Angalia unafiki wa Profesa Lipumba

Angalia unafiki wa Profesa Lipumba

‘Ni kweli nilishiriki kumkaribisha Lowassa UKAWA lakini dhamira na nafsi yangu inanisuta… Tumekaribisha watu wa CCM ambao waliipinga Rasimu ya Katiba, najiuliza tutaweza kusimamia malengo ya UKAWA‘
Mtoa mada unatoka Povu la nini wakati senetensi ya juu umei quote mwenyewe iko clear kabisa,ulitaka aongee nini zaidi ya hiko.

EL hakuwahi kuchangia Bunge Maalum la Katiba, hivyo msimamo wake ni kundi aliopo (UKAWA).
SIJUI ANAONGELEA WATU WAPI?
 
Hii ni sawa na Shehe kujiuzuru na kuwa muumini wa kawaida kisa kamsilimisha askofu aliyekuwa anaupinga uislam, sababu eti nimefanya makosa kumkaribisha mtu aliyekuwa anapinga uislam. Hata mtume Paulo,zamani akiitwa Sauli alikuwa katili zidi ya Ukristo hata kuua wote waliokuwa wanahubiri injili, lakini alivyobadilika na kuitwa Paulo alifanya kazi kubwa ya kueneza Injili na hata kuandika vitabu kadhaa vya Injili. Wakristo wa enzi hizo wangekuwa na akili kama za Lipumba wangemkataa Paulo.
Mifano ya dini na siasa are irrelevant,hili kosa huwa mnalirudia mara kwa mara
 
Katiba mpya ya wananchi haitopatikana kwa kuwakataa walioipinga bali ni kwa kuwachukua ili ndio watoe ukwel kwa wananchi dhamira mbaya ya maccm juu ya mchakato wa katiba mpya!
Ukweli wa dhamira mbaya tunaujua tayari,ukweli ambao hatuujui ni dhamira ya Lowassa
 
Tatizo mnadhani kila mwana Ukawa ni teamLowasa!
Mmechemsha sana!
Lowasa siwezi kumpigia kura hata iweje!
 
Mpaka sasa angalia mnufaika mkubwa wa UKAWA ni CHADEMA. Wengine wasindikizaji tu, hawana chao zaidi ya kutegemea huruma.


Lowassa ndio mnafiki na tapeli mkubwa. Kulikuwa hakuna haja Ya yeye kuchukua fomu ya kugombea urais akiwa CCM kama alitaka mabadiliko ya mfumo. Angetoka mapema sio mpaka akatwe

Watu wengi mnaongea bila kujua haya mambo yote ni ya kisiasa na mjue kama siasi inajengwa na unafiki. Asiyekua mnafiki ndani ya siasa huyo ni bora akaachana nayo. Usione vyama vyote vinavyounda Ukawa kama nia yao ni moja hapana, kwani ingekua hivyo wangewa wote wameunda chama kimoja wakakisajili kama chama cha ukawa. Ila hapo walipo wengine dans nia ya kudhofishana wao kwa wao na ndiyo mkenge ambao chadema wameingizwa na wenzao kwa kumfagilia Edo. kinacho fanyika ni kuipunguzia CDM uaminifu kwa watz ili kiburi cha wanacdm kishuke cha kujiona wao ndo chama tu cha upinzani TZ na tayari malengo yameshatia. Kuwa na MTU njia moja hahina maana ya wote mnaenda sehemu moja..

Wakuu mko sahihi kabisa, Lipumba nilikuwa namwita Profix baada ya baadhi ya kauli alizowahi kuzitoa huko nyuma lkn kwa hili nimeamini ni Prof kamili. Wanufaika wakuu hapa ni wale wale wenye uchu wa madaraka Lowassa na Seif Hamadi. Lowasa anataka awe Rais wa muungano kwa gharama zozote na Seif anataka kura za Lowasa Z'bar ili awe rais wa Zanzibar - anajua kabisa Lowasa hapati lkn yeye lengo lake litimie tu. Kwa kufanya hivyo anaiua CUF Huku Bara, kwani kwa juhudi za Lipumba angalau CUF ilipata wabunge 2 ama mmoja Bara na makubaliano yalikuwa kuwa LS awaunge mkono na wala siyo kugombea alitakiwa agombee Lipumba kwa ajili ya kuweka balance na kupata kura za watu fulani - sitaenda ndani zaidi.Lipumba kapima akaona hapana, na hii inakubalika kwani kama utakuwa unaenda mahali ukakuta kuwa njia unayoitumia siyo sahihi unahaki ya kubadili mwelekeo.
 



tazama boy language ya hiyo picha, inaonesha wazi kabisa lowasa analazimisha kumkumbatia professor lipumba na lipumba dhamira inamsuta, anamsukuma mikono lowasa bila kujijuwa na hata sura ya lipumba kwenye hiyo picha inaonesha yupo mbali kabisa na hayupo hapo, hata hiyo "smiling" ni wazi kabisa kuwa ni "plastic". Linganisha na hii...

11825845_1479232079065071_2826414531389383064_n.jpg

acha kutu danganya hivi hata picha huoni japo kusoma ni mgogoro
 
tatizo mnadhani kila mwana ukawa ni teamlowasa!
Mmechemsha sana!
Lowasa siwezi kumpigia kura hata iweje!
sasa toka lini wewe mwana c.c.m ukampigia kura kamanda lowassa wa ukawa?
 
Hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumi katika siasa. Bila ya matukio kama haya hiyo maana ya siasa haijatimia jamani!!!
 
Kwa maneno mengine Lipumba anatuambia hamwamini Lowassa. Lakini anakiamini chama kinachomwamini Lowassa na atakuwa mwanachama wa hiki chama mpaka mwaka 2020. Ni miaka mitano ya kusutwa na dhamira yake kila mara jina la Lowassa litakapotajwa ndani ya CUF. Kama kweli anaiheshimu dhamira yake ilipaswa ajiuzulu na uanachama.

Mwenyekiti mzima mwenye dhamana ya chama unapelekeshwa mpaka kuja kushtuka kipenga kimeshalia. Asitufanye sisi watoto, iko kitu anakificha hataki kueleza ukweli.
 
Hapa ilikuwa meza kuu, yuko Freeman Mbowe (CHADEMA), Edward Lowassa (CHADEMA) na Prof. Lipumba (CUF)
Ulimwengu wa Siasa Tanzania August 06 2015 umepokea headlines nyingine zenye uzito ambapo aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba ametangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti wa Chama hicho. Sentensi nyingine amesema hivi >>> 'Taarifa ya kung'atuka niliitoa August 01 2015, nilisubiri kukamilisha masuala ya UKAWA ndio nitoke… Ninaendelea kuwa Mwanachama wa CUF na nimelipia Kadi ya Uanachama mpaka 2020, sina mpango wa Kujiunga ACT'-Prof. Lipumba.Hapa nina pichaz nyingine Kumbukumbu ya July 28 2015 siku Edward Lowassaalivyokaribishwa rasmi CHADEMA na UKAWA.
Lowassa na Mama Regina Lowassa wanakumbatiana, pembeni yao niProf. Lipumba.

Edward Lowassa na Prof. Lipumba walikuwa wamekaa karibu kwenye meza kuu muda wote.

Edward Lowassa na Prof. Lipumba kuna wakati walikumbatiana.
Kuwa profesa si kuwa na akili, ni kuweza kufanya tu kitu kidogo mno kwa usahihi
 
Baba rizmoko alimuingiza chaka polofesa kuwa chama chakavu lishinda atapewa ulaji sasa kaona kinyume chake ndiyo anageuka sakala anahangaika.
 
&[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Ni kweli nilishiriki kumkaribisha Lowassa UKAWA lakini dhamira na nafsi yangu inanisuta&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG]; Tumekaribisha watu wa CCM ambao waliipinga Rasimu ya Katiba, najiuliza tutaweza kusimamia malengo ya UKAWA&[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];
Mtoa mada unatoka Povu la nini wakati senetensi ya juu umei quote mwenyewe iko clear kabisa,ulitaka aongee nini zaidi ya hiko.
Maamuz ni ya chama na si mtu mmoja. Kama chama bado hakijajitoa ukawa, anarud ongeze chama chenye sera tofaut na yéyé?? Anatumika bila kuulizia
 
Amakweli profesa anatoa kali ya siasa. Kwavile kalipia kadi ya uanachama ndo asifukuzwe cuf ?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom