CreativityCode
Senior Member
- Aug 8, 2020
- 158
- 653
Ni ukweli usiopingika kizazi cha viongozi wa kidunia na marais wa nchi kubwa duniani kimebadilika sana.
Tukianza na Katibu Mkuu wa UN ni kama amepoa sana na taasisi yake imekosa mashiko.
Tukija kwa Taifa la Marekani nalo sera zake za nje zimekosa meno kabisa kutokana na Rais wao Trump kuangalia zaidi mambo yake ya ndani kuliko ya nchi nyingine za dunia. Afrika ndiyo imeachwa kabisa ijiendee yenyewe.
Hali imekuwa tofauti kabisa na kizazi cha uongozi cha akina Obama, Ban Ki-Moon, Tony Blair ama Gordon Brown. Kizazi hiki cha viongozi wa dunia kilikuwa ni moto wa kuotea mbali kwani hakikumvumilia kiongozi yeyote duniani aliyekuwa na chembechembe za udikteta na kunyima watu haki ya kuishi na uhuru wa kujieleza.
Nawaambia ukweli kabisa Obama angekuwa madarakani Tanzania tungezungumza mengine.
Pia ashukuru sana coronavirus kwani imewafanya viongozi wa kidunia kushughulikia mambo yao zaidi kuliko ya nchi nyingine na ni nadra sana na wala tusitegemee kuona waangalizi wa uchaguzi kuja Tanzania hivyo huyu bwana na tume yake wanaweza kufanya lolote lile kuhakikisha wanakuwa madarakani.
Pengine tuishukuru teknolojia ya mawasiliano maana dunia inaweza kufuatilia chochote kile watakachokuwa wanakifanya hasa kwenye kujumlisha kura labda wasitumie computer maana zinaweka na kutuma records kwa mabeberu hivyo wataona kila gumashi litakalokuwa linafanywa.
SIKU NJEMA
Tukianza na Katibu Mkuu wa UN ni kama amepoa sana na taasisi yake imekosa mashiko.
Tukija kwa Taifa la Marekani nalo sera zake za nje zimekosa meno kabisa kutokana na Rais wao Trump kuangalia zaidi mambo yake ya ndani kuliko ya nchi nyingine za dunia. Afrika ndiyo imeachwa kabisa ijiendee yenyewe.
Hali imekuwa tofauti kabisa na kizazi cha uongozi cha akina Obama, Ban Ki-Moon, Tony Blair ama Gordon Brown. Kizazi hiki cha viongozi wa dunia kilikuwa ni moto wa kuotea mbali kwani hakikumvumilia kiongozi yeyote duniani aliyekuwa na chembechembe za udikteta na kunyima watu haki ya kuishi na uhuru wa kujieleza.
Nawaambia ukweli kabisa Obama angekuwa madarakani Tanzania tungezungumza mengine.
Pia ashukuru sana coronavirus kwani imewafanya viongozi wa kidunia kushughulikia mambo yao zaidi kuliko ya nchi nyingine na ni nadra sana na wala tusitegemee kuona waangalizi wa uchaguzi kuja Tanzania hivyo huyu bwana na tume yake wanaweza kufanya lolote lile kuhakikisha wanakuwa madarakani.
Pengine tuishukuru teknolojia ya mawasiliano maana dunia inaweza kufuatilia chochote kile watakachokuwa wanakifanya hasa kwenye kujumlisha kura labda wasitumie computer maana zinaweka na kutuma records kwa mabeberu hivyo wataona kila gumashi litakalokuwa linafanywa.
SIKU NJEMA