Arusha: TCRA kuwabana mafundi simu wasiosajiliwa

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,815
4,563
1580363932244.png


MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Kaskazini imetangaza kibano kwa mafundi wa vifaa vya kielektroniki zikiwamo simu za mkononi kwamba wale wasiosajiliwa hawataruhusiwa kufanya kazi hiyo.

TCRA imesema kibano hicho kitaanza Julai, mwaka huu, na kwamba hakuna fundi ambaye atafanya kazi kama hajasomea wala kusajiliwa hivyo ni muhimu kujiunga kwenye kikundi ili kupatiwa elimu.

Mwanasheria wa TCRA, Kant Mosha, alisema hayo juzi katika mkutano wa mafundi wa vifaa vya kielektroniki uliofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha.

Mushi aliwataka mafundi hao kuwa na usajili wa kikundi na hilo ndilo suluhisho.

Alisema mafundi simu ni kada ambayo ilikuwa imesahauliwa lakini kuanzia sasa, serikali imeamua kuwatambua, hivyo kuungana ni sehemu ya kufanikiwa kwa malengo yao.

Mwenyekiti wa Chama cha Mafundi Simu Kanda ya Ziwa, Maguwa Manyanda, aliwataka kutambua kwamba mafundi simu ni wa thamani kwa kuwa jamii inawategemea na wanachangia mapato ya serikali.

Kutokana na hali hiyo, alisema ni muhimu kuona umoja ndio suluhisho la changamoto zao.

Alisema mafunzo hayo yataondoa changamoto na kuwafanya kuwa huru katika shughuli zao za kila siku, hivyo umoja ni nguzo ya kuwafikisha kushirikiana na serikali katika masuala mbalimbali vikiwamo vyombo vya dola.

Manyanda alisema ili kila moja atende kazi zake ni muhimu akajiunga na umoja ili kuondoa changamoto zao ambazo zimekuwa
zikiwafanya kukumbana na misukosuko kutoka polisi.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Mafundi Simu Kanda ya Kaskazini, Nasri Mtengeti, alisema wamefurahi kupata elimu hiyo ya umoja ambayo itawasaidia kuondokana na changamoto mbalimbali.

Awali, akitoa mafunzo kwenye mkutano huo, Mratibu wa Vikundi hivyo kutoka TCRA, Mhandisi Kadaya Buluhye, aliwataka mafundi hao kufanya kazi kwenye umoja kwa lengo la kupata elimu na usajili.

Alisema Jeshi la Polisi linafanya kazi ya kulinda usalama na mali za raia, lakini umoja wao utasaidia kufanya kazi kwa karibu na jeshi hilo na kuondoa changamoto ambazo wamekuwa wakikumbana nazo kama mafundi.

IPP Media
 
Mtu kajiajiri anatengeneza simu miaka kadhaa sasa leo hii unamuambia umpe mafunzo, mafunzo gani ? Kinacho tafutwa hapa ni ku wa identify ili wawe wanalipa kodi, ambapo ni wazo zuri kwa maendeleo ya taifa
 
Sijui kama ninaelewa andiko hili. TCRA wanataka mafundi simu wawe wale waliosomea ufundi huo au wawe waliojiunga kwenye vikundi? Sijaona matakwa ya kusomo yakianishwa ni kisomo cha aina gani; "artisan, technician au digree"?. Kwa nini sharti la kuwa kwenye kikundi? Kwani mtu mwenye ujuzi wake akianzisha karakana akaajiri watu kwa nini alazimishwe kuwa ndani ya kikundi?
 
Wale wamachinga Mlipa vitambulisho bila kusoma! Tena mkawaruhusu wauze mbele ya maduka yetu;
Leo hawa mafundi waliosoma mnataka muwafundishe nyie ambao hamjui hata kubadili mic!
Yaani fundi akafundishwe na asiyekuwa fundi! Halafu apewe cheti asajiliwe kwenye kikundi!
Nani atakayekuwa na dhamana ya kikundi?
Nani atakayelipa kodi ya kikundi?
Kwanini kikundi?

Kwanini msiwape vitambulisho maalum kama vya wamachinga?
Ukiwabana mafundi simu, Automatically SIYE WATEJA WATATUPANDISHIA BEI YA MATENGENEZO KWA KISINGIZO CHA KULIPIA LESENI ZAO!
 
Hapa tunasomeshwa namba mpaka za kiarabu sasa kwa kuwa za kiingereza na za kirumi zilishaisha
 
Mtu kajiajiri anatengeneza simu miaka kadhaa sasa leo hii unamuambia umpe mafunzo, mafunzo gani ? Kinacho tafutwa hapa ni ku wa identify ili wawe wanalipa kodi, ambapo ni wazo zuri kwa maendeleo ya taifa
Kama ni kwa ajili ya kuwatambua ili waanze kulipa kodi ni jambo jema maana ni kwa ajili ya maendeleo ya Taifa kwa ujumla

Ila siyo kuanza kuwafungia eti kisa hawana elimu wakati ufundi ndio elimu yenyewe

Watafutiwe utaratibu maalum kama huo wa kuwapatia leseni bila kuangalia kigezo cha elimu.
Ila uwezo wa kutengeneza ndio kiwe kigezo hiii itasaidia watu wengi kujitokeza na kuchukua leseni hizo endapo watafanya kigezo kiwe elimu basi tutarjie simu kuanza kutengenezwa vyumbani mwao na lengo la serikali kukusanya mapato lisifikiwe kwa asilimia 100 badala yake tukatengeneza mianya ya rushwa kwa wa husika na baadhi ya watendaji wanao simamia sheria

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pesa zinatafutwa Aiseee. Eti kusoma.


MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Kaskazini imetangaza kibano kwa mafundi wa vifaa vya kielektroniki zikiwamo simu za mkononi kwamba wale wasiosajiliwa hawataruhusiwa kufanya kazi hiyo.

TCRA imesema kibano hicho kitaanza Julai, mwaka huu, na kwamba hakuna fundi ambaye atafanya kazi kama hajasomea wala kusajiliwa hivyo ni muhimu kujiunga kwenye kikundi ili kupatiwa elimu.

Mwanasheria wa TCRA, Kant Mosha, alisema hayo juzi katika mkutano wa mafundi wa vifaa vya kielektroniki uliofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha.

Mushi aliwataka mafundi hao kuwa na usajili wa kikundi na hilo ndilo suluhisho.

Alisema mafundi simu ni kada ambayo ilikuwa imesahauliwa lakini kuanzia sasa, serikali imeamua kuwatambua, hivyo kuungana ni sehemu ya kufanikiwa kwa malengo yao.

Mwenyekiti wa Chama cha Mafundi Simu Kanda ya Ziwa, Maguwa Manyanda, aliwataka kutambua kwamba mafundi simu ni wa thamani kwa kuwa jamii inawategemea na wanachangia mapato ya serikali.

Kutokana na hali hiyo, alisema ni muhimu kuona umoja ndio suluhisho la changamoto zao.

Alisema mafunzo hayo yataondoa changamoto na kuwafanya kuwa huru katika shughuli zao za kila siku, hivyo umoja ni nguzo ya kuwafikisha kushirikiana na serikali katika masuala mbalimbali vikiwamo vyombo vya dola.

Manyanda alisema ili kila moja atende kazi zake ni muhimu akajiunga na umoja ili kuondoa changamoto zao ambazo zimekuwa
zikiwafanya kukumbana na misukosuko kutoka polisi.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Mafundi Simu Kanda ya Kaskazini, Nasri Mtengeti, alisema wamefurahi kupata elimu hiyo ya umoja ambayo itawasaidia kuondokana na changamoto mbalimbali.

Awali, akitoa mafunzo kwenye mkutano huo, Mratibu wa Vikundi hivyo kutoka TCRA, Mhandisi Kadaya Buluhye, aliwataka mafundi hao kufanya kazi kwenye umoja kwa lengo la kupata elimu na usajili.

Alisema Jeshi la Polisi linafanya kazi ya kulinda usalama na mali za raia, lakini umoja wao utasaidia kufanya kazi kwa karibu na jeshi hilo na kuondoa changamoto ambazo wamekuwa wakikumbana nazo kama mafundi.

IPP Media

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yes wajulikane wachangie Taifa mbona sawa tu, ni nani anayefanya kazi na halipii kodi, wakat pesa anapata za kutosha tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom