Anguko la CHADEMA nani alaumiwe?

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Hakuna siri tena lile anguko la CHADEMA ambalo lilitabiriwa tangu Dkt. Slaa afanyiwe figisu na kuhama CHADEMA sasa limetimia.

Kiuhalisia lazima aliyesababisha anguko hili Watanzania wanatakiwa kumfahamu maana kuna watu walijitolea mali,muda na uhai wao sababu ya hiki chama.

Kuna watu wamepigwa risasi,walilipuliwa na mabomu huko Arusha na hata kuna watu walipoteza uhai kama Marehemu Daud Mwangosi.

Alaumiwe Mwenyekiti kwa kushindwa kusimamia Chama vizuri? Alaumiwe Mwenyekiti kwa kumkaribisha Lowassa? Alaumiwe Mwenyekiti Mbowe kwa matumizi mabaya ya pesa ya Chama? Walaumiwe wanachama ambao wanamuogopa Mwenyekiti wao kumkosoa hata akifanya makosa?

Uchaguzi umeisha, CCM imeshika dola,wapinzani mjipange kwa Uchaguzi wa mwaka 2050. Maana kwa sasa kuig'oa CCM hii makini inayotekeleza ahadi zake kwa wananchi ni ngumu kuiangusha.
 
Hakuna siri tena lile anguko la CHADEMA ambalo lilitabiriwa tangu Dkt. Slaa afanyiwe figisu na kuhama CHADEMA sasa limetimia.

Kiuhalisia lazima aliyesababisha anguko hili Watanzania wanatakiwa kumfahamu maana kuna watu walijitolea mali,muda na uhai wao sababu ya hiki chama...
Viongozi najua yapo Mambo mengi na mda ni mchache but mungu anajua chadema sio majengo bali ipo moyoni mwa watu
So tafadhali Sasa njoo na mpango chadema familia nchi nzima lengo kufanya wanachadema kuwa na umoja na mshikamano katika shida na raha wakati Mambo mengine inaendelea najua Kuna kipindi mlikua MNAFANYA hivi Sasa uimarisheni zaidi na uanze utekelezaji Mara moja mpaka kwenye vijiji ,chadema haiwezi kufa leo au kesho
 
Mnajifariji baada ya kutumia dola kubaki madarakani!CDM haiwezi kufa kirahisi namna hiyo,labda mtutoe roho zetu!

Mmeshinda uchaguzi kwa kutumia mabavu,ni wakati wa kutekeleza mliyoahidi!
*Ajira
*Bima ya Afya kwa watu wote
*Nyongeza ya mishahara
*Kuboresha maisha ya watu

Maeneo hayo wananchi watayapima!
 
Kikwete_mbowe.jpg


Hapo anawaza ''huyu mtu atanitambua siku nikikalia kile kiti'' hahaaha
 
Viongozi najua yapo Mambo mengi na mda ni mchache but mungu anajua chadema sio majengo bali ipo moyoni mwa watu
So tafadhali Sasa njoo na mpango chadema familia nchi nzima lengo kufanya wanachadema kuwa na umoja na mshikamano katika shida na raha wakati Mambo mengine inaendelea najua Kuna kipindi mlikua MNAFANYA hivi Sasa uimarisheni zaidi na uanze utekelezaji Mara moja mpaka kwenye vijiji ,chadema haiwezi kufa leo au kesho
Huko ni kujipa moyo au?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom