Mimi nilikuwa Arusha mwaka jana, na kwa kweli nilifurahishwa sana na mabadiliko niliyoyakuta baada ya miaka mingi. Lakini vilevile nilisikitishwa sana na jinsi mji ulivyokuwa na vurugu na ubovu wa miundo mbinu. Kwa mfano:
Soko kuu la mjini na soko la Kilombero yanahitaji usaidizi wa hali ya juu. Watu ni wengi sana, kiasi kwamba inabidi lijengwe soko linguine, tena nje ya mji ili kupunguza msongamano wa watu. Sidhani kama wale wafanyabiashara wanaopanga vitu chini, pale nje ya haya masoko, wanaridhika na ile hali
(Kwa soko kuu la mjini) Watu wanaofanya biashara, upande wa magharibi ma soko kuu karibu na (Petro Station zamani ilikuwa inamlikiwa na familia ya LUKUMAI) watafutiwe sehemu nyingine ya kufanya biashara badala ya kufunga barabara yote. Ni hatari sana kwa usalama wa raia.
Mji wa Arusha hauna barabara. Kila kitu lazima kipitie Uhuru Road. Matokeo yake hii barabara imekuwa kama kichochoro. E.g. Kiford kinatoka majengo JR kwenda mjini lazima waingie Uhuru Road vinginevyo hakuna safari. Kuna barabara ya kupitia Sakina, ambayo ingekuwa njia mbadala kwa wakazi wa Majengo JR na Sakina, lakini haifai kwa makongoro. Mji una barabara 4 tu: Uhuru road, barabara ya Sakina/Namanga, Barabara ya Njiro na Moshi Arusha. Ni barabara chache sana.
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri beid Unatisha. Yaani A-Town inhitaji uwanja mpya. Uwanja unatia kichefuchefu.
Mitaa ya Bondeni na Majengo, karibu na standi ya mabasi ni hatari tupu. Kuaanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 12 jioni hapapitiki. Bidhaa mpaka barabarani. Ukiwa ni gari kasheshe tupu. Yaani sehemu haipitiki. Ni hatari kwa maisha ya watumiaji.
Takataka zimezagaa mji mzima utafikiri mji hauna wasimamizi au watu hawalipi kodi.
Kulikuwa na mpango wa kujenga barabara upande wa SINONI ili kupungza msongamano Uhuru Road, sijui kama hilo limefanyika. Wageni wote wanalalamika tatizo la traffic mjini Arusha. Ni hatari sana kuvuka barabara. Madereva wa viford, bodaboda, mikokoteni na baiskeli hawaheshimu sheria za barabarani. Inaonekana Jiji halina suluhisho la hili tatizo.
Maeneo mapya yanayogawiwa kwa wananchi bado hayaendelezwi na serikali. Hakuna barabara, mifereji ya maji machafu, wala sehemu za mapumziko. Mfano mzuri ni NJIRO Barabara mbaya, hakuna mitaro ya maji machafu n.k
AJIRA: Vijana wengi, tena wenye nguvu za kufanya kazi hawana ajira. Ni kweli kwamba SEKTA ZA UTALII, MADINI NA USAFIRISHAJI zinatoa ajira kwa wananchi, lakini inabidi sekta ya viwanda ipewe kipaumbele. Hii itasaidia sana kukuza ajira na kuongeza pato la JIJI.
Administration ni zero!!!!! Ili mji uwe mji uende kama mji, unahitaji transportation, communication, electricity, water supply for human consumption, policing, garbage collection and sewer system. Na hapa ndipo Management imara inapohitajika, vinginevyo ni CHAOS. Laissez-faire approach kwenye city management ni MAJANGA. Huu ni mtazamo wangu tu.:A S 103: