Asanteni sana Kigoma-Dr Slaa.

Asanteni sana Kigoma-Dr Slaa.

Umoja Ndio fahari yetu, Undugu ndio Nguvu, Chuki na Ukabila hatuvitaki hata kamwe, Lazima tuungane,Tuijenge Nchi yetu, Asiwe hata mmoja,Anayetenganisha,Tunaishi na Tumaini. Nategemea Daima Tanzania, Hekima yetu ni Siasa iliyo safi Daima mimi Mtanzania Mwananchi Mzalendo, Kwa huzuni na Mateso Chadema wameteswa, Hawakushtushwa na risasi hawakushtushwa na Mijeledi, Nia yao Ukombozi. Chadema Daima.

Haya maneno ni mazuri, yanastahili kuwa utangulizi sijui kitabu gani cha cdm? Dr. Slaa is ready for the presidency. Tutoe support yetu yote kuhakikisha lengo ili linatimia.
 
kila siku nawaambia ccm kwamba,hila zao wanazozifanya ndio zinaipaisha chadema hawanisikii,lakini kwa kuwa ccm ni sikio la kufa hawaelewi ninalowaambia, nawaambia tena kadri watakavyofanya kuingilia mgogoro wa zito na chadema ndivyo watakavyoipaisha chadema

Wamechemsha sana mkuu!
 
Haya maneno ni mazuri, yanastahili kuwa utangulizi sijui kitabu gani cha cdm? Dr. Slaa is ready for the presidency. Tutoe support yetu yote kuhakikisha lengo ili linatimia.

Maneno kama haya ni wazi yanampa Faraja kubwa Simba wa Tanzania Dr Slaa.
 
Mimi nimefurahi sana moyoni mwangu. Mungu utubariki kama RSA. Freedom is coming tomorrow. Hata kule Africa Kusini kuna watu weusi waliokuwa wakimbeza Mandela.
 
hongera sana dr slaa mimi kweli nimefurai kwa ziara yake imeonyesha kwa walichokiamua kamati kuu pengine kilikuwa sahihi, lakini pia napongeza sna slaa kwa kelele adia slizopiga kwe nye nchi hii kweli zimesaidia
 
Jamani tuache utani Dr.Slaa anaweza, binafsi namkubali na pia nampongeza kwa ujasiri alio nao, hakika watanzania wengi tupo nyuma yake, kama wana jf walivyokwisha sema anatawala mioyoni mwetu, Mola amlinde, amtie nguvu hekima na busara katika harakati za kuikomboa Taifa letu.
 
Ili kuifikia Tanzania tunayoitaka tunahitaji chama makini na viongozi makini kama akina Dr.Slaa, hongera kwa kumaliza salama ziara ya Kigoma.
 
Ninauakika Dr. Slaa akirudi Kasulu waliompiga mawe atawasamehe, lakini pia atapokelewa zaidi ya mara nne ya umati uliokuwepo wakati ule. In fact nashauri cdm immpe ruhusa kurudi maeneo hayo si muda mlefu kuanzia sasa.
 
DR SLAA GWIJI LA SIASA na TEGEMEO HALISI LA WATANZANIA , MUNGU AKULINDE BABA .
 
Mimi nimefurahi sana moyoni mwangu. Mungu utubariki kama RSA. Freedom is coming tomorrow. Hata kule Africa Kusini kuna watu weusi waliokuwa wakimbeza Mandela.

nakupongeza sana mkuu , bila kung'ata ulimi DR SLAA NI MFANO HALISI WA MANDELA .
 
Molemo anajitahidi sana kumlisha maneno Dr Slaa. Hakika ziara yake imetonesha majeraha ya wana kigoma kutokana na mipango ovu dhidi ya kijana wao

Unataka kutuaminisha kwamba watu wa Kigoma wanataka wanasiasa waongo,wazushi,wanafiki na wabinafsi?maana leo AG ameliambia bunge ya kwamba Zitto alikiri mbele ya kamati kwamba hana majina wala account za walioficha fedha Uswis,sasa majreha yaliyotoneshwa ni kwa kipi? Maana kama wanakigoma walidhani kijana wao ni meadilifu basi hakuna kitu,na ndio maana CC ilimvua nyadhifa zake zote .
 
Gwiji wa Siasa Tanzania na Katibu Mkuu CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amefurahishwa na ukarimu wa watu wa Kigoma tangia aanze ziara ya kichama mkoani humo.

Akizungumza katika Baraza la Uongozi la Mkoa wa Kigoma kiongozi huyo wa kisiasa nchini alisema watu wa Kigoma wameonyesha mshikamano mkubwa na kupambana na wahuni wote waliokuwa wameagizwa kuvuruga ziara yake.

Kauli hiyo ya Dr Slaa inafuatia wahuni na wavuta bangi kujaribu kuvuruga mikutano yake lakini nguvu ya UMMA ilidhibiti hujuma hizo.

Wiki iliyopita watu walionyweshwa gongo na wengine walevi wa bangi waliandamana Kigoma mjini kulaani ujio wa Dr Slaa na kujiapiza endapo kama kiongozi huyo angekanyaga Kigoma mjini wangemdhuru.

Hata hivyo Dr Slaa aliingia Kigoma mjini kwa Kishindo kikubwa na kulakiwa na msururu wa magari na Pikipiki huku umati ukijipanga kandokando ya barabara na kupeperusha majani ya miti.

Kutokana na ujasiri wa Dr Slaa kupuuza vitisho vya wahuni hao baadhi ya watu wa Kigoma wamempachika jina la SIMBA WA TANZANIA.
Simba wa Tanzania! Labda wa kukausha au wa kuchora?!
 
Jamani tuache utani Dr.Slaa anaweza, binafsi namkubali na pia nampongeza kwa ujasiri alio nao, hakika watanzania wengi tupo nyuma yake, kama wana jf walivyokwisha sema anatawala mioyoni mwetu, Mola amlinde, amtie nguvu hekima na busara katika harakati za kuikomboa Taifa letu.

Maneno yako na yapate kibali machoni mwa Mungu!
 
Hata mimi nimewasifu watu wa Kigoma, Nasema asanteni sana. Kuweni makini mtaujua ukweli wa mambo.
 
Back
Top Bottom