Anguko kuu la CHADEMA

Anguko kuu la CHADEMA

Mbona kama unatufokea tukubali unachosema haya ni kweli kitasambaratika na akifuati sheria ya natural justice na ni cha ajabu sana ingawa ulikipenda sasa si ufurahi nini kutufokea
 
Pengine wewe ndiyo utaanguka, Chadema Ni chama pekee katika ukanda huu wa Afrika Mashariki inayopambana na vitisho vya Kila aina lakini bado inapumzi ogopa. Polisi, nadhani unawaelewa vizuri, wameifanya watawala wasilale usingizi.

Wewe Kama unataka kupima uwezo wa Chadema Mbowe aongee tu utawasikia viongozi wale wasiotulizana wakikimbizana kumjibu. Sasa hivi Gwajima naye ameachana kumnanga shetani na kugeukia kulaani Chadema. Nenda polisi useme Chadema Wana mkutano utaona magari ya washa na hata Yale mabovu yakitumuka mbio halafu eti useme anguko!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utaanza kuanguka wewe kabla ya CHADEMA si umeona Wassira alisema CHADEMA itakufa ameanza "KUFA' yeye kabla ya CHADEMA,
 
Chadema ni genge la wakora likiongozwa na Mbowe ,ni wakuogopwa kama ugonjwa wa ukoma ,hili genge lidisapie tu hata kwa kuvunja sheria za nchi ,likiachwa madhara yake ni makubwa sana kwa taifa

Sent using Jamii Forums mobile app
Inabidi msajili wa vyama vingi aliangalie hili suala kwa mapana na kwa maslahi ya Jamii.
 
Hivi ukimkataza mtoto wako asifanye jambo fulani halafu yeye akiwa na alili zake timamu kabisa akafanya, wewe kama mzazi utatoa muda wako umsikilize kwanini amefanya?

Hao wabunge baada ya kukatazwa ni kwanini wasinge protest pale pale kuonesha hawajaridhika na maamuzi ya kuwazuia wasiende bungeni? Tafsiri inayokuja hapo ni kwamba wamekaidi agizo halali la chama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kikundi, kusanyiko ama jumuia yoyote lazima iwe na miiko, misingi na itikadi zake...

Na huwezi kwenda kinyume au kuivuruga kwa makusudi ama kwa manufaa yako halafu uachwe hivi hivi...
Ukiona unaachwa bila kuwajibishwa ujue hiyo jumuia ni sawa na mfu!

Hapa mtaongea sana lakini ifahamike wazi kuwa unakuwa huru unapokuwa mtu peke yako...!!
Ukishaamua kujiunga na watu fulani lazima vigezo na masharti vizingatiwe...!!

Unapolalamikia vitu ambavyo viko wazi ndani ya jumuia yenu tena kwa wasio wanajumuia inaonesha wazi kuwa wewe kama mwanajumuia ndo una matatizo makubwa sana ya akili na maadili...!!

Anyway politicians karibia wote ni con-artists... Usiwaamini na wala usiweke matarajio makubwa sana juu yao...
 
Jipu la jirani linapokukera,lini ccm watajenga nchi bila kukumbuka timbwili za upinzani?

Jenga uchumi imara,miundombinu ya usafiri, afya, elimu, maji na kuwe na usalama wa watu kutoa maoni....
Uone huo upinzani utaanzaje kuwatisha.

Kwa hali hii hata mwana CCM akivaa nguo yenye rangi zinazoshabihiana na za vyama vya upande huo, mashavu yatawajaa bila hata sababu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani mtu akitoa mawazo yake yasipowafurahisha basi kalipwa buku saba...Hadi Lijualikali alilipwa buku saba!!! Hakuna anayekubali kukandamizwa na kulazimishwa kufanya vitu ambavyo sio ilhali uhalisia anauona. Msipobadilika mbona mtaita kila mTz buku saba.

Naona kuelekea uchaguzi mkuu mmejazwa humu ndani kujibu mashambulizi, lakini hali yenu itakuwa ngumu sana.
 
Naona kuelekea uchaguzi mkuu mmejazwa humu ndani kujibu mashambulizi, lakini hali yenu itakuwa ngumu sana.
Sasa si unaona mawazo yenu yalivyo...mtu akiwa against nanyi katumwa...kwamba huwa mnatenda kwa usahihi siku zote...Mtazamo mbovu kabisa
 
Habari ya asubuhi wanabodi?

Ni tumaini langu kwamba tuko salama na tunaendelea kupambana katika kulijenga taifa letu.

Ndugu wanabodi katika kuendelea na mapambano ya kulijenga taifa letu nawaomba sana msijisahau kujilinda na ugonjwa wa COVID-19. Tuendelee kuchukua tahadhali na kuwa waangalifu wa hali ya juu.

Wanabodi wa JF, kama kichwa cha uzi huu kisemavyo hapo juu ni kwamba CHADEMA ni chama cha ajabu sana kwani kimeshindwa kusimamia misingi ya demokrasia na haki asilia(Natural justice). Kwa mantiki hii CHADEMA mwaka huu imejichimbia kaburi bila kujijua.

Wanabodi, CHADEMA ni chama ambacho kinahubiri demokrasia na wakati mwingine huwa wanenda mbali zaidi na kumtuhumu mheshimiwa Rais wa JMT kwamba ni dikteta, hapendi ushauri n.k ila kwa kipindi hiki CHADEMA imedhihirisha ni jinsi gani walivyo wanafiki, wazandiki na madikteta kutokana na matendo ya mwenyekiti wao.

Wanabodi, CHADEMA kuwafukuza wabunge wake bila kuwapa haki ya kuwasikiliza wanatuonesha picha gani sisi wananchi wa kawaida?

Wanabodi, CHADEMA kutoa amri kwa wabunge wake wasiingie bungeni na kukataa kueleza lengo la hiyo amri na sababu za msingi za kufikia huo uamuzi wa kutokuingia bungeni na kutowashilikisha wabunge wake katika hilo jambo, je inaleta picha gani kwa wananchi wa kawaida na wanachama wake?

CHADEMA, kuwakata wabunge mishahara yao kwa ajili ya kuanzisha akaunti maalumu ambayo itawasaidia wabunge hao katika kampeni pale ambapo watakuwa wamekwama na kutumia hiy o hela kinyume na makubaliano ya wanufaika(wabunge wa CHADEMA) inaleta picha gani kwa jamii?

WanaCHADEMA ile demokrasia, utawala wa sheria na haki asilia ambayo mmekuwa mkihubiri bungeni, kwenye mitandao ya kijamii iko wapi katika chama chenu? Kwanini mnapenda kuwanyooshea wezenu vidole kwamba wao ni wachafu wakati nyie ndiyo wachafu wakuu, wazandiki na wanafiki wakubwa?

Kwa mantiki hiyo, mkipewa dhamana ya kuongoza nchi yetu mnataweza kweli? Kama mambo mmeshindwa kutekeleza katiba yenu pamoja na katiba ya JMT mtawezaje kuongoza nchi?

Mwaka 2005 nilitokea kuipenda sana CHADEMA kwani ilikuwa na watu wenye uwezo mkubwa sana katika mambo ya kisiasa. Waliposimama kutoa hotuba/hoja hakika ni watu ambao walionesha uwezo, ukomavu na weledi katika siasa. Ila kutokana na udikteta wa DJ umesababisha anguko kubwa sana la CHADEMA. Wale watu wote wameanza kuikimbia CHADEMA kwani inaongozwa na mtu ambaye siyo sahihi. Siku zote ni ngumu sana mtu mwenye akili ndogo kumuongoza mtu mwenye akili kubwa na ndiyo maana Dr. slaa, Zito Kabwe na wenzake waliondoka mapema CHADEMA kwani waliona mbali sana kama mnabii.

Mwisho, CHADEMA acheni unafiki wenu. Unafiki ni jambo baya sana katika Dunia hii. Kama mnafikiri wananchi hawaoni mnachofanya nawapa pole sana. Kwa sasa wananchi tupo makini sana. Sijui kwa mwaka huu matakuja na sera gani za kuwashawishi wanachi.

Ahsanteni na karibuni kwa michango.
Nenda kawaulize watabiri wenzako wa kifo cha Chadema, tangu walipoanza kutabiri miaka mingi iliyopita je ,Chadema imekufa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari ya asubuhi wanabodi?

Ni tumaini langu kwamba tuko salama na tunaendelea kupambana katika kulijenga taifa letu.

Ndugu wanabodi katika kuendelea na mapambano ya kulijenga taifa letu nawaomba sana msijisahau kujilinda na ugonjwa wa COVID-19. Tuendelee kuchukua tahadhali na kuwa waangalifu wa hali ya juu.

Wanabodi wa JF, kama kichwa cha uzi huu kisemavyo hapo juu ni kwamba CHADEMA ni chama cha ajabu sana kwani kimeshindwa kusimamia misingi ya demokrasia na haki asilia(Natural justice). Kwa mantiki hii CHADEMA mwaka huu imejichimbia kaburi bila kujijua.

Wanabodi, CHADEMA ni chama ambacho kinahubiri demokrasia na wakati mwingine huwa wanenda mbali zaidi na kumtuhumu mheshimiwa Rais wa JMT kwamba ni dikteta, hapendi ushauri n.k ila kwa kipindi hiki CHADEMA imedhihirisha ni jinsi gani walivyo wanafiki, wazandiki na madikteta kutokana na matendo ya mwenyekiti wao.

Wanabodi, CHADEMA kuwafukuza wabunge wake bila kuwapa haki ya kuwasikiliza wanatuonesha picha gani sisi wananchi wa kawaida?

Wanabodi, CHADEMA kutoa amri kwa wabunge wake wasiingie bungeni na kukataa kueleza lengo la hiyo amri na sababu za msingi za kufikia huo uamuzi wa kutokuingia bungeni na kutowashilikisha wabunge wake katika hilo jambo, je inaleta picha gani kwa wananchi wa kawaida na wanachama wake?

CHADEMA, kuwakata wabunge mishahara yao kwa ajili ya kuanzisha akaunti maalumu ambayo itawasaidia wabunge hao katika kampeni pale ambapo watakuwa wamekwama na kutumia hiy o hela kinyume na makubaliano ya wanufaika(wabunge wa CHADEMA) inaleta picha gani kwa jamii?

WanaCHADEMA ile demokrasia, utawala wa sheria na haki asilia ambayo mmekuwa mkihubiri bungeni, kwenye mitandao ya kijamii iko wapi katika chama chenu? Kwanini mnapenda kuwanyooshea wezenu vidole kwamba wao ni wachafu wakati nyie ndiyo wachafu wakuu, wazandiki na wanafiki wakubwa?

Kwa mantiki hiyo, mkipewa dhamana ya kuongoza nchi yetu mnataweza kweli? Kama mambo mmeshindwa kutekeleza katiba yenu pamoja na katiba ya JMT mtawezaje kuongoza nchi?

Mwaka 2005 nilitokea kuipenda sana CHADEMA kwani ilikuwa na watu wenye uwezo mkubwa sana katika mambo ya kisiasa. Waliposimama kutoa hotuba/hoja hakika ni watu ambao walionesha uwezo, ukomavu na weledi katika siasa. Ila kutokana na udikteta wa DJ umesababisha anguko kubwa sana la CHADEMA. Wale watu wote wameanza kuikimbia CHADEMA kwani inaongozwa na mtu ambaye siyo sahihi. Siku zote ni ngumu sana mtu mwenye akili ndogo kumuongoza mtu mwenye akili kubwa na ndiyo maana Dr. slaa, Zito Kabwe na wenzake waliondoka mapema CHADEMA kwani waliona mbali sana kama mnabii.

Mwisho, CHADEMA acheni unafiki wenu. Unafiki ni jambo baya sana katika Dunia hii. Kama mnafikiri wananchi hawaoni mnachofanya nawapa pole sana. Kwa sasa wananchi tupo makini sana. Sijui kwa mwaka huu matakuja na sera gani za kuwashawishi wanachi.

Ahsanteni na karibuni kwa michango.
How much are you paid for such a nonsense ?
 
Hizi ramli ziliasisiwa na mzee Wasira, nyie wengine fuata upepo tu.
Toka hizi porojo zisemwe ni muda sasa lakini CDM ipo tu. Itoshe tu kusema kuwa cdm ni chama kubwa na haliwezi kuisha. Wanatoka lakini lipo tu,hata kama hukipendi lazima ukikubali tu
 
Back
Top Bottom