Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
- Thread starter
- #41
PointMkuu yule mwenye mwenyekiti kule Kigoma kupotea kwake amehusishwa DSO, na hapa anatajwa DSO, jee sasa iwe wazi kuwa hawa ma DSO ndio watu wanaoteka na kuua wenzao?
Kule Tarime walio jaribu kumteka Zakaria usiku walikuwa maafisa usalama sema Mkuria yule akashtukia mchezo akawatwanga shaba mpaka wakajitambulisha, lakini ilikuwa imetoka na tungempata kwenye viroba.
Jee wananchi sasa wajue huwa hawa maafisa ndio wabaya wao? Kweli nchi ifikie hapo jamani?
Zamani hakuna watu walikuwa wanapendeka kama ikigundulika wewe ni UWT, Lakini sasa unaogopa hata kujulikana hivyo kwani unakuwa huna tofauti na mumiani mbele za raia.
Awamu ya Tano imepatwa na nini?