Mahakama siyo Chombo cha uadui, ni Chombo cha kudai haki
Ni matumaini yangu Viongozi wa Chadema watakuwa Wakomavu kisiasa na hivyo kuendlkea kufanya kazi na Zitto iwapo atashinda rufani yake katika baraza kuu
Na pia ni matumaini yangu Zitto atafanya kazi na viongozi wa Chadema bila kinyongo iwapo atashinda rufani yake katika baraza kuu.
Chadema itabidi iunde tume ya maridhiano na kusameheana ili "yaliyopita si ndwele tugange yajayo".
Pamoja na Uchambuzi mzuri wa Ndimara Tegambwage, ILA AMESAHAU OPTION MOJA AMBAYO NI "KUSAMEHEANA" KWA PANDE ZOTE MBILI BAADA YA SINTOFAHAMU NA KUKURUKAKARA ZOTE KUTOKEA.
MIMI NINASEMA INAWEZEKANA KWA PANDE ZOTE MBILI KUSAMEHEANA, KAMA MANDELA ALIWASAMEHE MAKABURU, ZITTO ATASHINDWAJE KUWASAMEHE WANAOMPIKIA JUNGU?
AU MBOWE ATASHINDWAJE KUMSAMEHE ZITTO KWA YALE ALIYOMKWAZA NAYO?.
Hoja ya Zitto kutokutakiwa Chadema ni hoja ya Kijinga, Kama Chadema ni kambi ya Mbowe basi Kweli hatakiwi, Lakini kama Chadema ni Ya WanaChadema kutoka nchi nzima basi Zitto anatikiwa, na Baraza Kuu ndiyo Chombo kitakachohitimisha hili