Anguko la January Makamba


ungeandika kwa kiswahili tu mkuu.
 
Ni hatari sana kuwa na viongozi WANAFIKI KAMA JANUARY MAKAMBA!MSOCHA kamfundisha tabia mbaya!
 

huyo ni mtoto wa mama,kwanza ubunge amepata kutoka na mzee wake alikuwa na kijinafasi kwny chama.sasa hakisema ukweli sianajua watampiga chini kwny ubunge next yr.kwanza fara tu!
 
Last edited by a moderator:

Hoja yako ni nini hasa; unapingana na intention, process au outcome?
 
 
Mimi sijawahi kumweka kwenye list ya viongozi watarajiwa wa nchi hii

same to me brother.Yaani ukoo wa Makamba,aghhh,watanzania bongo lala sana,huyu jamaa hakuna kitu utozi tu .
 
 
Mazingira kitu gani? Simtetei mtu wala simpingi mtu hapa. Hayo hayo mazingira?ya Makamba angewekwa mtu hapa angeanza kujinyea the same. Zitto yuko huru kwa kuwa yupo upande wa kukosoa. Hivi cdm ndio ingekuwa madarakan halafu ikawa inaborongai mnadhani haya makeke ya Zitto mngeyasikia? Mnadhani Makamba angechukua uamuzi sawa na Zitto? Sitaki kuamini kuwa JM hana uzalendo. Halafu kwa nini JM peke yake? Lazima mjiulize maswali kwanza kabla ya kuanza kuhukumu.

Bado JM ni kiongozi mzuri pale atakapopata mfumo mzuri. Anaweza kutofautiana na Zitto kwenye njia ya kufikia suluhu lakini wakawa na nia moja ya kufikia suluhu. Hii inadhihirisha kuwa hakuna njia moja ya kufikia suluhu. Ni jambo rahisi tu kuelewa kuwa si rahisi kiivyo kuanza kukosoa kwa uwazi kama Zitto mfumo uliokulea tangu mtoto hadi kuwa kiongozi ndani ya huo mfumo. Na badala ya kumlaumu mtu mmoja tena kupitia keyboard, tungeinngia mitaani kudhihirisha hili lakini hiyo courage hatuna! So let them disagree on methods but still have a common goal!
 
JM peke yake kwa sababu alitupa tumaini kwamba anaweza kuibadilisha ccm ikawa kipenzi cha watanzania
elewa hapa ishu sio chama gani madarakani bali ni NAMNA GANI HICHO CHAMA KITATUFAA
Kwa upande wa ccm JM alikuwa kioo na sasa kachafuka tena UHARO
 
huyo kijana anatamani uwaziri nishati na madini mnafiki tu.

huyo ni mnafiki tu hawezi piga kelele kuhusu mabovu ya tanesco kisha tukimwambia tuwawajibishe watendaji wabovu
anasema ican disagree with zito tusimsikie tena akipiga kelele.
 
January amejaa nidhamu ya uoga hana ujasiri hata chembe
 
Jamani mtoto wa nyoka sinyokatuuuuuuuu.kwanzahuyu jamaa nimnafiki na anajua kilakitu maana lakemtu harimtapishi kumbuka alikuwa muandishi wa rais hivyo amekulakodizenu vyakutosha maana alikuwa na vascodagama.huyo mtoto nihovyo sanaaaaaa hovyoka bisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Ni zao halisi la mfumo wa siasa za CCM sitarajii kitu cha ajabu sana kutoka kwake. Hata kama anatamani kuwa kama walivyo vijana wenzake walioko upinzani hawezi kupata nafasi na uhuru wa kutosha 'yupo ndani ya geti'
 

Ni kosa kumlinganisha Mhe.January Makamba na Mhes.Zitto Kabwe. Historia zao ni tofauti na maono yao vilevile. Kumlinganisha January na Zitto nikutomtendea haki Zitto. Hii ni kutokana na maono ya Zitto, akiwa kijana aliamua kujiunga na upinzani na baadae kugombea ubunge. Aligombea ubunge akiwa masikini na kwahiyo hakutumia fedha kupata uongozi/ ubunge. January alitumia vitendo vya rushwa kumchafua Mzee Shelukindo. Alimchafua sana Mzee Shelukindo, alimtishia sana mzee huyu bila sababu ya msingi. Hakuwa mstaarabu hata kidogo, hakumuonyesha heshima kutokana na umri wake. Zitto ana adabu sana na kasoro kidogo zinazoonekana kwa Zitto, nyingine zinachangiwa na umri wake mdogo.
 
Unajua katika uongozi, kuna kitu kimoja muhimu sana, kuwa na dhamiri ya kuutumikia umma. Extreme case ni kama zile za akina Mandela, Sokoine, na Mahatma Gandhi. na utaona kuna tabia uongozi zao zinachukuliwa sana na viongozi kama akina Dr wa ukweli, Zitto, Mnyika, Fipinjombe na wengine. Uoga unaotokana na kupoteza nafasi yako katika uongozi kwa namna yeyote ile ni mgongano wa kimaslahi katika sifa za kuwa kiongozi (Egoistic). wengi wanawinda nafasi za juu, wengine wanaogopa kupoteza uongozi. Hhii inawaondoa kabisa katika zile sifa walizokuwa nazo akina mzee mandela. Lemma yeye kaamua, lakini Makamba J, bado sijamuamini.

Opportunist is a very dangerous ruler and he is never regarded as a leader. Akina Makamba na Nape na wengine wa aina hii, umma unatakiwa kuwaangalia kwa jicho la kiuchunguzi zaidi. katika nchi hii kuna viongozi waliomzunguka Nyerere na kujifanya wajamaa kama akina Ki*****e, lakini Mwalimu alipotangulia, wakageuga kuwa Mapepari wakubwa.

Naunga mkono hoja.
 
 
january hana kitu ila tu anataka madaraka akisha pewa ndo atalala usingizi wa pono msimkubali kabisa jamani
 

mpaka watoke. we want it now. they are just vuvuzelas period.
 
Februari, Machi, Aprili, Mei, Juni, Julai, Agosti, Septemba, Oktoba, Novemba, Desemba. Chagua jina la mwezi mwingine badala ya Januari. So far, Januari imeshapita; labda kama mnaongelea habari za miaka ijayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…