Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,637
Arusha. Amina Jamali (18) amekutwa amekufa katika nyumba ya kulala wageni ya Lightness iliyopo jijini Arusha.
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Salumu Hamduni ameieleza Mwananchi Digital leo Jumamosi Desemba 5, 2020 kuwa taarifa za awali ni kuwa msichana huyo amekufa kifo cha kawaida.
Akizungumzia tukio hilo mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kaloleni Magharibi, Hassan Sharifu amesema baada ya kupata taarifa za kifo hicho alifika eneo la tukio na kubainisha kuwa watu wa karibu wa msichana huyo walikuwa wakimtafuta bila mafanikio.
Amesema walipoona kimya kwa kuwa walimwona akiingia kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni walikwenda kumtafuta na walipogonga mlango haukufunguliwa lakini walipoufungua na kuingia ndani walimkuta amefariki dunia huku akiwa akitokwa damu puani.
©@Mwananchi
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Salumu Hamduni ameieleza Mwananchi Digital leo Jumamosi Desemba 5, 2020 kuwa taarifa za awali ni kuwa msichana huyo amekufa kifo cha kawaida.
Akizungumzia tukio hilo mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kaloleni Magharibi, Hassan Sharifu amesema baada ya kupata taarifa za kifo hicho alifika eneo la tukio na kubainisha kuwa watu wa karibu wa msichana huyo walikuwa wakimtafuta bila mafanikio.
Amesema walipoona kimya kwa kuwa walimwona akiingia kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni walikwenda kumtafuta na walipogonga mlango haukufunguliwa lakini walipoufungua na kuingia ndani walimkuta amefariki dunia huku akiwa akitokwa damu puani.
©@Mwananchi