Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Habari za Usajili.

Aaron Ramsey anazungumza na timu tano za nje ya Uingereza.



Aaron Ramsey yupo huru kuzungumza na timu yoyote itakayota kumsajili kuanzia tarehe 1 mwezi huu wa January.

Mchezaji huyo wa kiungo wa Arsenal na timu ya taifa ya Wales anaruhusiwa kusaini mkataba mpya au kukubali mkataba mpya kuanzia leo hii kabla ya mkataba wake na Arsenal haujamalizika mwezi Julai mwaka huu.

Ramsey yupo huru kuzungumza na timu za Bayern Munich, Inter Milan, Juventus, Paris St-Germain na Real Madrid.

Arsenal walimwekezea mezani Ramsey mapendekezo ya mkataba mpya wa miaka minne mwezi September mwaka jana, lakini badae wakaachana nao kutokana na sababu za kifedha na kimpira.

Kocha wa Arsenal Unai Emery alitaka amtumie Ramsey katika uundaji wa timu mpya lakini hali hiyo imekuwa ngumu kwa Ramsey kutoweza kufuata mpango huo mpya wa Emery na pia Arsenal kutopenda kugharamia mikataba yenye gharama kubwa kwa wachezaji ambao ufanisi wao uwanjani hauridhishi,.

Itakumbukwa kuwa wakti wa usaili kocha Emery alikuja na taarifa za kila mchezaji wa Arsenal taarifa ambayo ilijaa vigezo vyote ambavyo wachezaji wanatakiwa kufuata.

Hadi sasa wachezaji Mesut Ozil na Aaron Ramsey viwango vyao vya uchezaji na ufanisi bado havijaweza kumshawishi kocha Emery kuendelea kuwatumia uwanjani.

Juventus ya Italia imempa offer Ramsey ya mkataba wa miaka minne wenye mshahara wa wastani wa pauni milioni 5.8 kwa mwaka, ambapo kama akicheza nusu ya mechi zote basi atapewa mshahara wa pauni milioni 6.3.

Endapo atacheza asilimia 70 ya mechi za timu hiyo na kuweza kuwa mmja wa wachezaji waandamizi Ramsey atalipwa mshahara wa pauni milioni 7 kwa mwaka sawa na pauni 138,000 kwa wiki.

Ramsey tayari amezungumza na PSG ambao wanataka kubadilishana na Arsenal mchezaji wa kiungo Adrien Rabiot lakini Ramsey anapendelea kwenda timu ya Juventus.
 
Nitakumis endapo utaondoka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Atuondolee na lichtstneiner amechoka yule mzee asije fia uwanjani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Some bad Arsenal results against big teams in last 7 years :

Bayern 5-1 (thrice)
Liverpool 4-0
Liverpool 5-1
Chelsea 6-0
City 6-3
United 8-2
City 3-0 (twice)

Wenger failed to build a sustainable defence in over 10 years. Some unwilling to give Emery even 6 months. Sounds fair.
 
Bila kusahau

Liverpool 3 Arsenal 6

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati uku kwetu Africa tukiwa kwenye kutawaliwa kumbe wenzetu walikuwa wanakipiga tu?

Zile sheria 17 za soka zilikuwepo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Arsenal news: Bodi ya Arsenal ina Imani na Unai Emery lakini haitaidhinisha fedha zaidi za usajili mwezi huu.

Emery kupewa kitita cha kutosha kusajili wachezaji mwezi Juni


Unai Emery akiwa na wachezaji wake kwenye mafunzo -Training.


Bodi ya klabu ya Arsenal badi ina Imani na kocha Unai Emery licha ya matokeo mabaya ya kufungwa na Liverpool mabao 5-1.

Arsenal sasa ipo nyuma ya Chelsea kwa point tano na baadae leo ikishinda mechi na Fulham inaweza kupunguza pengo kuwa point 2.

Unai Emery alisaini wachezaji watano msimu ulopita lakini hadi sasa ni Lucas Torreira na Matteo Guendouzi ambao wameng'ara uwanjani.

Wachezaji ambao walisajiliwa an Emery ni pamoja na Lucas Torreira kutoka Sampdoria, pauni 27.0milioni, Bernd Leno kutoka Bayer 04 Leverkusen kwa pauni 22.50m Sokratis kutoka Borussia Dortmund kwa pauni 14.40m, Mattéo Guendouzi kutoka FC Lorient pauni 7.20m na Stephan Lichtsteiner kutoka Juventus ambae alisajiliwa bure.

Bodi ya Arsenal imeamua Emery afanye kazi na kikosi alicho nacho na kusubiri mwezi Juni huku kikosi hicho kikiwa na wachezaji kadhaa ambao ni majeruhi, lakini huku ikiangalia uwezekano wa kupata wachezaji wa mkopo.

Habari za uhakika kabisa zinasema kwamba mmiliki wa timu ya Arsenal Stan Kroenke hatatoa fedha za ziada kwenye dirisha hili la usajili lakini atakuwa tayari kutoa kitita cha kutosha mwezi Juni ili kumfanya Unai Emery asajili wachezaji anaowataka mwenyewe.

Endapo Stan Kroenke atatoa fedha zake mwenyewe basi Arsenal wanaweza kuadhibiwa kuwa kutofuata mfumo uitwao Financila Fair Play unaokataza wamiliki wa timu kutumia fedha za nje ya bajeti kwa msimu uliopo.

Habari za timu itayocheza na Fulham baadae leo kufuata, stay Tuned.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…