Balaa tupu! Utu na ubinadamu vimebaki kuwa historia miongoni mwa wa watanzania wengi, maadili ya babu zetu sasa zatiwa kapuni, na wala hakuna anayethubutu kuziendeleza, pia hata hofu ya mwenyezi mungu sasa nayo imepungua, watu wanafukuzana kutenda dhambi na uhalifu wa kila namna ili tu wapate kuziridhisha nafsi zao huku wakiangamiza maelfu. Hii ndiyo tanzania ya leo, maskini hathaminiwi tena, watawala na wenye navyo leo ndio habari inayozungumzwa mjini, makabwela ili kupata haki yao ni lazima kitu kidogo, ahaaha! Nauliza watanzania wenzangu hii habari ya kitu kidogo ililetwa na pepo za kutoka upande gani? Mara utasikia oh niandalie maji ya kunywa je? Haya maji wanataka lita ngapi?
Watanzania tubadilike, tuache ujanjaujanja na wizi, uonevu, rushwa pamoja na tabia zingine chafu .