Asikudanganye mtu, "mtoto wa Nyoka ni Nyoka"

Asikudanganye mtu, "mtoto wa Nyoka ni Nyoka"

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
34,259
Reaction score
79,826
"MTOTO WA NYOKA NI NYOKA"

Na, Robert Heriel

Panya huzaa panya
Paka huzaa paka
Mbwa huzaa mbwa.,.....n.k

Mtoto wa nyoka ni nyoka, wahenga walisema kisha wakaongezea, maji hufuata mkondo. Baadaye Yesu wa Nazareth akasema; huwezi chuma tini kwenye zabibu" Hii ni kusema, muembe huzaa maembe, Mzabibu huzaa zabibu n.k

Malaya huzaa Malaya
Mwizi huzaa mwizi
Muuaji huzaa muuaji
Mdhulumaji huzaa mdhalumaji.

Kabla sijafika Mbali, nitoe lengo la Makala hii.

LENGO: Vijana tuwe makini katika chaguzi za maisha hasa tunapoenda kuchagua wenzi wa maisha. Kwani kwa kutokufanya hivyo inaweza kuleta athari baadaye.

Tuendelee sasa.

Huwezi muambia malaya aache umalaya ikiwa yeye ndio asili yake. Huwezi mwambia mchoyo aache uchoyo wakati yeye ndio asili yake. Huwezi mwambie mdhulumaji aache dhuluma wakati yeye ndio asili yake. Huwezi mwambia mvivu aache uvivu wakati hiyo ndio asili yake. Viumbe wote tuliomo humu duniani tunaongozwa na silika. Kila mtu anasilika yake kulingana na asili yake aliyoirithi kutoka kwa wazazi wake.

Siku hizi watu wanahangaika katika ndoa, siku hizi ni kawaida kwa ndoa kuvunjika kutokana na kutokuelewana ndani ya ndoa. Vijana wa siku hizi tumekosea sehemu nyeti sana ambayo ndio msingi wa mahusiano.

Vijana wanahangaika kutafuta wanawake warembo wa sura na maumbile. Wanahangaika kutafuta wanawake wenye matako makubwa, na nyonga nene. Wakati huo huo wanawake nao wanahangaika kutafuta wanaume wenye pesa na utajiri mwingi, wakitafuta wanaume wenye kazi zenye vipato vizuri. Wanahangaika kutafuta wanaume wazuri wa sura na warefu wa maumbile

Wanasahau jambo moja muhimu, "Mtoto wa Nyoka ni Nyoka" Wanasahau kuangalia tabia au silika za wazazi wa mwezi anayemtafuta.

Wakati wa zamani haikuwa hivyo, ilikuwa lazima uchunguzi ufanyike. Mchumba alikuwa akichunguzwa, tabia na silika za jamii yao, magonjwa na maradhi ya kurithi yao, imani, mila, na desturi zao, uchapakazi, kisha mwisho kabisa maumbile. Wazee wa zamani walikuwa na sababu kubwa na muhimu ya kufanya hivyo. Moja wapo ni kutokuharibu kizazi chao

Wazee wa zamani walijua kabisa mtoto wa nyoka ni nyoka. Endapo mzazi ni mchoyo, mwizi, malaya, muuaji basi hata watoto wake watakuwa hivyo. Na ndivyo ilivyo.

Kikawaida, ukitaka kuoa mwanamke yeyote yule lazima umuangalie mama yake, kisha uangalie ukoo wao na jamii aliyotoka kwa ujumla. Pia ukitaka kuolewa na mwanaume, basi sharti umuangalie Baba ya huyo mume mtarajiwa, kisha angalia ukoo na jamii anayotoka. Hapo ndio utajua tabia halisi ya mke wako baadaye atakapofikisha umri kama wa Mkwe wako huyo

Ukiona mtu ni malaya basi jua wazazi wake au mmoja kati ya mzazi wake ni Malaya. Ukiona Mtu ni mwizi basi jua kabisa wazazi wake au mmoja wa wazazi wake ni mwizi. Asilimia zaidi ya 99% mtoto hurithi tabia kutoka kwa wazazi wake iwe mama au baba au ukoo, au jamii husika ya wazazi wake.

Kuna watu wataniambia kuwa mbona kuna wazazi wanatabia nzuri, wengine ni wachungaji au mashehe lakini watoto wao wanatabia mbaya?
Jibu ni kuwa, wazazi hao ni wanafiki, hakuna mzazi mwenye tabia nzuri alafu mtoto akawa na tabia mbaya hiyo haipo na haitokuja kutokea. Kinachofanyika ni kuwa baadhi ya wazazi hujifanya watakatifu mbele ya jamii lakini kwa kificho hufanya maovu. Na kama hafanyi kabisa basi kimwili hafanyi maovu lakini nafsi yake inafanya uovu kwa kutamani kuufanya sema mazingira hayaruhusu.

Upo ushahidi wa kutosha kuwa jinsi mzazi alivyo ndivyo mtoto wake atakavyokuwa kwa sehemu kubwa. Kama Baba yako alioa na akaacha wanawake zaidi ya mmoja kabla hajazeeka basi kunauwezekano mkubwa nawe ukafanya vivyo hivyo.
Hata hapo mtaani, au angalia kwenye ukoo wenu, au familia yenu, fanya utafiti mdogo, Watoto wengi ambao Baba zao walitia Mimba na kutelekeza mabinti waliowatia mimba utashangaa nao asilimia kubwa wamefanya hivyo hivyo. Alafu wale ambao Baba zao walizaa kwenye ndoa bila kuzaa nje ya ndoa basi kwa asilimia kubwa nao wamefanya kama baba zao.

Pia chunguza, wamama wengi ambao wamezaa na mwanaume zaidi ya mmoja basi hata watoto wao nao kwa asilimia kubwa hufuata mtindo huo huo. Au Wamama ambao hawaishi na waume zao utashangaa hata watoto wao hawaishi na waume zao kwa asilimia kubwa. Lakini wamama ambao wameolewa na wamedumu kwenye ndoa mpaka uzee au mpaka mmoja wa wanandao amefariki basi watoto wao kwa sehemu kubwa huolewa na kudumu kwenye ndoa.

Unapooa au kuolewa lazima uzingatie kitu inaitwa Tabia ta mtu unayeenda kuoa au kuoelewa naye. Usiishie kwenye kutafuta uzuri au pesa, ukasababisha maafa kwenye kizazi chako.

Kuna watu wanasema tabia mtu anaweza kubadilishwa. Ni uongo. Tabia haibadiliki, tabia ni asili ya mtu. Inatoka ndani ya mtu sio nje. Tabia ni kama ngozi tu, ukiichubua kwa mafuta ya kemikali ili ngozi iwe nyeupe, itakuwa nyeupe lakini ndani ni nyeusi tuu. Ndio maana mtu hata ajichubue vipi awe mweupe kama mzungu lakini lazima azae mtoto mweusi.

Vivyo hivyo kwa tabia, unaweza ukajitahidi kuibadilisha tabia kwa sehemu kubwa, yaani kuichubua mpaka ukaonekana kweli umebadilika lakini kwa ndani hujabadilika. Utakuwa umeacha kwa nje tuu lakini kwa ndani tabia ile inaendelea. Tabia ukiizima inajificha kwenye unconscious mind. Yaani inakuwa kama haipo kumbe ipo. Tabia hiyo unairithisha kwa watoto na kama watoto hutowachubua basi itadhihirika.

Ndio maana unakuta mchungaji au sheikhe unawezamkuta swala tano na mtu mwema kwa nje, lakini watoto wake wakawa wahuni na waovu. Hiyo ni kutokana na tabia halisi ya wazazi au mmoja wa mzazi kuwa ni muovu au mhuni.

Hii pia unaweza ikuta kwa Watoto waliozaliwa na wazazi waovu au wahuni. Unaweza kuta mtoto amezungukwa na wahuni, lakini asiwe mhuni, asivute bangi, asiwe malaya licha ya kuzungukwa na malaya. Hii inatokana na kuwa, mzazi wake mmoja sio mhuni kiasili au sio malaya.

Na kama wazazi wote kiasili ni wahuni, malaya, wachawi, wachoyo piga ua garagaza huyo mtoto lazima awe na tabia hizo hizo.

Huwezi oa mwanamke malaya alafu ukamfanya aache umalaya, never ever. Utahangaika wee! Ukifanikiwa sana atafanya kwa siri kubwa. Na kama hatafanya basi, atawarithisha watoto wako uliowazaa. Yaani utazaa vitoto malaya, au vichoyo, au viizi, viuaji na maovu mengine.

Unaweza ukahangaika kumlea mtoto wee, pigia kelele wee! Chapa bakora wee! Lakini nakuhakikishia kama amerithi kwako au kwa mwenza wako utakuwa unajihangaisha tuu.

Kwa wale wanasaikolojia wataungana na mimi hasa waliomsoma mwanasaikolojia Nguli aitwaye Sigmund Freud.
Huyo ameelezea kinagaubaga jambo hili katika nadharia yake "Freudian Psychoanalytic Theory of Personality"

Pia kwa wale wasomaji wa vitabu vya teolojia hasa Biblia wataungana na mimi kuwa Kwenye ishu za Kiroho, Mtoto wa Nyoka ni nyoka siku zote wala hataweza kubadilika.

Na ndio maana Yesu anakuambia, "usifungwe nira na wasio amini" Mungu aliwaambia waisrael wasioane wala kuolewa na mataifa mengine bali wachukuane wao kwa wao.

Huwezi ukazaliana na malaya alafu ukamuomba Mungu watoto wako wasiwe malaya. Huwezi na haiwezi kutokeo.
Huwezi taka kuzaa na mzungu au muarabu alafu ukataka kizazi chako kibaki kuwa cha Kiafrika, ni lazima mtoto atatoka chotara.

Huwezi kufunga ndoa na kuzaa na muuaji alafu ndani ya nyumba ukaomba asiwepo muuaji wakati unafahamu fika kwenye kizazi chako lazima atoke muuaji kwani mama/baba ni muuaji.

Kama unataka watoto warefu, basi chukua mtu mrefu
Kama unataka watoto weupe, chukua mtu mweupe
Lazima kwenye kizazi chako atatako mtoto mweupe iwe watoto au wajukuu.

WITO:
Lazima tuwe makini tunapoenda kuanzisha mahusiano ya kindoa. Tuzingatie mahitaji yetu.
Kama hutaki malaya, basi usioe malaya kwa maana huna uatakachokifanya akabadilika, zaidi sana unaenda kuzalisha malaya zaidi duniani.
Kama hutaki mchoyo basi usioe mwanamke mchoyo.


Utajuaje tabia za mwenzi unayetaka kumuoa, fanya tafiti kwa wazazi wake, ukoo wao, ndani ya miezi sita utajua mbivu na mbichi.

Kumbuka: Tabia hujificha kwenye unconscious mind pale super- ego inapokuwa na nguvu zaidi ya Ego. Kumbuka tabia ya Mtu(Human Behaviour) inajengwa na mambo matatu yaliyopo kwenye fikra(Mind) mambo hayo ni Id, Ego, na Super ego
Id - Instincts (Silika) Hii haibadiliki) Mtu huirithi kutoka kwa wazazi.
Ego - Reality (Uhalisia)
Super-ego _ Morality (Maadili) Hutokana na jamii

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
 
Basi huyo kijana atokaye ktk familia ya kitapeli kuanzia baba hata watoto wote akaondoka kutoka huko kwao kuja kunieleza habari za kunipenda nami nikaitisha kikao ktk halmashauri ya kichwa changu jibu likapatikana kuwa huyu hastahili kwakuwa atafanya utapeli nyumbani mwetu nami siko tayari kutapeliwa. Basi baada ya jibu kijana alirudi kwao huku akininung'unikia kwa kutoshikamana nae ktk safari ya huba!

Tabia ya kurithi ni ngumu sana kumbadili mtu aisee.
 
Japo sio wote mkuu,

Bill graham mhubiri mashuhuri sana marekani , mama yake alikuwa Malaya, alizaliwa nje ya ndoa! Na alikuwa ana kiri hilo, lakini yeye akaja kuwa mhubiri mkubwa sana kuwahi kutokea Duniani,

Alisema usifungwe na hatima yako, historia yako isikuhukumu wala tusihukumu watu kwahistoria yao, wapo waliozaliwa na makahaba, wachawi, majambazi hata wendawazimu lakini watoto wakaja kuwa watu waungwana sana!

Sio kila aliyetokana na familia mbaya nae LAZIMA awe mbaya! kama ingekuwa hivyo basi kusingekuwa na haja ya kuwa na makanisa na misikiti maana tayari aliyezaliwa na m-baya naye pia ni m-baya sasa unamuhubiria yanini?!

Mtoto hata chukua maovu ya baba wala baba hata chukua maovu ya mwana. Haki yake mwenye haki itakuwa juu yake mwenyewe! Na uovu wake mtu mwovu utakuwa juu yake mwenyewe! Usihukumu kirahisi tu!
 
Japo sio wote mkuu,

Bill graham mhubiri mashuhuru sana marekani , mama yake alikuwa Malaya, alizaliwa nje ya ndoa! Na alikuwa ana kiri hilo, lakini yeye akaja kuwa mhubiri mkubwa sana kuwahi kutokea Duniani,

Alisema usifingwe na hatima yako, historian yako isikuhukumu wala tusihukumu watu kwahistoria yao, wapo waliozaliwa na makahaba, wachawi, majambazi hata wendawazimu lakini watoto wakaja kuwa watu waungwana sana!

Sio kila aliyetikana na familia mbaya nae LAZIMA awe mbaya! kama ingekuwa hivyo basi kusingekuwa na haja ya kuwa na makanisa na misikiti maana tayari aliyezaliwa na mbaya naye pia ni mbaya sasa unamuhubiria yanini?!

Mtoto hata chukua maovu ya baba wala baba hata chukua maovu ya mwana. Haki yake mwenye haki itakuwa juu yake mwenyewe! Na uovu wake maovu utakuwa juu yake mwenyewe! Usihukumu kirahisi tu!


Nimelieleza hilo Mkuu.

Unafikiri ni kwa nini dhambi au uvou hauishi licha ya Mungu kuangamiza kizazi chote wakati wa Nuhu?

Ukioa mwanamke ambaye mama yake ni malaya tambua kuwa siku isiyo na jina utalia kilio cha mbuzi meee! Kama hutalizwa na mkeo basi utalizwa na watoto wako wa kuwazaa.

Kuna kitu kwenye saikolojia psychoanalysis ambapo inaeleza kuwa Zipo tabia hujificha kwenye ung'amuzi bwete kutokana na superego(hasa maadili ya kwenye jamii) Mtu unaweza kumuona ni mchungaji mashuhuri lakini kwa ndani kabisa akawa na tabia ya asili ya uovu iliyojificha ambayo hii lazima itarithishwa kwenda kwa watoto. Ndio maana nikakuambia Malaya huzaa malaya, mwizi huzaa mwizi.
Sema wengine huwa tuli, wengine huwa moto
 
Basi huyo kijana atokaye ktk familia ya kitapeli kuanzia baba hata watoto wote akaondoka kutoka huko kwao kuja kunieleza habari za kunipenda nami nikaitisha kikao ktk halmashauri ya kichwa changu jibu likapatikana kuwa huyu hastahili kwakuwa atafanya utapeli nyumbani mwetu nami siko tayari kutapeliwa. Basi baada ya jibu kijana alirudi kwao huku akininung'unikia kwa kutoshikamana nae ktk safari ya huba!

Tabia ya kurithi ni ngumu sana kumbadili mtu aisee.


Unaogopa matapeli eeeh?
 
Nimelieleza hilo Mkuu.

Unafikiri ni kwa nini dhambi au uvou hauishi licha ya Mungu kuangamiza kizazi chote wakati wa Nuhu?

Ukioa mwanamke ambaye mama yake ni malaya tambua kuwa siku isiyo na jina utalia kilio cha mbuzi meee! Kama hutalizwa na mkeo basi utalizwa na watoto wako wa kuwazaa.

Kuna kitu kwenye saikolojia psychoanalysis ambapo inaeleza kuwa Zipo tabia hujificha kwenye ung'amuzi bwete kutokana na superego(hasa maadili ya kwenye jamii) Mtu unaweza kumuona ni mchungaji mashuhuri lakini kwa ndani kabisa akawa na tabia ya asili ya uovu iliyojificha ambayo hii lazima itarithishwa kwenda kwa watoto. Ndio maana nikakuambia Malaya huzaa malaya, mwizi huzaa mwizi.
Sema wengine huwa tuli, wengine huwa moto


Nakuelewa mkuu,,

Na nakubali kuwa tabia huweza kurithishwa maana watoto wanarithi (wanaiga) Yale wanayoyaona kutoka kwa wazazi wao na jamii inayowazunguka!

Lakini kuhusu swali lako kwamba kwanini dhambi haiishi licha yaMungu kuwaangamiza wanadamu kipindi cha Nuhu na Sodoma na Gomorah, ni kwamba dhambi asili yake ni Shetani ndiye aliyeingiza dhambi bustanini eden, hivyo basi Shetani bado hajafa, wala hajazeeka huwezi kumaliza dhambi wakati muasisi wake angalia anatenda kazi mchana na usiku,

Yesu alisema "nyakati zaja tena hamta utumia tena msemo huu, kwamba baba wamekula zabibu mbichi na watoto wao wamepata ganzi la meno!"

"Kwakuwa watoto hawatarithi dhambi ya baba wala wazazi hawatachukua dhambi ya watoto wao, Bali roho ile itendayo dhambi ndio itakayo kufa, kwakuwa mshahara wa dhambi ni mauti"

Kumbuka hata Rahabu alikuwa Kahaba lakini aliokolewa yeye na familia yake na akaja kuwa kwenye ukoo wa kuzaliwa Yesu japo hakuwa Myahudi,

Paulo au Sauli (mtume) alikuwa muuaji kabla, lakini akaja kuwa mtume!

Tukisema dhambi urithiwa basi hakuna atakaye pona mkuu,, maana hakuna mtu ambaye ni mkamilifu asilimia mia au anatokana na familia takatifu, ukichunguza kila familia ina historia Fulani mbaya! Either Mjomba, babu, bibi, baba mdogo, mkubwa au ndugu, either walikuwa wachawi, washirikina, waabudu mizimu, nk

Hebu soma historia ya nyerere uone jinsi mamayake alivyotengwa kwasababu ya kutuhumiwa imani za kishirikina (uchawi) kwasababu alikuwa akizaa watoto wanakufa, sasa mkuu tusemeje?! Kuwa nyerere hasingefaa kuwa Rais kwakuwa eti mama yake aliwahi kutuhumiwa mchawi?! Lakini akaja kuwa Rais Mzuri kuwahi kutokea Afrika!

Mkapa familia yake iliwahi kutuhumiwa kuwa wachawi reference gazeti la msemakweli no: ISSN 0856-5090 Toleo 1194 jumapili August 2-8, 2020.

Sasa tusemeje pia Mkapa hakufaa kuwa Rais kwakuwa familia yake iliwahi kutuhumiwa uchawi na wanakijiji wenzake?! Lakini akaja kuwa msomi Mzuri na Rais Mzuri pia!

Ndio maana nasema sio kila mtu atokaye kwenye familia mbaya au zenye kutuhumiwa vibaya basi lazima awe mbaya! Hapana mkuu!
 
Nakuelewa mkuu,,

Na nakubali kuwa tabia huweza kurithishwa maana watoto wanarithi (wanaiga) Yale wanayoyaona kutoka kwa wazazi wao na jamii inayowazunguka!

Lakini kuhusu swali lako kwamba kwanini dhambi haiishi licha yaMungu kuwaangamiza wanadamu kipindi cha Nuhu na Sodoma na Gomorah, ni kwamba dhambi asili yake ni Shetani ndiye aliyeingiza dhambi bustanini eden, hivyo basi Shetani bado hajafa, wala hajazeeka huwezi kumaliza dhambi wakati muasisi wake angalia anatenda kazi mchana na usiku,

Yesu alisema "nyakati zaja tena hamta kutumia tena msemo huu, kwamba baba wamekuja dhabibu mbichi na watoto wao wamepata ganzi la meno!"

"Kwakuwa watoto hawatarithi dhambi ya baba wala wazazi hawatachukua dhambi ya watoto wao, Bali roho ile itendayo dhambi ndio itakayo kufa, kwakuwa mshahara wa dhambi ni mauti"

Kumbuka hata Rahabu alikuwa Kahaba lakini aliokolewa yeye na familia yake na akaja kuwa kwenye ukoo wa kuzaliwa Yesu japo hakuwa Myahudi,

Paulo au Sauli (mtume) alikuwa muuaji kabla, lakini akaja kuwa mtume!

Tukisema dhambi urithiwa basi hakuna atakaye pona mkuu,, maana hakuna mtu ambaye ni mkamilifu asilimia mia au anatokana na familia takatifu, ukichinguza kila familia inahistoria Fulani mbaya! Either Mjomba, babu, bibi, baba mdogo, mkubwa au ndugu, either waliokuwa wachawi, washirikina, waabudu mizimu, nk

Hebu soma historian ya nyerere uone jinsi mamayake alivyotengwa kwasababu ya kutuhumiwa imani za kishirikina (uchawi), sasa mkuu tusemeje?! Kuwa nyerere hasingefaa kuwa Rais kwakuwa eti mama yake aliwahi kutuhumiwa mchawi?!

Mkapa familia yake iliwahi kutuhumiwa kuwa wachawi reference gazeti la msemakweli no: ISSN 0856-5090 Toleo 1194 jumapili August 2-8, 2020.

Sasa tusemeje pia Mkapa hakufaa kuwa Rais kwakuwa familia yake iliwahi kutuhumiwa uchawi na wanakijiji wenzake?!

Ndio maana nasema sio kila mtu ataokaye kwenye familia mbaya au zenye kutuhumiwa vibaya basi lazima awe mbaya! Hapana mkuu!


Hapa sizungumzii kuokolewa Mkuu, nazungumzia ishu nzima ya familia na kuanzisha kizazi chako.

Wokovu unatokana na kutubu, toba.

Unaweza kuwa mwema lakini dhambi moja ikakufanya usipate wokovu kwa sababu hukutubu
Lakini mwingine anaweza kuwa mdhambi mkubwa lakini akaokolewa kwa sababu alitubu dakika ya mwisho.

Hapa tunazungumzia familia na kizazi.

Huwezi badilisha asili.
 
Hapa sizungumzii kuokolewa Mkuu, nazungumzia ishu nzima ya familia na kuanzisha kizazi chako.

Wokovu unatokana na kutubu, toba.

Unaweza kuwa mwema lakini dhambi moja ikakufanya usipate wokovu kwa sababu hukutubu
Lakini mwingine anaweza kuwa mdhambi mkubwa lakini akaokolewa kwa sababu alitubu dakika ya mwisho.

Hapa tunazungumzia familia na kizazi.

Huwezi badilisha asili.


Nimekuelewa sana,, mkuu

Na sija base sana kwenye mambo ya kuokolewa peke yake mkuu,

Ndio maana nimekupa mfano wa familia ya Nyerere na mkapa pia, hawa hawakuwa walokole wala makasisi lakini walikuwa watu wazuri tu licha ya familia zao (wazazi) kutuhumiwa wachawi!

Ndio maana sikubaliani sana kwamba kila mtu atokaye kwenye familia mbaya lazima moja kwa moja Naye awe mbaya! Nope! Labda tuseme may possibility not probably!
 
Nimekuelewa sana,, mkuu

Na sija base sana kwenye mambo ya kuokolewa peke yake mkuu,

Ndio maana nimekupa mfano wa familia ya Nyerere na mkapa pia, hawa hawakuwa walokole wala makasisi lakini waliokuwa watu wazuri tu licha ya familia zao (wazazi) kutuhumiwa wachawi!

Ndio maana sikubaliani sana kwamba kila mtu atokaye kwenye familia mbaya lazima moja kwa moja Nate awe mbaya! Nope! Labda tusemeje may possibility not probably!


Nani alikuambia kuwa watu hao walikuwa wazuri?

Ogopa watu hawa duniani

1. Waandishi
2. Mafarisayo (watu wote wajifanyao watu wa Mungu)
3. Tekonolojia
 
Nani alikuambia kuwa watu hao walikuwa wazuri?

Ogopa watu hawa duniani

1. Waandishi
2. Mafarisayo (watu wote wajifanyao watu wa Mungu)
3. Tekonolojia


Kwahiyo mkuu,,, waliyofanya Nyerere na Mkapa ni mabaya na Maovu?!
 
Japo sio wote mkuu,

Bill graham mhubiri mashuhuri sana marekani , mama yake alikuwa Malaya, alizaliwa nje ya ndoa! Na alikuwa ana kiri hilo, lakini yeye akaja kuwa mhubiri mkubwa sana kuwahi kutokea Duniani,

Alisema usifungwe na hatima yako, historia yako isikuhukumu wala tusihukumu watu kwahistoria yao, wapo waliozaliwa na makahaba, wachawi, majambazi hata wendawazimu lakini watoto wakaja kuwa watu waungwana sana!

Sio kila aliyetokana na familia mbaya nae LAZIMA awe mbaya! kama ingekuwa hivyo basi kusingekuwa na haja ya kuwa na makanisa na misikiti maana tayari aliyezaliwa na m-baya naye pia ni m-baya sasa unamuhubiria yanini?!

Mtoto hata chukua maovu ya baba wala baba hata chukua maovu ya mwana. Haki yake mwenye haki itakuwa juu yake mwenyewe! Na uovu wake mtu mwovu utakuwa juu yake mwenyewe! Usihukumu kirahisi tu!
Uko sahihi.
 
Kwahiyo mkuu,,, waliyofanya Nyerere na Mkapa ni mabaya na Maovu?!

Mimi sikuwa watu wa karibu yao siwezi kuhitimisha lolote kuhusu wao.
Ila nimeshakuambia ogopa watu hao hapo juu.

Kwenye Historia tafuta kile kilichofichwa kisijulikane na watu, hicho ndio ukweli.
 
Mimi sikuwa watu wa karibu yao siwezi kuhitimisha lolote kuhusu wao.
Ila nimeshakuambia ogopa watu hao hapo juu.

Kwenye Historia tafuta kile kilichofichwa kisijulikane na watu, hicho ndio ukweli.


Ndio maana nikasema sio wote mkuu, wanaozaliwa au kutokea kwenye familia mbaya basi nao ni wabaya, tusi "generalized" isn't fair at all,,,

Uliposema "nani alikwambia hao walikuwa wazuri?!" nikashtuka kidogo!

Mwisho tukubali tu kutokubaliana, nakubaliana na wewe kidogo kuwa kuna asilimia Fulani (uwezekano kiasi) kwamba kwavile watoto huiga (hujifunza tabia) kwayale wanayoyaona kwa wazazi au jamii inayowazunguka basi Mara nyingi huwa rahisi kuiga tabia za wazazi/jamii inayowazunguka!

Lakini pia tukubaliane sio wote wala sio sahihi kusema ni lazima mtu aige/awe na tabia ya wazazi wake au familia yake au jamii inayowazunguka! Itakuwa hatuwatendei haki kabisa, kuna watu wametokana na mama makahaba lakini wao wako very decent, kuna watu wametokana na wazazi walevi lakini wao ni watu safi kabisa, kuna wengine wamezaliwa na wazazi wachawi au washirikina lakini wao hawataki hata kusikia habari za ushirikina au uchawi kadhalika na majambazi na wahuni,

Tabia inaweza kubadilika mkuu, sio ngozi kwamba haivuliki, tusiwahukumu watu wote wanaofanyabidii kuwa watu safi kwenye jamii.
 
Ndio maana nikasema sio wote mkuu, wanaozaliwa au kutokea kwenye familia mbaya basi nao ni wabaya, tusi "generalized" isn't fair at all,,,

Uliposema "nani alikwambia hao walikuwa wazuri?!" nikashtuka kidogo!

Mwisho tukubali tu kutokubaliana, nakubaliana na wewe kidogo kuwa kuna asilimia Fulani (uwezekano kiasi) kwamba kwavile watoto huiga (hujifunza tabia) kwayale wanayoyaona kwa wazazi au jamii inayowazunguka basi Mara nyingi huwa rahisi kuiga tabia za wazazi/jamii inayowazunguka!

Lakini pia tukubaliane sio wote wala sio sahihi kusema ni lazima mtu aige/awe na tabia ya wazazi wake au familia yake au jamii inayowazunguka! Itakuwa hatuwatendei haki kabisa, kuna watu wametokana na mama makahaba lakini wao wako very decent, kuna watu wametokana na wazazi walevi lakini wao ni watu safi kabisa, kuna wengine wamezaliwa na wazazi wachawi au washirikina lakini wao hawataki hata kusikia habari za ushirikina au uchawi kadhalika na majambazi na wahuni,

Tabia inaweza kubadilika mkuu, sio ngozi kwamba haivuliki, tusiwahukumu watu wote wanaofanyabidii kuwa watu safi kwenye jamii.
Usidanganye,tabia ya mtu ni kama ngozi haiwezi badilika kamwe, yan unapo tafuta parsonality ya mtu,tabia ndio determination yake kama huamini oa malaya afu majibu utayapata mwenyewe
 
Usidanganye,tabia ya mtu ni kama ngozi haiwezi badilika kamwe, yan unapo tafuta parsonality ya mtu,tabia ndio determination yake kama huamini oa malaya afu majibu utayapata mwenyewe


Sio kweli mkuu,,, watu wangapi wamebadilika tabia kaka,,,

Kumbuka hata watakatifu hawakuzaliwa wakiwa watakatifu,,,

Watakatifu ni wenye dhambi walio tubu!
 
Back
Top Bottom