Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ni kosa kubwa sana Arsenal itakuwa imefanya, yale yale ya Sebastian Larsson na Serge Gnabry.
Tusiwe watu wa kulaumu kila jambo bila kuangalia pande zote,

Ishu ya Gnabry dogo alitaka kuhakikishiwa namba 1st 11 na kwa muda ule alikuwa bado sana,
Na kumbe Bayern walishaongea nae tayari wampitishe mlango wa nyuma(Werder Bremen) ili wamchukue kirahisi, hivyo fitna ilifanyika hapa, hivyo suala la madai ya 1st 11 ilikuwa kama anatingisha tu,

Suala la Lucas yeye madai yake ni nafasi ya kucheza ktk 1st 11 pia na Arteta ameshindwa kumhakikishia hilo, maana Mikel yupo kwenye hatua ya kuijenga upya timu, na yeye ndio anajua yupi anafaa na yupi hafai kuwepo katika mifumo yake,

NB: Hakuna kocha yeyote duniani anayetaka mchezaji wake mzuri/tegemeo aondoke tena ktk kipindi kama hiki cha ujenzi wa timu, tuwe na subira tumpe muda kocha ajenge timu.
 
Yes! Ukiwa na Squad Depth hata treble unapigania, hata akisajiliwa Partey bado Torreira abaki tuwe na viungo waliokamilika wanne maana kwa wiki ni mechi mbili hadi tatu lazima wote watacheza.

Good idea, the problem comes to wage bill, that is the reason they are offloading even our dependable backup players like AMN, Torreira and Kolasinac. Ukisema uwauze akina Willock, Smith na Nketiah, definitely they cannot fetch good price. Most of the teams selling are in dire need of cash to replace outgoing players
 
Kumuondosha Torreira na Kolašinac bora kumuondoa Sokratis, Maitland-Niles na takataka aina ya Willock, Nelson na Nketiah.

Depth Squad Matter
 
Auba ni mshambuliaji mzuri naweza kusema level ya akina Thierry Henry

Ila kabla Auba hajaja Arsenal ilikuwa ya 2, 3 lakini Auba alipokuja 2018 Arsenal ikashika nafasi ya 6 au 6, na sasa 8
 
Inauma sana na itazidi kuuma Willian kuja Arsenal chama kubwa
Mahesabu yenu aisee!, hayana tofauti na kilimo cha matikiti maji.
Kikosi hiki ni nooma tuombe wasajiliwe tu!!
 
Breaking news.
No more food will be served at the emirates stadium. Players will be authorized to carry packed lunch from home due to the firing of the kitchen staff to fund captain aubameyang's contract.
Live from London.


 
Ambitious Arsenal are set to spend £100million this summer to sign key targets Thomas Partey, Gabriel Magalhaes and Dani Ceballos. [Mark Irwin]
 
Hivi Chelsea wataenda uwanjani kweli?

Kamati ya wajumbe:
 
Sifa za Gabriel Magalhães :

Ni mzuri sana kwenye kukaba 1v1 yani uso kwa uso. Ana nguvu sana, ana kasi pia na ni mwepesi. Na ni mzuri sana kwenye mipira ya juu, urefu wake ni 6ft 3 inches.

Gabriel ana wastani wa kucheza mipira 5.1 ya juu ndani ya dk 90 msimu huu na alifanikiwa kushinda mipira 3.4 ndani ya dk 90.

Kwa kulinganisha tu, Van Dijk na Maguire wana wastani wa kushinda mipira ya juu kwa 4.9 na 4.6.

Gabriel Magalhães hapitiki kirahisi na wachezaji wenye kasi, kitu ambacho mabeki wetu wa kati wa sasa kina washinda sana.

Magalhães sio aina ya beki wa kuchezea mpira kama Luiz, Laporte n.k ila anajitahidi katika hilo kutokana na aina ya mchezo wa Lille ya kuanza kucheza kutokea nyuma kama sisi chini ya Arteta.

Magalhães anajitahidi kupiga mipira mirefu pia na hakuna beki wa Ligue 1 aliyemzidi katika kupiga basi ndefu katika robo ya mwisho ya adui.

Magalhães ana mapungufu pia kama wachezaji wengine na kwa upande wake swala la positioning anahitaji kulifanyia kazi hasa kama atakuja ndani ya EPL.

#coyg
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…