Apple ni marufuku kutumia chaji za Android

Wewe papai embu Soma kwa utulivu alichoandika jamaa ndicho Apple walichosisitiza.

Kwamba Type C kama waya wenye tech ya kawaida hauna shida,Ni Sawa na huo waa apple unaokuja na Simu,shida Ni hizi nyaya zenye Kasi zaidi ambazo sio mahusi kwa kwa simu husika za Apple.

Halafu huyu jamaa unayemjibu Kama umelewa ukimtumia vyema atakusaidia sana.
 
Unayemwelekeza huyo hili ndoo jukwaa lake....hatupingi mtazamo wako ila heshimu idea yake pia ikikufaa chukua isipokufaa pita vile
 
Watatema ndoano, yani apple wakiyakoroga huwa hawakubali lawama, lazima waitupie kwingine. Apple kwa sasa anagaragazwa na Google pixel, utawala wake mwisho mwaka huu. Pixel 8 ni 🔥 hiyo 9 ndio itakuwa funga kazi. Apple ibaki kwa wapenda show off.
 
Sasa kama type c ya iPhone ina pin 9 na za android zina pin 11, hapo ikichomeka hy yenye pin 11 si itakuwa inapeleka moto kwenye hizo pin 9 za iPhone huku pin mbili zilizobakia zitakuwa hazifanyi kazi au ipo vp.?

CC: Chief-Mkwawa
 
Sasa kama type c ya iPhone ina pin 9 na za android zina pin 11, hapo ikichomeka hy yenye pin 11 si itakuwa inapeleka moto kwenye hizo pin 9 za iPhone huku pin mbili zilizobakia zitakuwa hazifanyi kazi au ipo vp.?

CC: Chief-Mkwawa
Mkuu usb C ni Usb C na ina pin kibao, Jumla zipo pin 24 hivyo si kweli kwamba moja ina pin 9 na nyengine pin 11 zote zina pin 24
.

Namna ya kutumia hizo pin ndio inatofautiana na hakuna pin za Android na Ios bali kuna Pina za
-usb 2.0, usb 3.0, 3.1, 3.2, usb 4.0 etc
-usb power delivery, Qualcom fast charge, Vooc, warp charge etc.

Hizo usb no kuanzia 2 mpaka 4 zina maanisha speed ya kuingiza na kutoa data, simu zenye usb 3 kupanda zina uwezo wa video out kutumia simu yako na tv ama monitor kupitia type C.



Pin za katikati hizo hutumika kwenye usb 2.0 kwa simu zenye usb za kizamani lowend hizo pin 4 tu zinawatosha. Sometime unaweza ukanunua waya ukawa hauwezi kutumia kutoa video out ina maana huo waya una pin 4 tu za katikati hasa waya za bei rahisi za kichina

Hio njano inaonesha pin za power delivery ambayo iphone inatumia, inabidi charger ya iPhone iwe na pin kwenye hizo njano, uashawahi kuona waya zinachaji tu simu hazipitishi data? Ina maana hizo waya zina pin hizo za njano tu ila hawana pin za data.

Kwanini Apple wanasema Charger za Android zinaweza kuleta joto? Proprietary charger kama za Kina Oppo zinatumia mfumo tofauti na standard za type C angalia mchoro wa Vooc


Vooc Charger inatumia Vbus kwenye pin zetu za Type C pamoja na zile pin za usb 2.0 haitumii zile pin za standard za power delivery hivyo charger zao na usb cable zao sababu sio standard
1. Hazita fast charge Iphone na simu nyengine yoyote ambayo sio ya kwao
2. Zinaweza zalisha hilo joto sababu zinapeleka umeme kwenye Pin tofauti na simu haijakua programmed kupokea umeme kwa hizo pin so kutakua na process fulani ya kukataa.

Long story short mkuu, we fuata standard, power delivery yoyote ile ipo sawa na itatumia pin zile zile
 
Hahaha
Mkuu sikatai Google Pixel zipo vizuri.
Ila Apple ana simu nzuri kuliko za Google Pixel.
Ni wewe tu uchague unataka iOS au Android maana software no subjective.
Ila tuje kwenye mambo mengine display, battery life, overall camera system, gaming and performance, speakers, video quality, Face ID, nk Apple zipo vizuri kuliko Google
 
Mkuu... Ni kweli unachosema ila mimi naona kwa Watz kama wakinunua iPhone 15 series ni heri tu na charger za Type C wanunue za Apple maana wengi hapa Bongo hawana uelewa wa haya mambo

Huoni umeelimisha kidogo tu watu wanasema utawaunguzia simu zao [emoji23][emoji23][emoji23]

Kwenye haya mambo Wabongo bado sana
 
Sio kweli. User experience ni nzuri zaidi kwenye pixel phones. On paper apple zipo vizuri. Kitu ambacho kwa sasa apple bado wapo juu ni video. Basi. Display anagaragazwa vibaya na super actua display za pixel, design anapigwa. Camera anapigwa. Software ndio anagaragazwa mbali kabisa, huwezi fananisha siri na Google assistant, transcription, translation,haptics. Acha we. Apple's reign is up.
 
*iPhone 15 Pro Max ina performance kubwa zaidi kupitia AnTuTu v10 benchmark, iPhone 15 Pro Max ina 1571000 score wakati hiyo Pixel 8 Pro ina 1141000 score. Inapitwa hata na 14 Pro kwenye performance
Google Pixel 8 Pro inatumia Google Tensor G3 (4nm) wakati 15 Pro Max ina Apple A17 Pro ambayo inafanya iPhone 15 Pro Max kuwa na performance kubwa kwa asilimia 38 zaidi ya Pixel 8 Pro
Benchmark zote zinaonesha Pixel imekalishwa parefu kuanzia GPU hadi CPU

*Hiyo display unayosema kuwa imeishinda iPhone ubora ni display ya Pixel ipi. Kama ni 8 Pro, basi Pixel 8 Pro imefanikiwa kushinda brightness simu zote kasoro iPhone 15 series.

*Kwenye ukaaji wa chaji huku Pixel ndio haigusi kabisa. Battery test za Google Pixel 8 Pro na iPhone 15 Pro Max zimefanywa na results zinajitosheleza. Soma hapa

GOOGLE PIXEL 8 PRO
Web browsing: 11hrs 6min
Watching videos: 15hrs 40min
Gaming: 4hrs 19min
Standby: 81hrs
General battery life: 30hrs 8min

IPHONE 15 PRO MAX
Web browsing: 17hrs 3min
Watching videos: 22hrs 31min
Gaming: 6hrs 42min
Standby: 154hrs
General battery life: 48hrs 25min

Hakuna sehemu hata moja ambayo Pixel katoboa mbele ya iPhone

*Speakers: iPhone 15 Pro Max ina Dolby Atmos, Pixel 8 Pro haina.

Na bado iPhone 15 Pro Max inawekewa uwezo wa kucheza games za Resident Evil Village, Resident Evil 4 Remake na Assassin's Creed Mirage mwaka huu (2024) kama tu unavyocheza kwenye PS bila kubadili chochote

Flagship za Apple ziko vizuri kushinda Pixel, kinachokuja kutofautisha unachohitaji ni software tu, aidha unataka Android au iOS ila kwa sehemu nyingine nyingi iPhone zipo vizuri

Halafu kwenye kamera kiujumla, Google Pixel 8 Pro inapitwa na iPhone 15 Pro Max. Angalia comparison mbalimbali mfano anza na hii [emoji116][emoji116]

View: https://youtu.be/RyVitycWTZU?si=NAa4TDVOM9XfSF5e
 
Apple Ni Wazuri Wana Marketing Skills Kubwa,hapo Wanatengeneza Soko La Usb Zao Baada Ya Kuona Zinaanza Kudoda,Pia Walitoa Headphone Jack Kwenye Flagship Zao Kuanzia Iphone 7 Wakisingizia Aina Ya Display Kumbe Wanakuza Soko La Earpod Na Ndo Wanachofanya Sasa
 
Hizo ni on paper sio real life, ma benchmark yapo calibrated na iphone mzee, The best display ni ya pixel 8 series no doubt. Kwenye camera ni video tu ndio apple ipo juu, pengine ni taabani. Acha kukariri. Apple sio kila kitu.
 
Ukitumia charger ya android iPhone 15 inakupa taadhari utumie made for iphone (MFI) cable/charger
 
Hizo ni on paper sio real life, ma benchmark yapo calibrated na iphone mzee, The best display ni ya pixel 8 series no doubt. Kwenye camera ni video tu ndio apple ipo juu, pengine ni taabani. Acha kukariri. Apple sio kila kitu.
Niambie maana ya On paper ni nini mzee

Google Pixel 8 Pro on paper wanasema inafikia peak brightness ya 2400nits, iPhone 15 Pro Max ni 2000nits
Lakini gsmarena wametest wamekuta Google Pixel 8 Pro inafikia 1600nits tu, iPhone 15 Pro Max anafikia hadi 1800 huko.
Hapo nani anadanganya on paper??

Kwenye kamera unaanzaje kusema iPhone ni video tu? Basi na mimi nasema Pixel ni picha tu kwingine majanga. Itakuwa sahihi kusema hivyo?
Hiyo video ya camera comparison niliyokuwekea umejisumbua hata kuiangalia? Kamera overall ni kuanzia main camera, ultrawide camera, telephoto lens, selfie camera na kuna mengi sana ya kutest ukiondoa hizo video na picha za kupoint na kushoot. Nimekuwekea hiyo video ili uone maana on paper Pixel 8 Pro ina camera specs nzuri kuliko iPhone ila kwenye kuzitest iPhone inaperform better kuliko Pixel 8 Pro. Again nani anadanganya on paper?

Kuhusu battery life, hizo sio results za On paper. Pixel 8 Pro ina 5050mAh on paper na iPhone 15 Pro Max ina around 4000mAh ila bado inatunza chaji parefu kushinda Pixel 8 Pro. Pixel 8 Pro ina utunzaji wa chaji mbovu ukifananisha na iPhone 15 Pro Max. Hii sio on paper mzee. Gsmarena wametest, kasome review Acha ubishi
Hapa pia, nani kadanganya on paper?

Kwenye performance Google Pixel 8 Pro imeachwa mbali na iPhone 15 Pro Max kuanzia on paper hadi in real life. Tests zimefanywa kaangalie. Gsmarena wamethibitisha, Pixel 8 Pro inazidiwa performance hadi na Qualcomm Snapdragon 8+ Gen 1 ambayo hii imetumika kwenye Xiaomi 12S Ultra. Kama Xiaomi 12S Ultra inazidi Pixel 8 Pro kwenye performance, sembuse iPhone 15 Pro Max?

Acha kusema neno "ON PAPER" kama hujui maana yake badala yake kafanye utafiti kwanza ndio uje kutetea unachokisema kwa data
 
Android pin 11 na iPhone 15 pin 9 sasa bado ni layman au mnaponda tu
 
Wewe unamjua Chief Mkwawa au umekurupuka?

Waambie iPhones wazilete zikiwa na charger waache blah blah
 
Apple aliondoa earphone jack ili kuungana na sera ya utunzaji wa mazingira,
Earphone na charger vinachafua sana mazingira ndiomana wamelazimishwa pia kuungana na wengine kwenye matumizi ya type C ili kupunguza uchafuzi wa mazingira, mana charger zitakuwa chache ikiwa tutakuwa tunashare kati ya brand na brand nyingine.

Fikiria una iphone na android afu una charger mbili tofauti, hata port ya type C atakuja aitoe kabisa mana matarajio Yao ni kuwa na simu ambayo Haina tundu kabisa.
 
Android pin 11 na iPhone 15 pin 9 sasa bado ni layman au mnaponda tu
Type C zote ni pin 24/12 huwezi ukaweka type C Yako mwenyewe ikaitwa Type C. There is a reason kwanini ni standard, standard ina maana zinafanana zote, we unafikiri Umoja wa Ulaya ni wajinga kuforce Apple Watumie Type C halafu wawaache waharibu standard?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…