Arsenal bado wamng'ang'ania Alvarez

Arsenal bado wamng'ang'ania Alvarez

Miss Halima

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2026
Posts
226
Reaction score
507
Zikisalia siku tatu kabla ya dirisha la usajili kufungwa rasmi, Arsenal hawajakata tamaa katika harakati zao za kumsajili mshambuliaji wa Argentina Julian Alvarez, 26, ambaye inadaiwa anataka kuondoka Atletico Madrid. (Mail).

Manchester City wanamfuatilia kiungo mshambuliaji wa Everton Iliman Ndiaye, 26, ambaye thamani yake ni takriban pauni milioni 80. (Guardian)

Aston Villa imewasiliana moja kwa moja na AC Milan kuhusu winga wa Ureno Rafael Leao, 27, katika jitihada za kuipiku Galatasaray katika mbio za kumsajili. (Fabrizio Romano)

Nottingham Forest imewasilisha ofa yenye thamani ya hadi pauni milioni 22 kwa beki wa pembeni wa Crystal Palace na Colombia, Daniel Munoz, 30. (Athletic)

Atletico Madrid inafikira kuwasajili washambuliaji wa Brazil Igor Jesus, 25, wa Nottingham Forest na Gabriel Jesus, 29, wa Arsenal. (Fichajes)
1787903617242.png
 
Sisi kama Man utd tunasemaje, Atletico endeleeni kukaza. Hauzwi!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom