more88
JF-Expert Member
- Apr 9, 2016
- 447
- 412
Kama kichwa kinavyojieleza, leo hii katika kata ya Sakina Arusha tumeona wafanya biashara wadogo wenye mitaji ambayo wengi wao ni kuanzia laki 5 hadi milion 2 wakifungiwa biashara zao na maafisa waliojitambulisha kuwa wanatokea Manispaa ya Arusha
Kuna baadhi walipewa vitambulisho vipya vya wajasiriamali vile vya elfu 20 lakini cha ajabu maafisa hao wamevikataa na kuwataka wakakate leseni ya biashara. nakumbuka Rais Magufuli amekuwa akisisitiza vitambulisho vitagawiwa kwa wafanya biashara ambao mitaji yao ni chini ya MILION 4 (NNE) sasa kwa nn hawa maafisa wa manispaa wanapingana na kauli ya RAIS
Kwa sasa hata sisi wafanyakazi tunaona hali ilivyo mbaya kibiashara huku mtaani, kwa nini wasingesubiri hata hili janga la korona lipite maana limeathiri biashara nyingi sana na kufa kwa mitaji? Badala yake wanakuja kufunga viduka vidogo huku mitaani hadi watu leo tumekosa huduma, maana hata dawa tumeshindwa kununua
Ombi langu ni kwamba tunaomba maafisa biashara wazingatie maelekezo aliyotoa rais kuhusu wajasiriamali wadogo pasipo kuwaonea na kuwawekea makufuli katika biashara zao, na je ni sahihi kumfungia mtu biashara bila kumpa elimu na muda wa kwenda kulipa?
Kuna harufu ya rushwa katika hili zoezi tunaomba mamlaka husika ziingilie kati kuzuia wananchi kuonewa.
Kuna baadhi walipewa vitambulisho vipya vya wajasiriamali vile vya elfu 20 lakini cha ajabu maafisa hao wamevikataa na kuwataka wakakate leseni ya biashara. nakumbuka Rais Magufuli amekuwa akisisitiza vitambulisho vitagawiwa kwa wafanya biashara ambao mitaji yao ni chini ya MILION 4 (NNE) sasa kwa nn hawa maafisa wa manispaa wanapingana na kauli ya RAIS
Kwa sasa hata sisi wafanyakazi tunaona hali ilivyo mbaya kibiashara huku mtaani, kwa nini wasingesubiri hata hili janga la korona lipite maana limeathiri biashara nyingi sana na kufa kwa mitaji? Badala yake wanakuja kufunga viduka vidogo huku mitaani hadi watu leo tumekosa huduma, maana hata dawa tumeshindwa kununua
Ombi langu ni kwamba tunaomba maafisa biashara wazingatie maelekezo aliyotoa rais kuhusu wajasiriamali wadogo pasipo kuwaonea na kuwawekea makufuli katika biashara zao, na je ni sahihi kumfungia mtu biashara bila kumpa elimu na muda wa kwenda kulipa?
Kuna harufu ya rushwa katika hili zoezi tunaomba mamlaka husika ziingilie kati kuzuia wananchi kuonewa.