Arsenal (The Gunners) | Special Thread

So far mwanzo mzuri sana. Misimu ya nyuma tulikua tunaharibiwa mbio za ubingwa na mechi kama hizi za akina Sunderland, Brighton, Brentford, Bournemouth bila kumsahau Aston Villa na Newcastle. Tumepiga Villa kwao, tumechuchukua points 3 juani (Stadium of Lights) next weekend tuko AMEX stadium kwa watukutu wengine Brighton. Tukishinda hii mechi itakua ni huge boost kwa timu yetu kuelekea international break. Timu ipo, at least now unaangalia kwenye bench unaona kuna watu wa kubadilisha mchezo. Kuna mdau amemzungumzia Saka, mi naongeza na Eze, jamaa amekua na performance ya kupanda na kushuka na ni kama anaanza kupoteza kujiamini hivi...!
 
Ugomvi ulipotokea katika hapa na pale Konsa akamnasa Xhaka.

Akamtikisa kwanza ila Xhaka naye mbabe akagoma.

Konsa akamuambia Xhaka "Tuonane nje"

Wazee tumesajili gaidi. Aina ya beki forward anakua anamuogopa hata kumsogelea.

Konsa hajajali kama Xhaka aliwahi kua kapteni pale Arsenal na mwisho akamuonyesha ishara ya kuchinja
 


Unafunga, ukileta ujinga unapigwa makofi
By February arsenal, anatangazwa ubingwa
 
arsenal inacheza mpira mgumu mno wa kimahesabu ambao unahitaji mchezaji uwe vizuri kwenye ubongo.. ni kama una solve trigonometry and calculus questions.

hauhitaji wachezaji wa kukimbia hovyo na mpira.
 
Sisi ambao tumeanza kufuatilia mpira kabla ya ujio wa makocha wanaodictate kuanzia kujiposition mpaka idadi ya pasi tulikua tunamuangalia mchezaji na kufurahia anachofanya.

Hatukuwahi kua busy kuangalia statistics iwe pasi, chance creation au assists. Ndiyo sababu kizazi chetu kilimheshimu Drogba na kuamini ni bonge la striker.

Lakini hivi karibuni wameanza kumuita average kwakua amefunga magoli 104 misimu 9 aliyoishi EPL. Ni kama kusema kila msimu alikua na wastani wa magoli 11.4.

Kwa mpira wa siku hizi Okocha na Ronaldinho wangeonekana hawajui kwakua entertainment waliyonayo miguuni haikupi magoli constantly. Tulienjoy kuona akifanya step overs, akizipiga roulettes, akiwapiga watu kanzu. Magoli atafunga Etoo ila macho yetu kwa Dinho.

Na tutakumbuka goli la Dinho dhidi ya Chelsea alilofunga huku anakata viuno kuliko magoli mengi ya Etoo.

Newcastle walikua na mtu anaitwa Alan StMaximin, aina ya wachezaji kama Okocha. Bahati mbaya alikuja era ambayo ule mpira unahesabiwa unakwamisha mashambulizi akauzwa China.

Angalia ligi ya EPL wachezaji wangapi wanajiexpress kama Ronaldinho? Hakuna. Sana sana mchezaji atafanya step over au atafanya body faint ili a-cut in ashoot. Kwa miaka yetu ya karibuni waasisi wa aina hii ya wing alikua Ribery na Roben.

United walinunua winger ambaye ilidhaniwa atakuja na hizo expressions na kunyanyasa mabeki, Antony, hakumaliza misimu miwili.

Sasa tuje kwa Saka. Timu ya taifa ya UK alikuepo Southgate kama kocha alikua akiita timu ya taifa Saka anaanza, akipumzika anaingia Madueke au Palmer.

Amekuja Tuchel, huyu sasa hata kumuita Palmer timu ya taifa hajamuita na walikua wote chelsea hawa. Sasa swali ni imekuaje makocha wanne wote wanaona Saka anatakiwa awe kule alipo?

Jibu jepesi ni output. Na hii ilisemwa mwanzoni kabisa msimu wa 22/23 kwamba hana madoido anautegemea sana mguu wa kushoto lakini haina shida kwakua anautendea haki mguu wake wa kushoto.

Saka alikua mchezaji mwenye speed kuliko Martinelli. Alivyopata injury na kurudi amepunguza kukimbia na decision making imekua ya uoga tofauti na mwanzo lakini Arsenal bado haina RW wa kumsusia wing ile. Usifananishe Dowman na Yamal kwakua Yamal anacheza ligi ambayo Rodri anaishangaa inakuaje na wachezaji dhaifu wapo ligi kuu.

Pili angalia Saka akipata mpira anatakiwa kuwavuka wachezaji wangapi? Mara nyingi ni wawili au watatu na kilichosemwa msimu wa 22/23 kwamba hana madoido bado tunakiona hapa kwamba hawezi wachambua watu watatu bila kutoa pasi.

Tafuta wingers wa timu zingine hua wanazingirwa na wapinzani wangapi ili kuelewa kwanini huyu dogo kila kocha anaona ni mtu sahihi kua RW.
 
Hapa nitaonyesha screenshots za RW wengine ambao timu zao zipo ndani ya top four.

Kwa sasa hivi top four ipo Arsenal, Man City, Hull na chelsea.

RW wa City ni Semenyo. Wa Hull ni Belloumi na wa chelsea ni Neto.

Sasa angalia kwenye hizi screenshots kisha ujibu mwenyewe kwanini Saka bado ni chaguo la kwanza kwa makocha wote.

 
Kwa niliyeanza kufuatilia mpira zamani Jesus ni ST bora kwangu kuliko Kai na Gyokeres kwa sababu naamini Jesus akibaki na mabeki wawili hashindwi kuwafuata huko huko kwenye boksi.

Hatotumia nguvu, atajaribu kufanya faints na Cruyff turns ili kumfikia kipa. Hapa utakumbuka goli alilowapiga nyumbu, inasemekana Dalot bado anaslide.

Kai atageuka kutafuta wa kumpa pasi.

Gyokeres atalazimisha kwenda kwa kutumia nguvu na atapoteza mpira.

Lakini chukua stats.

Gyokeres amescore magoli 20 hivi. Kamzidi Drogba kwa wastani ambaye for years anahesabiwa ni legend. Sasa kwanini Gyokeres anapokea maneno mengi?

Mwaka 1998 tulisuluhu na Middlesbrough 1 - 1 mashabiki wakawa wanazomea. Wenger akasema "Ni ngumu mtu aliyezoea kula caviar akakubali kurudi kula soseji"

Jibu hilo hapo.

Arsenal ilishakua standard ya mpira quality na sexy football kiasi kwamba mashabiki waliona hawastahili suluhu na hawastahili mpira unaoboa.

Abramovich aliwahi kutaka kumfukuza Mourinho kwakua aliona chelsea inacheza mpira wa hovyo ikilinganishwa na Arsenal.

Mashabiki wanakubali kwamba Gyokeres ni mzuri kuscore ila wanaona wanalishwa soseji wakati wamezoea caviar.

Sasa hii timu iwe hivi hivi kila kitu kuanzia wachezaji, kocha na matokeo halafu iwe ni manchester united au chelsea. Uone kama kuna shabiki wao atayekuja kusema Saka hafai au Gyokeres hafai.
 
Penati waliyogewa Sunderland watu wameikalia kimya kwakua matokeo yapo upande wetu.

Mchezaji wa Sunderland anaanza kwa kumshika Konsa jezi na kumvuta, Konsa anareact.

Refa anasema Konsa kamdondosha mtu.

VAR inaangalia inakubaliana na uamuzi wa penati.

Lakini hakuna aliyeangalia nani kaanza kumshika mwenzake. Arteta amesema inabidi wapewe maelezo juu ya kilichotokea.

Hii imesapotiwa na baadhi ya wanamichezo wa zamani, kama mtakumbuka ni siku nne tu zimepita tangu tulivyoleteqa ripoti kwamba dhidi ya Villa ilibidi tugewe penati ila refa na VAR wakafunika.
 
Swali la kujiuliza.

Upuuzi aliofanya Foden kama bado kocha angekua Pep angeufanya?

Umeona siku hizi hasira za kipuuzi hazipo Arsenal?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…