Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 49,325
- 152,136
Nashukuru Askofu Mokiwa kwa kuanika unafiki wa sisi waumini tunaojidai kuguswa sana na imani zetu wakati ni wanafiki.
Nilileta mada inayofanana na anayoyasema Baba Askofu watu hapa wakanishambulia kwa kujifanya eti wamechukizwa sana na nilichokisema juu ya imani zao.
Ni ajabu sana tunaguswa na imani zetu kuliko matendo yetu.Naendelea kusisitiza ni bora wapagani kuliko sisi wenye dini tulioja unafiki wa kupitiliza mbele ya macho ya mwenyezi mungu.
Makonda nae kaja na yake!
Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa
Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa, ametaja majipu 10 yaliyoko makanisani na kuwataka Watanzania kujisafisha kwa kuacha mambo yasiyompendeza Mungu, ikiwamo migogoro ndani ya makanisa.
Askofu Mokiwa amesema ndani ya makanisa kuna mawe makubwa aliyoyafananisha na majipu ambayo hata Yesu Kristo anasononeshwa nayo.
Hayo aliyasema jana katika ibada ya Pasaka iliyoadhimishwa kitaifa katika Kanisa la Mtakatifu Albano, Upanga jijini Dar es Salaam.
Askofu Mokiwa alitaja jipu la kwanza kuwa ni uwapo wa mashindano makanisani, huku akisema siku hizi makanisa yanashindana kwa kuangalia kanisa lipi kubwa kuliko lingine na kanisa linamiliki shule ngapi.
Alisema: "Ushindani wa kanisa gani ni kubwa kuliko lingine, kanisa gani lina mali kuliko lingine, askofu anayeongoza kanisa fulani ni kabila fulani, na kanisa gani lina waumini wengi kuliko lingine na kanisa gani lina vituo vingi vya kulelea watoto yatima kuliko lingine.
“Imefika wakati sasa makanisa yajitathmini na kuanza kupunguza kuzungumza mambo ya nje ya kijamii na badala yake waelekezane uovu unaopatikana ndani ya makanisa,” alisema.
Jipu lingine alilitaja kuwa ni maaskofu kupigana vita. Alisema kuna tabia ya askofu mmoja kumchimba askofu mwingine, kupanga mapinduzi dhidi ya askofu mwenzake, pamoja kutukanana.
Alisema kuna tabia ya askofu kuacha eneo lake na kuingia katika eneo la askofu mwingine na kusababisha misuguano.
Jipu lingine alisema ni mapinduzi ndani ya makanisa, kuwa kuna ugumu wa moyo na kusalimiana kwa badhi ya waumini wa makanisa na kwamba waumini siku hizi wanasemana na kusingiziana, hivyo kumekuwapo kwa uongo ndani ya taasisi hizo ambazo dhima yake ni kuleta amani na furaha miongoni mwa waumuni.
Askofu Mokiwa alitaja tatizo lingine kuwa ni chuki baina ya waumini, huku watu wakiwa hawasalimiani na hawapendani, jambo ambalo hata askofu anapojaribu kuwaita na kuwapatanisha, wanakimbia kwa kutoa udhuru.
Alisema jipu lingine ni uwapo wa nguvu ya pesa kanisani au nguvu ya mtu ndani ya kanisa, ambayo inasababisha kuvurugika kwa kanisa.
Askofu Mokiwa alisema: "Kuna watu makanisani wanatumia pesa kwa manufaa yao wenyewe. Mbona hujitolei kusaidia watoto yatima? Mbona hujitolei kuwasaidi kikundi cha uinjilisti kwenda kuhubiri? Watu wa namna hiyo wana lengo la kuvunja amani."
Alitaja jipu lingine kuwa ni wizi na ulaghai na kwamba katika makanisa kuna ulaghai uliokithiri.
Jipu lingine alisema kuwa ni uwapo wa roho ya uchochezi kwa baadhi ya waumini makanisani, huku pia akitaja uwapo wa injili za kibiashara kwa baadhi ya makanisa kutumia injili kujiingizia kipato kwa kufanya miujiza.
Askofu Mokiwa alisema jipu lingine ni uwapo wa wivu na uzushi ndani ya makanisa.
“Siku hizi hayo mambo yanaitwa majipu ambayo yanasababisha kanisa kushindwa kuendelea, wakristo wanashindwa kumwona Mungu kwa sababu kuna watu waliotofauti ndani ya makanisa,” alisema Mokiwa.
MAKONDA: ATAKAYEOMBA ULINZI KANISANI KUSWEKWA NDANI
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika ibada hiyo aliliomba kanisa kumsaidia kutimiza wajibu wake kwa kunyoosha mienendo ya waumini wake, huku akitumia nafasi hiyo kusisitiza agizo lake la kuwataka wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhakiki silaha zao ndani ya siku 90.
“Kuanzia Julai Mosi, mwaka huu mimi mwenyewe nitaongoza msako wa kukagua silaha ambazo hazijahakikiwa. Sitakuwa na huruma, wala sitamwangalia mtu usoni,” alisema Makonda.
Makonda alisema kwa sasa jiji la Dar es Salaam haliko salama kutokana uwapo wa silaha ambazo hazieleweki.
Aliwaomba waumini wa Kikristo, ambao jana walikuwa wanaadhimisha Sikukuu ya Pasaka, kujitolea kuchangia maendeleo ya mkoa ikiwa ni pamoja na kumaliza tatizo la madawati.
“Juzi kuna mama mmoja Kimara, ni kiongozi wa kanisa, anasema kuna shughuli kanisani, anaomba ulinzi. Nikamuuliza wa nini, akasema unajua huku kuna rushwa. Nikashangaa kusikia eti kanisani napo kuna rushwa, hadi leo siamini. Sasa nasema yeyote atakayepiga simu kuomba ulinzi wa polisi kanisani namweka ndani,” alisema Makonda.
CHANZO: NIPASHE
Nilileta mada inayofanana na anayoyasema Baba Askofu watu hapa wakanishambulia kwa kujifanya eti wamechukizwa sana na nilichokisema juu ya imani zao.
Ni ajabu sana tunaguswa na imani zetu kuliko matendo yetu.Naendelea kusisitiza ni bora wapagani kuliko sisi wenye dini tulioja unafiki wa kupitiliza mbele ya macho ya mwenyezi mungu.
Makonda nae kaja na yake!

Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa
Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa, ametaja majipu 10 yaliyoko makanisani na kuwataka Watanzania kujisafisha kwa kuacha mambo yasiyompendeza Mungu, ikiwamo migogoro ndani ya makanisa.
Askofu Mokiwa amesema ndani ya makanisa kuna mawe makubwa aliyoyafananisha na majipu ambayo hata Yesu Kristo anasononeshwa nayo.
Hayo aliyasema jana katika ibada ya Pasaka iliyoadhimishwa kitaifa katika Kanisa la Mtakatifu Albano, Upanga jijini Dar es Salaam.
Askofu Mokiwa alitaja jipu la kwanza kuwa ni uwapo wa mashindano makanisani, huku akisema siku hizi makanisa yanashindana kwa kuangalia kanisa lipi kubwa kuliko lingine na kanisa linamiliki shule ngapi.
Alisema: "Ushindani wa kanisa gani ni kubwa kuliko lingine, kanisa gani lina mali kuliko lingine, askofu anayeongoza kanisa fulani ni kabila fulani, na kanisa gani lina waumini wengi kuliko lingine na kanisa gani lina vituo vingi vya kulelea watoto yatima kuliko lingine.
“Imefika wakati sasa makanisa yajitathmini na kuanza kupunguza kuzungumza mambo ya nje ya kijamii na badala yake waelekezane uovu unaopatikana ndani ya makanisa,” alisema.
Jipu lingine alilitaja kuwa ni maaskofu kupigana vita. Alisema kuna tabia ya askofu mmoja kumchimba askofu mwingine, kupanga mapinduzi dhidi ya askofu mwenzake, pamoja kutukanana.
Alisema kuna tabia ya askofu kuacha eneo lake na kuingia katika eneo la askofu mwingine na kusababisha misuguano.
Jipu lingine alisema ni mapinduzi ndani ya makanisa, kuwa kuna ugumu wa moyo na kusalimiana kwa badhi ya waumini wa makanisa na kwamba waumini siku hizi wanasemana na kusingiziana, hivyo kumekuwapo kwa uongo ndani ya taasisi hizo ambazo dhima yake ni kuleta amani na furaha miongoni mwa waumuni.
Askofu Mokiwa alitaja tatizo lingine kuwa ni chuki baina ya waumini, huku watu wakiwa hawasalimiani na hawapendani, jambo ambalo hata askofu anapojaribu kuwaita na kuwapatanisha, wanakimbia kwa kutoa udhuru.
Alisema jipu lingine ni uwapo wa nguvu ya pesa kanisani au nguvu ya mtu ndani ya kanisa, ambayo inasababisha kuvurugika kwa kanisa.
Askofu Mokiwa alisema: "Kuna watu makanisani wanatumia pesa kwa manufaa yao wenyewe. Mbona hujitolei kusaidia watoto yatima? Mbona hujitolei kuwasaidi kikundi cha uinjilisti kwenda kuhubiri? Watu wa namna hiyo wana lengo la kuvunja amani."
Alitaja jipu lingine kuwa ni wizi na ulaghai na kwamba katika makanisa kuna ulaghai uliokithiri.
Jipu lingine alisema kuwa ni uwapo wa roho ya uchochezi kwa baadhi ya waumini makanisani, huku pia akitaja uwapo wa injili za kibiashara kwa baadhi ya makanisa kutumia injili kujiingizia kipato kwa kufanya miujiza.
Askofu Mokiwa alisema jipu lingine ni uwapo wa wivu na uzushi ndani ya makanisa.
“Siku hizi hayo mambo yanaitwa majipu ambayo yanasababisha kanisa kushindwa kuendelea, wakristo wanashindwa kumwona Mungu kwa sababu kuna watu waliotofauti ndani ya makanisa,” alisema Mokiwa.
MAKONDA: ATAKAYEOMBA ULINZI KANISANI KUSWEKWA NDANI
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika ibada hiyo aliliomba kanisa kumsaidia kutimiza wajibu wake kwa kunyoosha mienendo ya waumini wake, huku akitumia nafasi hiyo kusisitiza agizo lake la kuwataka wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhakiki silaha zao ndani ya siku 90.
“Kuanzia Julai Mosi, mwaka huu mimi mwenyewe nitaongoza msako wa kukagua silaha ambazo hazijahakikiwa. Sitakuwa na huruma, wala sitamwangalia mtu usoni,” alisema Makonda.
Makonda alisema kwa sasa jiji la Dar es Salaam haliko salama kutokana uwapo wa silaha ambazo hazieleweki.
Aliwaomba waumini wa Kikristo, ambao jana walikuwa wanaadhimisha Sikukuu ya Pasaka, kujitolea kuchangia maendeleo ya mkoa ikiwa ni pamoja na kumaliza tatizo la madawati.
“Juzi kuna mama mmoja Kimara, ni kiongozi wa kanisa, anasema kuna shughuli kanisani, anaomba ulinzi. Nikamuuliza wa nini, akasema unajua huku kuna rushwa. Nikashangaa kusikia eti kanisani napo kuna rushwa, hadi leo siamini. Sasa nasema yeyote atakayepiga simu kuomba ulinzi wa polisi kanisani namweka ndani,” alisema Makonda.
CHANZO: NIPASHE