Kukubali kuielewa na kuikubali historia ya arusha kutaifanya ccm pia kukubalika arusha,japo kwa taratibu mno,Mbunge wa mwisho wa halali kutoka ccm hapo arusha alikuwa ni Kanali kinana,tokea hapo ccm haikuwahi kuwa na mbunge aliyechaguliwa kihalali arusha,anguko la ccm arusha halikuanza awamu hii ya chadema kama ma whistle blower wao wanavyodhani,wala wana arusha si tu waumini wa chadema kama inavyofikirika,bali ni wapenda mabadiliko,mabomu ya machozi na risasi za moto hazijaanza wala kuletwa na chadema,mabomu yalipigwa kwenye mkutano wa Augustine mrema akiwa nccr,yalipigwa akiwa Tlp,mabomu na risasi vilirindima kipindi cha uchaguzi uliompa mh Malla ubunge ulioporwa baaadaye na ccm,Mh lema alipogombea kupitia Tlp pia mabomu yalihusika,naweza sema nimeyajua mabomu kabla y kuijua Chadema,Nikiwa kijana mdogo 18- nilipewa dili na ccm la kuwakusanya vijana wakamata nyoka,ili kwenda kuvuruga mikutano ya mrema(Augustine)walichokifanya vijana wale ni kudondosha nyoka katikati ya mkutano na kisha kupiga kelele kuwashtua watu ili wasi concentrate na mkutano,Arusha haikuwahi kurudi nyuma kwenye field ya mabadiliko,Tatizo la ccm ni kujilazimisha na kulazimisha dunia iamini kwamba Chadema ndiyo tatizo,they are in the wrong track,wakitaka kweli kulielewa tatizo la arusha wasifupishe upeo,waangalie mbali zaidi ya miaka kumi iliyopita,na wataona michirizi ya tatizo ilipotokea,na huko wanaweza kulibaini tatizo,tena ndani yao wenyewe.