu.
Science has led me to understand this phenomena.