Arafat Haji mtu chuma kweli kweli

Oh

Unajua vizuri katiba ya nchi?
Raia asiye Raia wa Tanzania hawezi kumiliki ardhi Tanzania
Hao Wachina wanamiliki vipi ardhi Tanzania
Nenda kwenye website yao,hizo nyumba zinamilikiwa na kampuni ya kichina,wanafanya biashara ya Apartments,mbona hujiulizi Feza Schools ni ya Waturuki,wamewezaje kumiliki ardhi Tanzania?
 
Hivyo Arafat ndio point tatu zenu utoponyo lasivyo Derby haitachezwa Siyo???? Hahahaha hahaha

Wenye akili ni wawili tuu


Hahahaha
 
Vihoja na viroja haviishi Tanzania yangu!
Nikajua labda Mama Karume angalau anaweza kuwa na kauli ya mwisho, sasa kumbe Hersi anafanya nini pale Yanga!???
Huwezi kuelewa
 
Msimu ujao sisi TFF tunakuja na klabu ambayo haimiliki uwanja wa mazoezi hakuna kucheza ligi. Anzeni kuboresha pale kaunda ,aah.
Hawana ubavu huo. Kwanza hao viongozi wa wakati huo watakua wanajielewa, sio kama hawa wa sasa ambao mwaka huu hawatoboi kwenye hizo nafasi zao.
 
Usitupoteze kizembe,sema viongozi wetu wote vyuma akiwemo hersi.
Mnaweza kufanikiwa mchana ila kumbukeni siku huwa hazigandi mtakuwa mmeingia kwenye kitabu cheusi cha usalama.Ni suala la muda tu hii ni Tanzania
 
TFF wamefanya utoto sana yaani mechi inatangazwa saa sita eti hakuna mechi na bila sababu yeyote ya msingi watafute sehemu ya kutoa points kwa hizo Timu waache mambo zao Karia hamna mtu.
 
Uyo chawa kawa chuma tokea lini,maisha yake anategemea teuzi za serikali ili aish aigomee serikali,
Si Bora hata uyo hersi kidogo anaweza kuwa na msimamo
 
Ni lini TFF na bodi ya ligi waliwahi kubali hayo mambo ya hovyo ya Yanga au timu zingine? Yanga na timu zingine wamemewajibishwa kwa kupigwa faini mara ngapi kutokana na kukiuka kanuni? Kwanini wao wanapovuruga kanuni wasiwajibike wanajificha kwenye kichaka cha busara na serikali?

Yanga si kwamba hiyo mechi hawataki kucheza. Karia hakuwa sawa kutoa kauli ya "kwani wao wako sawa kwenye uongozi wao?" Ilionyesha wazi kuna kitu kimekosewa anatafuta pa kukosea badala ya kuwajibika. Lakini aliharibu zaidi aliposema wakaendelee kucheza sinema. Hii ni dharau kwa viongozi wenzie wanaowakilisha mashabiki na wanachama zaidi ya 25M. Akikubali kuwa alikosea na kuomba msamaha Yanga inacheza mechi ya derby hata kama haitakuwa kwa kuachia ngazi.

Bodi ya ligi wakikubali walikiuka kanuni na kuwajibika Yanga inacheza Derby badala ya kukazana kuomba msaada kwa serikali. Bodi ya ligi timu zikikiuka kanuni wanazibonda kwa nini wao wasiwajibike kwa kwa hasara walizasabisha walipoahirisha mechi kwa utaratibu usio sahihi?

Mimi naamini Yanga inacheza Derby ila kuna watu lazima wawajibike kwa kauli zao au kukiuka kanuni.
 
Akili za wamasimba hizi. Hicho kikao ni cha kutoa points tatu? Hujui nani kikanuni anapaswa kutoa points tatu?
Anayepaswa kikanuni kutoa points 3 ameshawajibu kwenye barua yenu kuwa hilo haliwezekani kwa sababu hamna uhalali wa kikanuni wa kupewa hizo points 3.Suluhisho ni kwenda CAS,sasa nyie badala ya kusubiri barua ya maamuzi,kila siku mnatupugia kelele za "hatuchezi"
 
Una maana kwa vile Arafat anashinda Kizimkazi kwa Rais wa JMT basi Rais ataibeba Yanga katika hili sakata mlilolianzisha wenyewe, tutaona.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…