mriringa
JF-Expert Member
- Jan 17, 2017
- 783
- 835
Miaka ya nyuma akili yangu iliwaza kwamba tajiri ni mtu mwenye fedha za kutosha na sikuwahi kuwaza kwamba tajiri mbali na kuwa fedha ila anaongozwa na umiliki wa asset za kutosha.
Tajiri anayemiliki ardhi ya kutosha na ndani yake akaweka mazao ya muda mrefu Hadi kuvuna ni tajiri mwenye maono makubwa na mara nyingi huchekwa kama wametupa fedha zao. Fedha ikikaa bila kuzaliana Haina maana.
Ninachotaka kusema ni kwamba vijana ni muda Sasa wa kuwaza kumiliki ardhi walau usiwe na chini ya eka 10+ na hakikisha unamiliki kisheria na panda miti ya mbao au matunda na uitunze kama mboni ya jicho lako.
Nilimchukia sana baba yangu kumiliki ardhi zaidi ya eka 100 kipindi mdogo na niliona anajitesa wakati ni mtumishi na anakula mshahara mkubwa tu ila Sasa Kila mwaka anauza viwanja zaidi 50 katika umri wake wa miaka 80 kasoro na hahitaji msaada wowote kutoka kwa watoto wake maana anajiweza kuliko hata sisi watoto wake.
Wakati unaofaa ni sasa na usichague wapi ununue ardhi bali popote inapopatikana ardhi na mfukoni fedha ipo usichelewe kuiandaa kesho Yako ili kuepuka kuja kuwalaumu watoto wako kwamba hawakusaidii.
Mimi nimeamua ni wakati wako eeh mpendwa kuamua Sasa kumiliki ardhi ya kutosha maana Kuna mikoa ardhi bado haiuzwi gharama kubwa.
Tajiri anayemiliki ardhi ya kutosha na ndani yake akaweka mazao ya muda mrefu Hadi kuvuna ni tajiri mwenye maono makubwa na mara nyingi huchekwa kama wametupa fedha zao. Fedha ikikaa bila kuzaliana Haina maana.
Ninachotaka kusema ni kwamba vijana ni muda Sasa wa kuwaza kumiliki ardhi walau usiwe na chini ya eka 10+ na hakikisha unamiliki kisheria na panda miti ya mbao au matunda na uitunze kama mboni ya jicho lako.
Nilimchukia sana baba yangu kumiliki ardhi zaidi ya eka 100 kipindi mdogo na niliona anajitesa wakati ni mtumishi na anakula mshahara mkubwa tu ila Sasa Kila mwaka anauza viwanja zaidi 50 katika umri wake wa miaka 80 kasoro na hahitaji msaada wowote kutoka kwa watoto wake maana anajiweza kuliko hata sisi watoto wake.
Wakati unaofaa ni sasa na usichague wapi ununue ardhi bali popote inapopatikana ardhi na mfukoni fedha ipo usichelewe kuiandaa kesho Yako ili kuepuka kuja kuwalaumu watoto wako kwamba hawakusaidii.
Mimi nimeamua ni wakati wako eeh mpendwa kuamua Sasa kumiliki ardhi ya kutosha maana Kuna mikoa ardhi bado haiuzwi gharama kubwa.