Ansbert Ngurumo: Roma 1,300, CCM 50

Ansbert Ngurumo: Roma 1,300, CCM 50

CCM imezaliwa mwaka 1977. Hivi sasa ina miaka 35. Mwandishi anaueleza umma kuwa CCM bado itakuwa na nguvu kwa miaka mingine 15 mpaka itakapotimiza miaka 50. Si haba...
ccm ni mixture ya ASP & TANU na ni viongozi wa vyama hivyo vilivyoungana walikiongoza kwa mmuda mrefu na sera zao ndio zipo kwenye ccm ya sasa. Unaweza sema hakikuzaliwa bali kilipatiwa jina jipya lengo lilikuwa kuondoa utofauti wa majina ili kupata nguvu ya umoja.
 
ccm ni mixture ya ASP & TANU na ni viongozi wa vyama hivyo vilivyoungana walikiongoza kwa mmuda mrefu na sera zao ndio zipo kwenye ccm ya sasa. Unaweza sema hakikuzaliwa bali kilipatiwa jina jipya lengo lilikuwa kuondoa utofauti wa majina ili kupata nguvu ya umoja.

Hiyo ni tafsiri yako. Mwandishi hakusema hayo, labda unithibitishie kuwa wewe ndio mwandishi wa article hii. Yeye amesema CCM itakufa ikifikisha miaka 50.
 
kaandika kwa hisia zake af anasingizia kuwa ni watu wa ccm.yeye anapandikiza chuki zake kwa jamii baada ya kukosa ile nafasi ya mkugenzi wa habari ikulu kama alivotarajia.Ansbert Ngurumo ukimfahamu wala hakupi shida.

small minds discuss people instead of ideas
 
kwa hiyo ccm na serikali zitakufa kwa sababu hazina hela? mwandishi kilaza jina linamlinda

Mbona unakuwa mvivu wa kusoma na kumwelewa Ngurumo? Nini unachouliza ambacho hajakueleza?
 
kwa hiyo ccm na serikali zitakufa kwa sababu hazina hela? mwandishi kilaza jina linamlinda

Mbona unakuwa mvivu wa kusoma na kumwelewa Ngurumo? Nini unachouliza ambacho hajakueleza?
 
Hiyo ni tafsiri yako. Mwandishi hakusema hayo, labda unithibitishie kuwa wewe ndio mwandishi wa article hii. Yeye amesema CCM itakufa ikifikisha miaka 50.

Mkuu acha kutoka povu na kuleta uongo, ni wapi Ngurumo kasema CCM itakufa ikifikisha miaka 50?
Msome vizuri halafu nukuu hapo mahali.
 
kaandika kwa hisia zake af anasingizia kuwa ni watu wa ccm.yeye anapandikiza chuki zake kwa jamii baada ya kukosa ile nafasi ya mkugenzi wa habari ikulu kama alivotarajia.Ansbert Ngurumo ukimfahamu wala hakupi shida.

Hata wewe huna tofauti na Ansbert Ngurumo,ukinyimwa posho tu nawe utasema hivyo hivyo.
 
Ansbert ana hasira hadi anakosa objectivity kwenye uandishi wake; anywayz wana seminary wengi wamefura wanasubiri padre awe rais..wananchi hawataki wanapeleka hasira zao kwa JK.
 
kaandika kwa hisia zake af anasingizia kuwa ni watu wa ccm.yeye anapandikiza chuki zake kwa jamii baada ya kukosa ile nafasi ya mkugenzi wa habari ikulu kama alivotarajia.Ansbert Ngurumo ukimfahamu wala hakupi shida.
Si kweli hata kidogo! kijana huyu ni great thinker mwenye Tanzania moyoni mwake. Si muoga wala mbabaishaji kama unavyotaka tuamini na ukimsoma katika makala zake kadhaa utagundua ni mtu mwenye uchungu na nchi yake. Hilo la kuteuliwa Mkurugenzi wa Habari Ikulu unalijua wewe, lakni ninavyomfahamu si mtu wa kujipendekeza kama yule jamaa anayetia aibu fani ya uandishi pale magogoni. Nafikiri unamjua. Shame on him!
 
Ansbert ana hasira hadi anakosa objectivity kwenye uandishi wake; anywayz wana seminary wengi wamefura wanasubiri padre awe rais..wananchi hawataki wanapeleka hasira zao kwa JK.

Topical, normally your are topically. Thibitisha ktk article hii ni wapi Ansbert kakosa mashiko. Halafu tuendelee kuupima uelewa wako kisha akili yako.
 
Ansbert ana hasira hadi anakosa objectivity kwenye uandishi wake; anywayz wana seminary wengi wamefura wanasubiri padre awe rais..wananchi hawataki wanapeleka hasira zao kwa JK.
Udini umekujaa mpaka Mndukuni. Bokohalali wee!!
 
kaandika kwa hisia zake af anasingizia kuwa ni watu wa ccm.yeye anapandikiza chuki zake kwa jamii baada ya kukosa ile nafasi ya mkugenzi wa habari ikulu kama alivotarajia.Ansbert Ngurumo ukimfahamu wala hakupi shida.
anapandikizaje chuki kitu alichoandika ni ukweli mtupu. ugumu wa maisha unafanya watu tuwachukie watawala. acha majungu wewe huo ukurugenzi wa habari lini alikuambia anautaka.? unashangaza mimi nilidhani ungekosoa yale aliyoyaandika lakini inaonesha unachuki naye binafsi. mtu anayekukosoa ni mzuri musipende kusifiwa na misifa ya kijinga.
 
ukimjadili mmakonde lazima umjadili na ndonya yake. huwezi kujadili hoja bila kujua kama imetolewa na nani na kwa nini. tunasoma kitabu cha shaban robert cha maisha yangu na baada ya miaka hamsini Ansbert Ngurumo ameandika sana kuhusu serikali na CCM. Ni kweli anaandika kwa hisia kali sana lakini ukweli unabaki kwamba Ngurumo alikuwa na mategemeo makubwa kwenye serikali ya JK ambayo kwa bahati mbaya hakupata
 
sasa hivi Ansbert Ngurumo anaweza kusema lolote. ameshawahi kuandika kwamba ni haki yake kumkashifu, kumsema na hata kumtukana Rais Kikwete na serikali yake. ameshasema hana mtu mwingine wa kumtukana. hasemi wazi lakini kwa vyovyote anafanya kazi ya kumshukuru Mbowe ambaye alimuokoa jalalani na kumpeleka kusoma Uingereza kwa ajili ya kazi ya kuitukana CCM.

anangoja chama cha Mbowe kuingia madarakani ili akumbukwe. Ni lazima asaidie CCM kufa angalau hata kwa maneno. Atangoja sana.
 
Ansbert Ngurumu hajui tofauti kati ya dola ya kirumi ilijiweka na CCM na serikali yake imewekwa kwa sanduku la kura. Utabiri wa Ngurumo sawa na wa Sheikh Arhamu Yahya kwa sababu serikali nyingi duniani kuanzia miaka ya 1929/30 zimekubwa na mtikisiko wa fedha, lakini hazijaanguka kama vile Marekani na Uingereza. Nadhani Ngurumo anasema tu bila kuangalia ukweli. Hivi anafahamu matatizo ya kifedha ya serikali kama ya Zimbabwe au Somalia ambako hatutaki kufika.

Hivi Ngurumo anataka kuwaeleza watanzania kwamba serikali ya CCM ikianguka ni nini kitakachofuata. Ngurumo ashukuru demokrasia pana ambayo inaruhusu mtu afanye hata mambo anavyotaka kama afanyavyo Ngurumo.
 
Si kweli hata kidogo! kijana huyu ni great thinker mwenye Tanzania moyoni mwake. Si muoga wala mbabaishaji kama unavyotaka tuamini na ukimsoma katika makala zake kadhaa utagundua ni mtu mwenye uchungu na nchi yake. Hilo la kuteuliwa Mkurugenzi wa Habari Ikulu unalijua wewe, lakni ninavyomfahamu si mtu wa kujipendekeza kama yule jamaa anayetia aibu fani ya uandishi pale magogoni. Nafikiri unamjua. Shame on him!

Idd Amin Dada yule nduli alipoitwaa Uganda aliipewa majina mazuri mbalimbali kama vile mkombozi, mtu wa watu, mtu mwenye uchungu na Uganda lakini baada ya muda waganda wakalia na kusaga meno wakati wa utawla wake. Moyo wa mtu unatunza siri nyingi ni mapema kumsifu Ngurumo kwamba ana uchungu na nchi wakati hana madaraka yeyote. Ukitaka kujua tabia ya mtu mpatie madaraka.
 
CCM imezaliwa mwaka 1977. Hivi sasa ina miaka 35. Mwandishi anaueleza umma kuwa CCM bado itakuwa na nguvu kwa miaka mingine 15 mpaka itakapotimiza miaka 50. Si haba...

Hapana Mkuu, Ngurumo anaposema miaka 50 ya CCM ana maanisha CCM ile iliyorithi mirathi ya TANU. Ndiyo tunakubali CCM ilizaliwa 1977 lakini ni muendelezo wa TANU. Ndiyo maana mwenyekiti aliyekuwepo TANU ndiyo yule yule aliendelea kuingoza CCM, hata wajumbe wengi wa vikao vikubwa vya TANU (Mfano Mkutano Mkuu, Halmashauri Kuu na Kamati kuu) weliendelea kuwa wajumbe wa vikao hivyo hivyo vya CCM!
 
Back
Top Bottom