ARUSHA: Mwisho wa kutembea saa nne Usiku

ARUSHA: Mwisho wa kutembea saa nne Usiku

Nataman hiyo marufuku itolewe hapa dar nione utekelezaji wake. Hata waseme saa6 mwisho!! Wataambulia patupu. Saa nne ndio watu tunakoga ili tutoke et nikalale!!!
 
Nadhani kwa mwendo huu siku za karibu watu wataanza kuwekwa kizuizini hasa viongozi wa uponzani.
 
Ujue hiyo ndio itakuwa kwa nchi nzima.

Uamuzi huu una athari mbaya sana kwa CCM na serikali yake.
Mimi nikiwaambia CCM kuwa hawana akili ila hawataki kuamini.
Waache waboronge, Msekwa alipohojiwa jana alisema kuwa adui wa CCM ni CCM wenyewe.
 
Ninahisi Sept. 1 amri itakuwa ni kutembea mwisho saa 12 Jioni nchi nzima. Namba ni lazima isomeke. Hii itatusaidia sana koundokana na ujinga wa kuchagua kwa mazoea.
 
Shift za usiku hospitalini ataenda yeye na mkewe au anaongea pasipo kushirikisha ubongo
 
hahahaha hapo kazi itakuwa ni" kufyatua watoto" baada ya mwaka population huko A town itatisha.
 
Naona wafanye kwa nchi nzima kutembea mwisho saa 4,ili kila mwananchi aamke kutoka usingizini ajue hii nchi inaenda wapi!
 
Nadhani ni kutekeleza agizo la mfalme la kufyatua watoto lianze kutekelezwa mara 1
 
Viwanda halafu mnataka saa 12???????????????????? Kweli wabongo sio serious hata kidogo. Hivi huko sio kutangaza hali ya hatari? Hajui kwamba wengine wana majukumu yanaisha saa 4 hivyo wanatakiwa kurudi makwao? Viwanda byebye, Uchumi kwishaaaa!
 
Nampongeza sana aliebuni ukuta! Ameweza kuwahamisha serikali nzima attention yao imehamia ukuta! Ikifika tarehe 1 tunasogeza mbele mwezi 1 hadi 1st Oct! Mwendo ndio huo!!! Policcm wamechotwa akili zote!! Hawajielewi masikini!!
 
Iliwahi kuandikwa hapa kwamba dikteta uchwara atatangaza curfew sasa usishangae wilaya na hata mikoa chungu nzima kufuata hili, na saa nne ya usiku inaweza kufanywa saa mbili za usiku asionekane kiumbe yoyote yule anayeitwa binadamu barabarani.

Wakuu,

Nilibahatika kwenda kwenye mkutano leo nikamsikia mkuu wa wilaya ya Arumeru akisema mwisho wa kutembea ni saa nne usiku. Yaani mpaka kufikia saa tano asionekane raia yeyote zaidi ya askari polisi.

Huku akimsisitiza mkuu wa polisi "nadhani umenielewa" Hii imekaaje kihaki za raia wadau.
 
Wakuu,

Nilibahatika kwenda kwenye mkutano leo nikamsikia mkuu wa wilaya ya Arumeru akisema mwisho wa kutembea ni saa nne usiku. Yaani mpaka kufikia saa tano asionekane raia yeyote zaidi ya askari polisi.

Huku akimsisitiza mkuu wa polisi "nadhani umenielewa" Hii imekaaje kihaki za raia wadau.

Je ana mamlaka ya kutoa kauli hio?
Wataalam wa sheria nisaidieni plz
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nikitoka Mbeya via Chalinze nafika Arusha mda gani??

Au ndio nikeshe stendi??

Kachemka huyooo....
 
Hana mamlaka ya kutoa kauli kama hiyo, amekurupuka lakini tusisahau kwamba tuko kwenye zama za kukurupuka anajua atatoa kauli kama hii na hakuna atayemkaripia huyu kwa kutoa kauli ambayo hastahili kuitoa. Mwenye kustahili kuitoa kauli hii ni Magufuli na lazima atangaze sababu za kuweka curfew, au huyu DC labda kapata kibali kutoka Ikulu cha kuzuia watu kuwepo barabarani baada ya saa nne za usiku.

Je ana mamlaka ya kutoa kauli hio?
Wataalam wa sheria nisaidieni plz
 
Back
Top Bottom